Extroverted Introvert
JF-Expert Member
- Aug 18, 2022
- 599
- 1,565
Hata Gsm ni mtengeneza jezi,, au mmesahau ni nyie mnasemaga Gsm anachukua pesa zote ila yanga anapewa 1000 kwa kila jeziHao ndo Main Sponsors wa hizo Clubs tajwa?
Wengine hapo naona kama watengeneza Jezi vile......
Ana wenge la kufa mtu! N April anakandwa 5G tena!Huyu mzee ana zeeka vibaya,,,hii yote imekuja baada ya kichapo cha 5.
Tatizo linakuja Mkurugenzi wa Miradi wa GSM ni Rais wa Yanga.GSM ni mmilki wa Yanga au ni mdhamini? Kama ni mdhamini tu mgongano wa maslahi unatoka wapi?
Tuangalie wenzetu wanafanyaje kuhusu sonsorship na ownership. UEFA kwa mfano wanaruhusu mtu mmoja au kampuni moja kuwa kit sponsor kwa zaidi ya timu moja lakini hawaruhusu mtu mmoja kumiliki timu zaidi ya timu moja kwenye mashindano yao ingawa kuna dalili wanaweza kulegeza msimamo huo.
Shirt sponsor hahusiki na day to day running of the club.
GSM is only a shirt sponsor wa hizo timu sita not the owner. Kwa nini watu wanaweweseka.
Kuna kitu amvacho kila mtu anajua kwamba Simba ana matawi yake(timu). Kwa mfano kila mtu anajua Coastal Union ni tawi la Simba lakini wamekaa kimya. Ni lini Coastal Union iliifunga Simba? Lakini katika mechi nne zilizopita Ihefu kaifunga Yanga mara mbili. Msimu huu ndiyo timu pekee iliyoifunga Yanga. Swali la kujiuliza why now? Tumuulize Jemedari Said.
unashangaa nini,wakati azam inafadhili timu zote ligi kuuNyaraka ya malalamiko makali, ya wanaojiita wadau wa utetezi wa usawa katika ligi kuu, imenaswa na Times Digital, ikiwa na maneno makali na yenye hisia kali.
Kwa ufupi imeanza kwa kujieleza namna hii.
KUMB:
Ombi la Haraka la Uchunguzi wa Ushindani wa Haki katika Ligi Kuu ya NBC
Mpendwa Mheshimiwa/Bibi,
Tunakuandikia kukuletea jambo linalotia wasiwasi mkubwa kuhusu uadilifu na usawa wa Ligi Kuu ya NBC nchini Tanzania.
Kama wadau na watetezi wa usawa katika nyanja ya soka, tunaamini ni muhimu kushughulikia masuala yanayoweza kuhatarisha uadilifu wa ligi.
Imefahamika kuwa mmoja wa wanahisa wa klabu ndani ya Ligi Kuu ya NBC pia anafadhili vilabu vingine sita vya ligi hiyo hiyo.
Klabu hizo ni pamoja na Namungo, Coastal Union, Ihefu, Tanzania Prisons, Singida Fountain Gate, na Young Africans, zote zikifadhiliwa kupitia kampuni tanzu au ubia wa chapa.
NIMECOPY KWA BARAKA MPENJA
Udhamini wa GSM na AZAM ni tofauti usijizime dataAzam wanadhamini timu zote za ligi kuu, GSM anatakiwa aongeze timu za ku dhamini zifikie 16.
Hakuna utofauti wowote ila ukiamua ku utafuta utaupata.Udhamini wa GSM na AZAM ni tofauti usijizime data
Ningeiona barua ningeamini coz sitaki kukubali kama Jemedari amekua mpuuzi kiasi hiki.
Pia angeanisha kwa huo udhamini wa timj nyingi nani ni mnufaika na kwa namna gani?
1. Miaka kadhaa nyuma Sportpesa walidhamini simba na yanga, pia nadhani bia ya kilimanjaro ilidhamini simba na yanga, nani alionewa na nan alinufaika?
2. Kuna timu za JKT Tanzania na Mashujaa zote ni za jeshi mbona hilo halioni?
3. Azam media wanadhamini ligi yote na wanafamilia ya azam wanamiliki timu mbona huo mgongano hauoni?
Kama ni kweli ameandika barua hiyo basi amejishushia heshima kwangu mimi.