Ombi la wachimbaji wadogo kiomoni kwa mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano wa tanzania, dr. Samia.

Ombi la wachimbaji wadogo kiomoni kwa mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano wa tanzania, dr. Samia.

popah21

Member
Joined
Jun 8, 2023
Posts
13
Reaction score
6
Sisi wachimbaji wadogo kutokea mkoani Tanga wilaya ya Tanga kata ya Kiomoni mtaa wa Kiomoni, tunamuomba mheshimiwa raisi awaamrishe makamishna wa mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro waweze kutulipa fidia zetu, tumekua tukidai fidia zetu miaka na miaka kutokea mwaka 2021, tunasomesha watoto katika hali ngumu, tuliahidiwa tutalipwa fidia kutokana na mamlaka kuchua maeneo yetu tuliyokua tukiyamiliki kihalali kabisa, ila imefikia hatua hatuna namna zaidi ya kukuomba mheshimiwa raisi utusaidie, tunaishi katika mazingira magumu kwa zaidi ya miaka mitatu Sasa, wengine ni wajane tunaishi kwa tabu sana, tunakuomba mheshimiwa raisi uunde tume itakayokuja kushughulikia hili suala,
 
Imekua ni changamoto ya muda mrefu hali inayowafanya watu wachukie Serikali yao, tunaomba sana sisi wachimbaji wadogo tuzingatiwe
 
Suala linawahitaji mawaziri wawil, Maliasili na Utalii pamoja na WAZIRI wa Madini Hawa ndio wanaweza kutusaidia
 
tuliahidiwa tutalipwa fidia kutokana na mamlaka kuchua maeneo yetu tuliyokua tukiyamiliki kihalali kabisa, i
Heri yenu ninyi, sisi wa Ngorongoro tumebebwa mzobe mzobe na kuhamishiwa Kijiji cha Msonera.

Tumeondolewa kwenye makazi yetu, ktk ardhi ya mababu zetu kisha tukajengewa mabanda ya vyoo ambavyo wamevibatiza jina la nyumba huko Msonera
 
Huruma ya Serikali ya Jamhuri wa Tanzania kwa sisi wananchi wake Iko wapi?
 
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro yamepewa mandate ya kusimamia mapango ya AMBONI CAVES ambayo mwanzon yalikua chini ya Mali Kale, ila kutokana Serikali ilichakata na kuona umuhimu wa mapango wakayakabidhi mapango kwa Ngorongoro
 
Back
Top Bottom