Nilimsikia jana akijibu hizo critics..nikasikitika sana..kwa kweli upeo wa wanamuziki wa kiBongo (Bongo Flava) bado ni mdogo sana.
Ommy Dimpoz badala ya kushukuru kuwa washabiki wake wamekuwa 'honest' na kulalamika video yake imekuwa na kiwango cha chini kuliko walivyotarajia...yeye akawashukia na kuwalaumu kuwa 'wanachonga' tuu bila kufahamu mambo ya video. Akitapa video imefanywa na Ogopa Deejays.
My Take: Sawa video imefanywa na watu wenye reputation, lakini video hiyo ilifanywa kwa ajili yetu sisi washabiki. Nasi hatuangalii kafanya nani, bali tunaangalia utamu wa video wenyewe....usipokuwepo hata kama video imefanywa na malaika tutaponda tu.
Ommy...go back to studio and come up with something of your status...and the status of the song! Wapo wanamuziki wengi tu wakubwa Marekani wamere-do the video kwa sababu walichemsha mwanzoni. Si jambo la kuonea aibu..ni jambo la kujifunza!