Ongeza rutuba kwenye ardhi yenye alkali

Ongeza rutuba kwenye ardhi yenye alkali

engmtolera

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
5,149
Reaction score
1,441
Ndugu Wakulima wenzangu, habari za majukumu

Moja ya tatizo kubwa linalopunguza uzalishaji wa mazao kwa wakulima wetu ni matumizi ya Ardhi yenye alkali kubwa kupita kiasi. Hapa namaanisha utakapopima udongo wako na kukuta pH yake ni zaidi ya 7 elewa kuwa huo udongo ni wa alkali na pH huenda hadi kufikia zaidi ya 10.

Udongo wenye sifa hii huwa na matatizo ya kutoshikilia virutubisho hususani wakati wa mvua au wakati wa kumwagilia na chumvi huwa ni nyingi na hii husababisha udongo kupoteza rutuba na kupunguza uzalishaji.

Zipo njia mbali mbali za kupunguza pH na chumvi, baadhi ya njia hizo ni gharama kwa wakulima wetu.

Kwa sasa tunafanya utafiti ili kuweza kutumia njia rahisi na zenye gharama nafuu kwa wakulima wetu. Moja ya hizo njia ni matumizi ya mkaa, gypsum, vinyesi vya wanyama n.k

Kwa sasa tumeweza kufanya utafiti kwa kutumia muunganiko wa Gypsum na EM, matokeo yameonekana ni mazuri na yanatia moyo.

Unaweza kupitia link hii hapa ili uweze kupata elimu zaidi.

Effect of effective microorganism and gypsum amendments on nutrient leaching, pH, electrical conductivity, and Okra growth parameters under coastal saline soil

Karibuni wadau, kwa maslahi mapana ya kilimo chetu.
 
Japo kwa ufupi nilitamani kujua matokeo mliyoyapata baada ya kutumia Gypsum Na EM. Baada ya kutumia hizo njia, PH ilishuka kwa kiasi gani?Na iliendelea kubaki hivyo hivyo kwa kipindi chote cha utafiti wenu?
 
Japo kwa ufupi nilitamani kujua matokeo mliyoyapata baada ya kutumia Gypsum Na EM. Baada ya kutumia hizo njia, PH ilishuka kwa kiasi gani?Na iliendelea kubaki hivyo hivyo kwa kipindi chote cha utafiti wenu?
Mkuu Kudasai,ukipitia chapisho letu utaona jinsi pH na Chumvi ilivyo shushwa na huu mchanganyiko wa Gypsum na EM, na kikubwa Zaidi ni kuwa EM ndiyo inasaidia kushusha pH kwa sababu Gpysum yenyewe huwa haina madhara kwa pH,na hii EM inashushaje pH ni kwasababu,EM ukisha itengeneza kikawaida ili uweze kuitumia ktk udongo au mmea ni lazima pH yake iwe chini ya 3.5,ikizidi hapo hutakiwi kuitumia,na hii unavyo itumia ktk udongo wenye alkali yenyewe huwa inaongeza tindikali-acid ambayo husaidia kushusha pH ya udongo.
EM inafanya mengi ktk udogo na mmea,ukipitia hiyo link hapo utaweza kupata elimu japo kwa chache wake.
 
Mkuu Kudasai,ukipitia chapisho letu utaona jinsi pH na Chumvi ilivyo shushwa na huu mchanganyiko wa Gypsum na EM, na kikubwa Zaidi ni kuwa EM ndiyo inasaidia kushusha pH kwa sababu Gpysum yenyewe huwa haina madhara kwa pH,na hii EM inashushaje pH ni kwasababu,EM ukisha itengeneza kikawaida ili uweze kuitumia ktk udongo au mmea ni lazima pH yake iwe chini ya 3.5,ikizidi hapo hutakiwi kuitumia,na hii unavyo itumia ktk udongo wenye alkali yenyewe huwa inaongeza tindikali-acid ambayo husaidia kushusha pH ya udongo.
EM inafanya mengi ktk udogo na mmea,ukipitia hiyo link hapo utaweza kupata elimu japo kwa chache wake.
Usiwe mvivu unapoamua kutoa mada za kuelimisha. Unafikiri wakulima wote wanajua EM ni nini?
 
Mkuu, kwanza nakushukuru sana kwa wasilisho lako hili kwetu la kutujuza juu utafiti mliofanya ili kutusaidia sisi wakulima kuboresha wingi wa mavuno ya mazao yetu
Nashukuru sana. Maana kwa wakutukwamua sisi wakulima ni ninyi watafiti wa uboreshaji rasilimali zinazosaida kupatikana mavuno mengi ikiwemo ardhi /udongo.

Sasa Mkuu kwa kuwa sisi tuliowengi hapa JF lakini wachache tunaopenda mambo ya kilimo kwenye jukwaa hili (nadhani) ; ungeturahisishia usomaji wetu hapa juu ya utafiti wenu kwa kutuwekea muhitasari wa utafiti wenu kwa kuonyesha wazi mambo haya :-
1. utangulizi mfupi wa utafiti wenu na umuhimu wake kwa sisi wakulima.
2. Lengo mahususi lililowaongoza kwenye utafiti huo.
3. Njia zenu za kisayansi mlizotumia ili kufanikisha lengo mahususi hapo juu namba mbili (maana tuna vijana wetu baadhi wanapenda mambo ya utafiti nao tungependa waje watujaribie utafiti huu kwa mazingira ya huku kwetu shambani labda kwa kuongezea vitu vingine kwenye utafiti ila kwa kufuata njia mliyotumia)
4.Matokeo kwa ufupi ya utafiti wenu hata kwa kutaja namba (kama mchangiaji hapo juu alivyopendekeza)
5.Ushauri wa jumla ya namna bora ya kutumia takwimu za matokeo ya utafiti wenu huu ili tupate matokeo tarajiwa ya mavuno yetu.
6. Pia ungetufafanulia baadhi ya maneno uliyotumia kuwasilisha ujumbe wako huu. Mfano. Maana enzi zetu za kujifunza tulikuwa na jamaa wanasomea mazingira kifupi cha EM. kilikuwa na maana tofauti na wale waliosomea mambo ya mitambo ya umeme na simu, ama wale wa elimu ya afya, ama wale wa elimu ya dini nakadhalika. Wote tukija hapa na misingi yetu hiyo ya zamani ya elimu yetu tunaweza tukapotoshana wakati wa kuwasimulia wenzetu ambao hawakupata nafasi ya kusoma ujumbe wako. Hivyo, Mkuu tunaomba utufikirie katika hili pia.

Mkuu ni hayo tu, ni matumaini yangu utatusaidia kujua kwa kina ingawa kwa ufupi utafiti wako. Hivyo 'viunganishi' vya utafiti wako ulivyoviweka kwa ajili ya maelezo ya kina, baadhi ya sisi 'wahenga' vitatupa taabu. Wewe tuwekee muhitasari tu kama nilivyokuomba hapo juu.

Natanguliza Shukrani.
 
Mkuu, kwanza nakushukuru sana kwa wasilisho lako hili kwetu la kutujuza juu utafiti mliofanya ili kutusaidia sisi wakulima kuboresha wingi wa mavuno ya mazao yetu
Nashukuru sana. Maana kwa wakutukwamua sisi wakulima ni ninyi watafiti wa uboreshaji rasilimali zinazosaida kupatikana mavuno mengi ikiwemo ardhi /udongo.

Sasa Mkuu kwa kuwa sisi tuliowengi hapa JF lakini wachache tunaopenda mambo ya kilimo kwenye jukwaa hili (nadhani) ; ungeturahisishia usomaji wetu hapa juu ya utafiti wenu kwa kutuwekea muhitasari wa utafiti wenu kwa kuonyesha wazi mambo haya :-
1. utangulizi mfupi wa utafiti wenu na umuhimu wake kwa sisi wakulima.
2. Lengo mahususi lililowaongoza kwenye utafiti huo.
3. Njia zenu za kisayansi mlizotumia ili kufanikisha lengo mahususi hapo juu namba mbili (maana tuna vijana wetu baadhi wanapenda mambo ya utafiti nao tungependa waje watujaribie utafiti huu kwa mazingira ya huku kwetu shambani labda kwa kuongezea vitu vingine kwenye utafiti ila kwa kufuata njia mliyotumia)
4.Matokeo kwa ufupi ya utafiti wenu hata kwa kutaja namba (kama mchangiaji hapo juu alivyopendekeza)
5.Ushauri wa jumla ya namna bora ya kutumia takwimu za matokeo ya utafiti wenu huu ili tupate matokeo tarajiwa ya mavuno yetu.
6. Pia ungetufafanulia baadhi ya maneno uliyotumia kuwasilisha ujumbe wako huu. Mfano. Maana enzi zetu za kujifunza tulikuwa na jamaa wanasomea mazingira kifupi cha EM. kilikuwa na maana tofauti na wale waliosomea mambo ya mitambo ya umeme na simu, ama wale wa elimu ya afya, ama wale wa elimu ya dini nakadhalika. Wote tukija hapa na misingi yetu hiyo ya zamani ya elimu yetu tunaweza tukapotoshana wakati wa kuwasimulia wenzetu ambao hawakupata nafasi ya kusoma ujumbe wako. Hivyo, Mkuu tunaomba utufikirie katika hili pia.

Mkuu ni hayo tu, ni matumaini yangu utatusaidia kujua kwa kina ingawa kwa ufupi utafiti wako. Hivyo 'viunganishi' vya utafiti wako ulivyoviweka kwa ajili ya maelezo ya kina, baadhi ya sisi 'wahenga' vitatupa taabu. Wewe tuwekee muhitasari tu kama nilivyokuomba hapo juu.

Natanguliza Shukrani.

Kwa ujumla wake ni kwamba utafiti wetu umejikita Zaidi ktk kutafuta njia za kusaidia kupunguza upotevu wa virutubisho vya udongo hususani ktk udongo wenye alkali, virutubisho hivyo ni muhimu sana ktk mmea ili kuweza kuusaidia ktk ukuaji wake na uzalishaji wa mazao kwa wingi Zaidi.Uwepo wa uwingi wa pH na Sodium (chumvi) vinasababisha udongo huu kushindwa kuzuia virutibisho visibaki ktk udongo pindi mvua zinaponyesha hata wakati tunafanya umwagiliaji.
Nini tumefanya
Tumetumia soil amendments kama Gypsum na EM ktk utafiti wetu ili kuweza kuona kama tutaweza punguza pH pamoja na chumvi na kuongeza virutubisho vilivyopotea na kuvishikilia visipotee
Nini maana ya Gypsum na EM
Hii ni ile gypsum tunayoifahamu lakini yenyewe ni FGD gypsum na kazi yake kubwa ni kuimarisha udongo ktk unyonyaji maji,kuimarisha bulk density ya udongo N.K
EM-Kirefu chake ni Effective microorganisms (EM) na mgunduzi wa hii EM ni Prof Higa toka Japan
Ina nini EM
Kwa ufupi tu ni kwamba EM ndani yake ina mchanganyiko wa yeasts, lactic acid bacteria, na photosynthetic bacteria na kazi yake kubwa ktk udongo ni kutengeneza mazingira mazuri kwa ukuaji na afya ya mmea.
Utaona ktk chapisho letu kuwa pH na chumvi vimepungua kwa asilimia 13.02 na 47.27 ukifananisha na ilivyo awali,na pia virutubisho vimeweza punguza ktk upotevu wake na baadhi vimeongezeka kama Manganise, Magnesium na hata Potasium.
Na kiukweli vipo vingi vimeelezwa ktk chapisho ukipata wasaa jaribu kupitia na kama kuna maboresho na ushauri tupo kuwasikiliza wakulima wenzetu.
EM si kitu kipya Tanzania,kimesha fanyiwa kazi Mwanza na kimeleta matokeo chanya,Kenya wenzetu walianza nayo muda na wanaitumia kwa mambo mengi mfano,kuoshea vyombo,kilimo,kusafishia maji taka,kuimarisha afya ya mifugo kwa kuchanganya ktk chakula.
Kwa ufupi ni hayo tu wadau
Asanteni.
 
Mkuu Mtolera, nimefanikiwa kusoma chapisho lako japo sehemu ya kwanza tu, "abstract". Nadhani ni chapisho zuri. Hongera sana.
Sasa hii Gypsum Na EM ninyi mnazalisha? Gharama zake zikoje? Mnashauri zitumike kwa muda gani kwenye shamba ili kuweza kushusha pH kwa level inayohitajika?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kudasai
Kwanza Naomba nichukue fursa hii kukushukuru kwa kupitia chapisho letu angarau kwa kiwango cha Abstact,lakini pia Naomba kuzipokea pongezi zako kwa dhati kwani unaelewa maana ya chapisho na muda unaotumika kuliandaa hapo tukiacha muda wa ufanyaji utafiti husika.
Kwa upande wa Gypsum,aina hii ya virutubisho vya udongo,imekuwa ikitumika na inaendelea kutumika ktk kilimo kwa muda mrefu sana na kwa utafiti wetu tulinunua ktk maduka ya yanajihusisha na huduma za kilimo hapa China.
Lakini pia EM,hii ni trade mark nayo inapatikana madukani sina hakika kwa ktk maduka ya Tanzania,ingawaje maeneo ya Mwanza wapo watafiti walisha wahi fanya utafiti unaoihusu EM,lakini kwa China tuliweza nunua ktk maduka yanayohusika na maswala ya kilimo,lakini ili uweze kuitumia ktk udongo au mmea kuna njia kadhaa za kuifanya iwe active,ingawaje unaweza watengeneza hawa microorganisms- EM wewe mwenyewe kwa kutumia mabaki ya vyakula,lakini tuliona tununue kutokana na muda si Rafiki.
Matumizi ya muunganiko wa Gypsum na EM ni vyema yakawa ya muda mrefu ili kuweza kuleta tija ktk udongo na baadhi ya watafiti,wanashauri kuwa matumizi ya muda mrefu ya hizi soil amendments ktk udongo ni nzuri Zaidi na hazina madhara kama ilivyo ktk mbolea za viwandani.
Kwa sasa tunaendelea na utafiti mwingine unao husisha mikaa ya mimea yaani biochar na EM,lengo hapa ni kutaka kuondokana na hizi mbolea zinazobakiza madhara makubwa ktk udongo.
Asante
 
Back
Top Bottom