Ongezeko la kiwango cha riba nchini Marekani laathiri uchumi wa Afrika

Ongezeko la kiwango cha riba nchini Marekani laathiri uchumi wa Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
微信图片_20220923190027.jpg
Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na janga la UVIKO-19, Marekani ilichapisha dola nyingi ili kuchochea uchumi. Lakini kuanzia mwaka huu, Marekani imegeuza sera ya kifedha na kuongeza viwango vya riba ili kukabiliana na mfumuko wa bei. Kitendo hicho kimekuwa moja ya vyanzo vikuu vya mfumuko wa bei duniani, haswa kimeleta athari kubwa kwa maendeleo ya uchumi wa nchi za Afrika.

Hivi karibuni, kwa kuwa Benki Kuu ya Marekani imepandisha kiwango cha riba kwa mfululizo, kiwango cha ubadilishanaji wa dola za Kimarekani kimeongezeka kwa kiasi kikubwa. Hali hii imesababisha ongezeko la bei ya chakula na nishati duniani, ambavyo vinauzwa kwa dola za Kimarekani, na kuleta shinikizo kubwa la mfumuko wa bei katika nchi za Afrika. Idara ya Takwimu ya Kenya hivi majuzi ilitangaza kuwa mfumuko wa bei nchini Kenya ulifikia asilimia 8.5 mwezi Agosti, ambacho ni kiwango cha juu zaidi katika miaka mitano iliyopita.

Hali ya nchi nyingine za Afrika ni mbaya zaidi. Kiwango cha mfumuko wa bei nchini Nigeria, ambayo ni nchi ya kwanza kwa ukubwa a uchumi barani Afrika, kilifikia asilimia 19.64 mwezi Julai. Ripoti iliyotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika inatabiri kuwa, wastani wa kiwango cha mfumuko wa bei cha nchi zote za Afrika kitafikia asilimia 13.5 mwaka huu.

Ili kukabiliana na shinikizo la juu la mfumuko wa bei, Benki Kuu za nchi nyingi za Afrika zimelazimika kuongeza kiwango cha riba. Matokeo ya moja kwa moja ya hatua hii ni kwamba, kasi ya ukuaji wa uchumi itapungua. Ripoti ya Benki ya Maendeleo ya Afrika inatabiri kwamba kasi ya ukuaji wa uchumi wa Afrika itapungua hadi asilimia 4.1 mwaka huu, na itakuwa chini sana ikilinganishwa na asilimia 6.9 ya mwaka jana.

Aidha, kiwango cha juu cha riba nchini Marekani pia kimeongeza kiwango cha ubadilishaji wa dola za Marekani, na kusababisha kushuka kwa thamani ya sarafu za nchi za Afrika, na hata baadi yao zinakabiliwa na hatari ya kushindwa kulipa madeni ya nje. Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kuwa hivi sasa nchi 22 za Afrika zinakumbwa na msukosuko wa kulipa madeni.

Vitendo hivi vya kutowajibika vya Marekani vimepingwa vikali na nchi za Afrika. Mwanauchumi wa Kenya Ken Gichinga anaona kuwa nchi nyingi za Afrika zinaagiza chakula na mafuta ghafi kutoka nje, na kupanda kwa kiwango cha riba cha Marekani kumeongeza kiwango cha dola, ambayo imeongeza moja kwa moja gharama ya uagizaji wa bidhaa hizo.

Wakati huo huo, wawekezaji wengi wa kimataifa wameondoka barani Afrika kutokana na mvuto wa kiwango cha juu cha riba nchini Marekani, hali ambayo imeathiri maendeleo ya uchumi wa Afrika. Mtaalamu wa masuala ya uhusiano wa kimataifa wa Nigeria Charles Onunajju amesema shughuli za uchumi na biashara ya nje za Nigeria na nchi nyingine za Afrika zina uhusiano wa karibu na akiba ya dola za kimarekani, jambo ambalo linamaanisha kwamba Marekani inaweza kuhamisha shinikizo la mfumuko wa bei kwa nchi za Afrika kupitia sera ya kifedha.

Marekani inasema ni kiongozi wa uchumi wa dunia. Hata hivyo, inarekebisha sera yake ya kifedha kama inavyopenda bila kujali kwamba italeta changamoto kwa nchi nyingine haswa nchi za Afrika, kitendo ambacho si cha kuwajibika.
 

Attachments

  • VCG111401313060.jpg
    VCG111401313060.jpg
    131.6 KB · Views: 7
Umedanganywa. Mfumuko wa bei umesababishwa na vita ya Urusi na Ukraine.

Urusi ndiye baba wa uchumi duniani na Putin ndiye rais wa dunia hii.

Marekani wanakudanganya tu.
 
Siku Afrika wakiamua kuwa na sarafu yao, wakiamua kujizalishia chakula chao wakaachana na ujinga wa mazao ya biashara wakaachana na lugha za kikoloni ndio wataondoka kwenye huu utumwa. Ila kwa aina ya vibaraka tulionao itachukua miaka 200 kufikia hapo.
 
Haiingii akilini kwamba kwa ardhi kubwa tuliyonayo bado Afrika imeshindwa kujitosheleza kwa chakula, ni aibu kubwa sana.

Afrika ndio ilipaswa kuilisha dunia kwa chakula lakini eti ndio inaagiza tena chakula kutoka nje ya bara na wakati mwingine eti kupewa misaada ya vyakula kutoka kwenye mataifa yenye uhaba mkubwa wa rasilimali ardhi.

Afrika bure kabisa na ndipo wamezidi kusingizia kwamba karibu shida zao zote husababishwa na wazungu huku ukweli ni wao kukosa uongozi madhubuti.
 
Back
Top Bottom