Ongezeko la kutisha la ugumba

Ongezeko la kutisha la ugumba

jerryempire

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
5,530
Reaction score
9,550
Habari,

Naomba niende moja kwa moja kwa moja kwenye mada.

Zamani ilikuwa wakikutana vijana ambao wako balehe na kushiriki tendo basi asilimia kubwa ni ndani ya miezi kadhaa tu walishapeana mimba.

Lakini hali kwa sasa imekuwa tofauti mno kwani ukienda kwenye mahospitali dada zetu wanaotafuta watoto wamekuwa ni wengi mno na ukienda kwa hawa tiba mbadala like dr mwaka ndo unaweza kuchoka kwa idadi hyo ya tatizo la uzazi.

Zamani ilikuwa tatizo hili la ugumba ni kwa wanawake zaidi lakini kwa sasa hata wanaume wengi wamekuwa na tatizo hili la uzazi kiasi cha kwamba huduma za IVF zimesogezwa sana mikoa ya Dar na Arusha na wateja kila siku wanamiminika.

Swali langu kwa serikali ni kwamba athari hii ya ugumba kwa watanzania wanaiona/wanaiujua?

Na kwanini hawachukui hatua kutoa elimu na hata kuongeza nguvu kwenye hili suala? maana tusipokuwa makini tunaweza kuelekea kubaya

Mwisho endapo kama serikali inalitambua hili tatizo kwanini madawa ya kutoa na kuzuia mimba yanatolewa kiholela kwenye maduka ya madawa?

Watanzania wenzangu naomba mstuke endapo kama hutopata mtoto kipindi hiki jitahidi uwe na uzao wako kwani miaka 5 au 10 ijayo kumpata mwanaume/mwanamke mwenye 100% sawa ya afya ya uzazi itakuwa changamoto mno kama serikali haitoliingilia kati hili swala.

Mwisho
Hii ni fursa kwa wanafunzi kusomea masuala ya afya upande wa uzazi ili baadae wakifaulu wakibahatika kufungua hospitali zao hakika watapiga sana hela kwani kwa sasa wagonjwa ni wengi mno na ndani ya miaka 10 ijayo wateja watakuwa wengi zaidi.

Kwani kwa sasa wagonjwa wengi wanalifanya hili kama siri lakini wengi ni wagonjwa na wanalijua hilo so ndani ya mda huo hapatakuwa na siri tena.
 
Kuna kitu huwa sielewi kwa kufanajisha vitu vya nyuma na sasa.

Binafsi huwezi kufananisha miaka ya nyuma na sasa maana kwanza idadi ya watu imetriple kama sio kudouble sasa lazima matatizo pia yataongezeka pia now days mitandao ipo so kila tukio ni rahisi kusikika kuliko huko nyuma.

Kwangu mimi wakati boraa kabisa ni wakati huu tulionao ambao kuna huduma nyingi za afya, elimu uhakika, na mambo mengi yapo kuliko huko nyuma.
 
Unakuta kabinti cha shule ya msingi ni kahuni kameanza mambo bado kadogo, hakataki kubeba mimba kanatumia dawa kuzuwia mimba. Mpaka kaje kamalize chuo kikuu tayari kameshaua mfumo wake wake wa uzazi utakuwa umeathirika kwa madawa hayo
 
Top 5 most populous countries in Africa:

1. 🇳🇬 Nigeria: 223.8 million
2. 🇪🇹Ethiopia: 126.5 million
3. 🇪🇬 Egypt: 112.7 million
4. 🇨🇩 DR Congo: 102.3 million
5. 🇹🇿 Tanzania: 67.4 million
 
Top 5 most populous countries in Africa:

1. 🇳🇬 Nigeria: 223.8 million
2. 🇪🇹Ethiopia: 126.5 million
3. 🇪🇬 Egypt: 112.7 million
4. 🇨🇩 DR Congo: 102.3 million
5. 🇹🇿 Tanzania: 67.4 million
So tunahitaji depopulation?
 
Ni kweli ugumba ulikuwepo tangu zamani lakini sasa hivi kuna ongezeko kwa wote wanawake na wanaume. Matatizo ya low sperm count yamekuwa mengi kuliko ilivyokuwa miaka ya huko nyuma. Kwa wanawake matatizo ya mauvimbe, PID, kuziba mirija nayo yamekuwa mengi sana. Hata cancer za via vya uzazi pia zimeongezeka kwa wanaume na wanawake pia. Sababu ziko nyingi sana. Kuna wanaozaliwa na ugumba ambao sasa hv ni wengi tu, na wengine wana develop ugumba ukubwani. Wengine wanajitakia wenyewe kutokana na matumizi mabaya ya madawa etc etc, na wengine ugumba unawapata kutokana na exposure ya vitu kama mionzi, madawa ya mimea etc etc. Ila kwa sasa technology imeimprove sana, kila mtu ana uwezo wa kuzaa, hata waliopita menopause 😜
 
Back
Top Bottom