Ongezeko la watu mjini chanzo cha umasikini wetu.

Ongezeko la watu mjini chanzo cha umasikini wetu.

ndayilagije

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2016
Posts
7,491
Reaction score
8,304
Swalama?
Nimepita njia ya morogpro juzi,dah!mji umefika chalinze,mwezi uliopita nilikuwa Nangwanda huko! mmmh sikuona mwanzo na mwisho wa mkuranga na daresalama! Kwa habari ya Bagamoyo tusiongee kabisa!
Najiuliza hizi nyumba zote zimesimama mahali palipokuwa na minazi mikorosho na miembe. Sijatulia vizuri nikapita hukooo visiwani,lahaula la kwata!tangu mjini mpaka Nungwi ni nyumba tupu.
Watanzania tunazaana aisee!hata aje malaika hawezi kutupa hizo sijui huduma bora za jamii.
Msongamano mtaani unazalisha migogoro mingi ya kisiasa na kiutamaduni., kiuchumi na kimani.
Nadhani tupunguze kasi kidogo.
Ni hayo tu ndugu wapendwa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa namsikia kiongozi wa vijana wa upinzani south Africa alisema Africa bado tunahitaj rasilimali watu tuzaane kwa wingi.tukija Tanzania nadhani ardhi ipo ya kutosha tatizo lipo kwenye mpangilio mbovu na ugawaji usiozingatia vipaumbele hasa makazi.bado tunatakiwa tuzaane ili wapatikane watu wa kupiga kazi
 
Nilikuwq namsikia kiongozi wa vijana qa upinzani south Africa alisema Africa bado tunahitaj rasilimali watu tuzaane kwa wingi.tukija Tanzania nadhani ardhi ipo ya kutosha tatizo lipo kwenye mpangilio mbovu na ugawaji usiozingatia vipaumbele hasa makazi.bado tunatakiwa tuzaane ili wapatikane watu wa kupiga kazi
Huenda uko sahihi!Sina hakika kama vijijini kuko hivi,lakini nikiangalia mfano vyombo vyetu vya usafiri !!inanipa shida kidogo, Watoto,wazee,vijana!ni nani atatuajiri?

Sent from my TECNO 7C using JamiiForums mobile app
 
Mkuu tatizo sio kuzaa, kamwe huwezi kuzuia uzazi ndugu yangu, hii ni nature ya kila kiumbe uzazi sio kwa binadamu pekee bali kila kiumbe hi.

Ilinitafakarisha sana juzi kuku ametoto vifanga niltaka kumuhamishia kwenye banda kwa usalama zaidi ajabu yule kuku japo alikua nje niliweza kumkamata kitu ambacha haiwezekani katika hali ya kawaida, alikua tayari kwa lolote lakini sio kuwaacha watoto wake. Mwezi jana mbuzi alizalia machungani mbali nyumbani nilibeba mtoto wake mbuzi aliwaacha wenziwe na kunifuata popote nilipoenda kitu ambacho sio cha kawaida kwa mbuzi kisa ni mtoto.

Hao ni hayawani wasio na akili, je sisi binadamu tulio na akili na utashi na upendo?
Kila binadamu chchote atakachofanya conclusion ni kuwa na mtoto n hio ni asili.

Ingechopaswa kujua watu wenye mamlaka ni kitu kama hicho. Kwa hio waandae mazingira mipangilio ya kuhudumia watu kiasi chochote wataotokea.

Pia ndugu kumbuka nawe umezaliwa, na tokeo lako ni moja kati ya bilioni, kwa hio hakuna aliepo hapa duniani kwa bahati mbaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ongezeko la watu ndiyo fursa ya kuongeza mzunguko wa hela. Dar-Morogoro kutoka Chalinze kungekuwa na break points ambazo zina migahawa, petrol stations, vyoo na mabafu. Wasafiri wa mabasi hata waendeshao magari yao waweze kusimama na kupumzika.

Hivyo vyote vingezalisha ajira lakini vinahitaji umeme na maji ya uhakika.
 
Hizi ndiyo akili za kiafrika....kuzaa ni lazima I'll tuishi lakini tunapoongezeka kama mbilimbi tuwe tunajipanga na matokeo basi.
Huwezi kuwa na chumba kimoja,halafu ukasema utazaa tu mpaka watoto waishe.
Bado naamini migogoro mingi ni sababu ya kusongamana sana.
Soon tutakuwa kama Nigerian,tuongoze kwa utapeli,ulozi,makanisa sijui na nini.
Tupange uzazi, vinginevyo tutakuwa na matatizo makubwa ya rasilimali .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
enendeni mkaazane muuujaze ulimwengu?!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Na kuitiisha nchi na viumbe vyote!!siyo kuvimaliza mkuu tunakoendea tutakosa mpaka maji ya kunywa like mkaa wa kupikia hatuna tayari,makazi mazuri hatuna. Tunalia na tulipoangukia ila tujiulize tulipojikwaa.
Swali liko palepale nani atatuajiri?????

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom