Online purchasing Crdb na Alibaba

Exchange rate ya debit cards zetu huwa juu more than 100sh per dollar.

VISA ya Equity huwa wananibadilishia $1 =2444

MPESA Mastercard wanakula 2540

Kama una option ya kuwa charged kwa TZS, yani huko unakonunua wafanye currency conversion wenyewe, itakuwa much cheaper
 
Exchange rate ya crdb sio exchange ya alibaba au bank kuu, kuwa mpole tu , shukuru hukupata overdraft.
Ukitaka kulipa kiwango unachoona online ni kuwa na account ya USD.
 
Mimi nawashangaa sana mnang'ang'ania hizo wakati kuna nmb na nimeshafanya online transactions mara nyingi tu na wanakata hapohapo unapofanya malipo mtaandaoni mesej inaingia muda huo huo unapofanya malipo, na hakuna makato ya bidhaa unayolipoa wakata kiasi kile kile cha bidhaa unayotaka kununua
 
You are not serious!! sasa huu ndio ushauri wangu...

Kwanza fungua account ya dola kwenye benkiunayoipenda, NMB, Stanbic, backlays na KCB naona wako vizuri eneo hili (visa card zao zina 2FA ambayo ni added level of security)!!

ela zako za TSH badilisha ziwe USD (nenda crdb watakubadilishia, ila kama una ela nyingi unaweza ongea nao wakakupa rate nzuri!!)

Baada ya kupata USD nenda kaweke kwenye account ya dola!!

Unapofanya manunuzi tumia account yenye USD na sio account yenye TZS!!

CRDB rate zao ni 2315 per 1USD!!

Kutumia mpesa itakukula pesa kijinga tumia bank hizo nlizokushauri hapo juu!!
 
Wakati wa kutrade hapo ktk exchange rate uliangalia buying au selling rate??
 
Asante sana mkuu nitafuata ushauri wako boss
 
Vip NMB wako vizuri katika soko la ununuzi mtandaoni
 
hivi paypal inafanya kazi bongo?
 
Sijajua benki walikupa sababu gani. Ila based on my experience with M-Pesa Mastercad unapolipia online purchase yako wanakukata 4% ya thamani ya gharama za hela unayolipia. Kama CRDB nao wanautaratibu huo wa kukata hela kila ulipiapo bidhaa mtandaoni, kwa hiyo kiasi ulichokitaja basi watakuwa wanakata asimilia 3% ya malipo yako.

6,673,219×3%= 200,196.57
Kiasi ambacho kinalingana na hicho ulichokitaja.
 
Ni sawa mkuu na Kama ni hivyo mbona hawaweki wazi Hizo taarifa ?
Mbona mpesa master card fee zao zipo wazi kabisa

crdb wanakuwa na hiden cost maana ukiangalia kwenye tariff guide yao hamna Hizo fee
 
Ni sawa mkuu na Kama ni hivyo mbona hawaweki wazi Hizo taarifa ?
Mbona mpesa master card fee zao zipo wazi kabisa

crdb wanakuwa na hiden cost maana ukiangalia kwenye tariff guide yao hamna Hizo fee
Sijajua sababu za kutoweka wazi hilo.
 
Aisee juzi Kati CRDB walinizingua hadi nikasajiri line ya voda. Halafu wawe open kwenye transaction fee
 
Vp bancABC.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…