Tcra huko usiwaze sana kabla ya KAZI. Kodi huanza kulipwa pale unapoanza kuona mafanikio.
Kama kuna madhui yanayoigusa Serikali ndiyo itakuwa balaaa. Ila kwa sasa tafuta vifaa anza KAZI, maana wengi huishia njiani na ndio HIVYO na kodi ishalambwa na Serikali Mkuu.
Ingia mzigoni.
Kuhusu vifaa (ungesema uko mkoa gani)
Itakuwa nafuu kukishauri.
Mfano: kama uko Dar Unaweza fanya windows shopping kariakoo ila uwe makini na bidhaa maana kuna vitu kama mic hapo usisite kufungua mfuko, vinginevyo utaambulia low quality brand ya mchina.
Vifaa pia unaweza agiza mtandao kupitia e-commerce website za
www.ebay.com,
www.alibaba.com,
www.aliexpress.com nk.
Unahitajika uwe na vifaa vya kuanzia:
1. Camera nzuri budget ni kama 900k
2. Laptop pc yenye specifications alau 4gb ram, 1terabite, 2.5 processors Intel core i5 5gen na ikiwa na dedicated graphics card ya 1gb ni faida zaidi.
3. Tripods stand
4. Lights
5. Mic utachagua mfuko wako ila kama una studio condenser microphone ni nzuri kampuni ziko nyingi sana na kama ni out door boom mic itakufaa pia.
6. Background unaweza tafuta greenscreen
7. Adobe premiere na Photoshop inakuhitaji uwe na maarifa nayo
8. Chumba au geto unalipa uwezo wa kuwa studio.
*****
Badget yako itakufanya uanze na kipi kwani sio lazima kuanza na vifaa vyote hivyo.
Piga kazi na ujue usingizi kwako utakuwa ni mama mkwe.
Nikutakie kila la heri Mkuu.
Mengine watakuongezea na utayafahamu Kwenye field huko huko