mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
Hii kampeni feki kabla ya Uchaguzi iliyopewa jina la ''Mama Hana Deni'' imekaa kimkakati kuisaidia CCM ambayo ndio inaongoza Serikali kuweza kuonesha miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa kwa kodi za wananchi. Sasa hii naona Baba Levo kaamua kuichukua akishirikiana na Online TVs nchini, kuzunguka nchi nzima kukagua hiyo miradi. Mbaya zaidi wanatembelea miradi mizuri mizuri na kuacha mingi ambayo imeshindwa kufanikiwa au kutelekezwa
Kuna tuhuma na hisia miongoni mwa watu kwamba baadhi ya vituo vya televisheni vya mtandaoni (Online TVs) vinaegemea upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM) au vimeingiliwa ili kutangaza habari zinazounga mkono serikali na chama tawala.
Hii inaweza kutafsiriwa kama...
Upendeleo - Baadhi ya watu wanaona kuwa vyombo hivyo havikosoi sana serikali au CCM na badala yake vinatoa taarifa zinazounga mkono sana chama hicho.
Kulipwa au kununuliwa - Kuna wanaodhani kwamba baadhi ya Online TVs wanalipwa ili kuendesha ajenda fulani za CCM.
Uoga wa kufungiwa - Wengine wanaona kuwa huenda vyombo hivyo vinaogopa kufungiwa na mamlaka kama hawataonyesha upendeleo kwa serikali.
Hiki anachofanya Baba Levo binafsi naona ni kampeni kwa Rais Samia na CCM kwasababu hizi
Wito wangu kwa Online TVs, najua njaa kali sana mtaani ila hii haiwazuii kusimamia weledi wenu ipasavyo. Igeni mfano wa Jambo TVs katika uhabarishaji wenu. Kuna maisha mengine baada ya uchawa, msije tumiwa na kutupwa.
Kuna tuhuma na hisia miongoni mwa watu kwamba baadhi ya vituo vya televisheni vya mtandaoni (Online TVs) vinaegemea upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM) au vimeingiliwa ili kutangaza habari zinazounga mkono serikali na chama tawala.
Hii inaweza kutafsiriwa kama...
Upendeleo - Baadhi ya watu wanaona kuwa vyombo hivyo havikosoi sana serikali au CCM na badala yake vinatoa taarifa zinazounga mkono sana chama hicho.
Kulipwa au kununuliwa - Kuna wanaodhani kwamba baadhi ya Online TVs wanalipwa ili kuendesha ajenda fulani za CCM.
Uoga wa kufungiwa - Wengine wanaona kuwa huenda vyombo hivyo vinaogopa kufungiwa na mamlaka kama hawataonyesha upendeleo kwa serikali.
Hiki anachofanya Baba Levo binafsi naona ni kampeni kwa Rais Samia na CCM kwasababu hizi
- Baba Levo ameonekana mara kadhaa kuonyesha wazi kumuunga mkono Rais Samia na CCM.
- Slogan ya "Mama Hana Deni" imetumika sana kama sehemu ya kuonyesha mafanikio ya serikali ya awamu ya sita na kuandaa mazingira ya uchaguzi mkuu 2025.
- Mara nyingi, kauli kama hizo kutoka kwa watu maarufu hutafsiriwa kama kampeni za chinichini za kuandaa wananchi kumpigia kura kiongozi au chama husika.
Wito wangu kwa Online TVs, najua njaa kali sana mtaani ila hii haiwazuii kusimamia weledi wenu ipasavyo. Igeni mfano wa Jambo TVs katika uhabarishaji wenu. Kuna maisha mengine baada ya uchawa, msije tumiwa na kutupwa.