Onyango aikacha Simba. Akimbilia Singida

Dr Restart

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
4,949
Reaction score
24,046
Beki Kisiki wa Kimataifa wa Kenya, Joash Onyango amesaini kandarasi kuitumikia timu ya Singida Fountain Gate.

Katika picha iliyopakiwa katika Mitandao ya kijamii, mlinzi huyo aliyekuwa anaitumikia Simba Sports Club ameonekana na Mkurugenzi wa Singida katika sehemu maalum ya kusaini Kandarasi huku akiwa na jezi rasmi za timu hiyo.

Haijajulikana ni kandarasi ya muda gani. Pia, haijaelezwa bayana kama ameenda kiujumla ama kwa mkopo.

Onyango sasa kuungana na mchezaji mwenzie Pascal Wawa, waliotengeneza ukuta imara sana walipokuwa Simba SC.
 
Bado sako, banda na chama. Nashauri simba iwapeleke kwa mkopo au wawauzie moja kwa moja trans camp au Ruvu shooting au kitayosce ...kwa kuwa hawana faida yoyote kwa simba
 
Kwa hali hii simba wasahau tena ubingwa msimu huu. Maana watatumia muda mwingi kukijenga upya kikosi chao. Msimu ujao, kama kawaida. Wanakibomoa tena.
Tulibeba mara 4
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…