ONYO: Timu itakaayomsajili Bernard Morrison (Toto tundu) itakuwa imekubali kukumbatia Mzinga wa Nyuki

ONYO: Timu itakaayomsajili Bernard Morrison (Toto tundu) itakuwa imekubali kukumbatia Mzinga wa Nyuki

Msizipangie timu, huyu mchezaji aliachwa na Simba kwa utovu wa nidhamu lakini yanga walifikiri wamewakomoa Simba kwa kumsajili lakini hukusikia viongozi au mashabiki wa Simba wakimnenea mabaya kwa kifupi kama mmeshindwana naye achaneni naye kwa amani
 
NALIA NGWENA niliona aibu Mimi kitendo cha Bernard Morrison kumpora pesa waziri wa sanaa na michezo Mhe. Chana.

Kwa haraka haraka ni kama kitendo cha kuchekesha lakini kwa NALIA NGWENA the great thinker mkombozi wa Fikra mpya kwa kweli siyo Jambo la busara (kiungwana).

Lakini tukio lingine kwenye mchezo wa Mbeya city vs Yanga Toto tundu Bernard Morrison alipokua akishangilia baada ya kutupiwa makopo na takataka the Super Ben alirudisha kwa mashabiki.

Sijui hili limekaaje kikanuni nafikiri Bodi ya ligi na TFF Kama atakua amefanya kosa basi atawajibishwa bila Shaka.

Tukio lingine lililo nichosha zaidi nakuona kabisa Bernad Morrison ni mtovu wa nidhamu ni pale Ikulu, Eng. Hersi kumtambulisha mbele ya Mhe. Rais lakini hakusimama kwa kweli aibu niliona Mimi na ninaimani kabisa Hersi alijisikia vibaya lakini alijikaza tu.

Lakini alipotambulishwa Mzinze alisimama Ila ilipofikia zamu yake aligoma kabisa kusimama.

Timu yoyote ya Tanzania itakayomsajili Bernard Morrison itambue Kabisa itakua imekumbatia mzinga wa Nyuki.

Nawasilisha hoja

View attachment 2648937
singida big stars watajiju
 
Alifanyaje ikulu?
Wakati Rais wao Eng Hersi akitambulisha wachezaji kwa Mh Rais alitajwa mara mbili mchezaji chipukizi klabuni Clement Mzinze lakini Morrison ndio akasimama badala ya Clement japo watu walifurahia kama kituko ila ilipofika zamu yake ya kutambulishwa akagoma kusimama tena mara mbili zote, hii haikuwa tabia njema hasa ukiangalia walikuwa wanatambulishwa kwa Rais wa nchi.
 
Msizipangie timu, huyu mchezaji aliachwa na Simba kwa utovu wa nidhamu lakini yanga walifikiri wamewakomoa Simba kwa kumsajili lakini hukusikia viongozi au mashabiki wa Simba wakimnenea mabaya kwa kifupi kama mmeshindwana naye achaneni naye kwa amani
Nakubaliana na wewe, ukimshindwa mke mwache aende usimsindikize Kwa makandokando.
 
Rudisha kwao akale egusi na fufu.
Tz nchi peke hata mkimbizi toka Malawi atatukuzwa
 
Wakati Rais wao Eng Hersi akitambulisha wachezaji kwa Mh Rais alitajwa mara mbili mchezaji chipukizi klabuni Clement Mzinze lakini Morrison ndio akasimama badala ya Clement japo watu walifurahia kama kituko ila ilipofika zamu yake ya kutambulishwa akagoma kusimama tena mara mbili zote, hii haikuwa tabia njema hasa ukiangalia walikuwa wanatambulishwa kwa Rais wa nchi.
Ila Hersi naye kwa nini alimuita "toto tundu"? Tukienda kipro, alikuwa na haki ya kuuchuna. Utani wa kwanza kusimama alipoitwa Mzize nao haukuwa na madhara, ulikuwa ni mkusanyiko wa kufurahi na kusherehekea, kama kuna mtu alikwazika huyo ndiyo ana shida.
 
Yanga hamna utamaduni wa kukosoa viongozi wenu hasa kipindi kama hiki ambacho timu inaonekana kufanya vizuri ila Morrison hakutakiwa kuachwa.

Morrison hata kama kacheza mechi chache ila mchango wake kwenye timu ni mkubwa sana. Ukisema kacheza mechi 15 tu, je umehesabu hata zile ambazo alikuwa tayari kucheza ila hakupangwa? Umehesabu goli alilofunga dhidi ya Marumo ambalo kwa kiasi kikubwa ndiyo lililoipeleka Yanga fainali? Tofauti ya zawadi za fedha na medali kati ya kuishia nusu fainali na kucheza fainali zinatosha kumlipa mshahara wa mwaka mzima, kuvumilia utoro wake na chenchi ikabaki. Labda uniambie sababu kubwa ni alivyogoma kufanyiwa sub ile mechi ya Chamazi au uniambie utani aliofanya Ikulu.

Kuna ule uzi jamaa mmoja aliuliza mahesabu ya kihasibu kuhusu usajili wa Aziz Ki. Goli alilofunga dhidi ya Club Africain lilitosha kufumbia macho madhaifu yake mengine yote aliyoonyesha msimu mzima maana bila lile goli Yanga ndiyo ilikuwa bye bye mashindano ya kimataifa. Ni kwa mtazamo huo huo naangalia thamani ya Morrison.
 
Back
Top Bottom