ONYO: Ukiweka agano la damu hakikisha unalitimiza, or else...

ONYO: Ukiweka agano la damu hakikisha unalitimiza, or else...

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
18,037
Reaction score
33,681
Kuna watu wanapo pitia kwenye kipindi fulani kigumu au wanapo kuwa wanahitaji jambo fulani litokee katika maisha yao huwa wanaweka nadhiri ama kujiapiza kwamba endapo watafanikiwa kupita salama katika kipindi hicho kigumu au endapo jambo wanalo litaka litatokea basi watachinja kuku, mbuzi, kondoo, ama n'gombe .

Unapo toa kauli hii jua tayari umesha weka ahadi katika ulimwengu wa roho ambayo lazima uitimze. Tambua kwamba tayari kauli yako ipo recorded kwenye ardhi. Usipotimiza nadhiri yako basi jua ya kwamba kila unapo kanyaga hatua yako juu ya ardhi au kila unapo tumia kitu chochote ambacho ni zao la ardhi ardhi inapiga kelele kukumbusha ahadi yako. Ardhi inahitaji kunywa damu ambayo uli ahidi. Maisha ya mwanadamu kuanzia siku anakuja duniani hadi siku anarudi kwa muumba wake yote yapo recorded kwenye ardhi. Wachawi wanaweza kujua kila kitu kuhusu maisha yako na nyota yako kwa kutumia ardhi. Hata YESU wakati ana andika chini kwenye ardhi mbele ya wale jamaa walio enda kumshitaki Maria Magdalena, wataalamu wanasema alikuwa anatazama rekodi za watesi wale kwenye ardhi. Alicho kuwa anakifanya ni kama wewe unavyo weza kusearch taarifa za mtu fulani kwenye internet.

Yohana 8:4-11​

Kisha wakamwuliza Yesu, “Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi. Katika sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?” Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole. Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, “Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.” Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini. Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitangulia wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale. Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, “Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?” Huyo mwanamke akamjibu, “Bwana, hakuna hata mmoja!” Naye Yesu akamwambia, “Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena.”

Wataalamu wa kiroho wanasema wakati Yesu ana andika juu ya ardhi aliweza kuona kila kitu au kila jambo au kila dhambi iliyo fanywa na jamaa wale. Jamaa hao kilicho wafanya kukimbia ni kuona kuhusu habari zao kwenye maandishi yale ambayo Yesu alikuwa akiyaandika. Mfano labda miongoni mwao yupo mmoja alikuwa anatembea na mke wa mwenzake so alipo ona habari zake hapo hakuwa na jinsi zaidi ya kukimbia.

KATIKA HALI YA KAWAIDA HAIWEZEKANI WATU WAKIMBIE MBIO JUST KWA KUAMBIWA KWAMBA KAMA KATI YENU HAKUNA MWENYE DHAMBI BASI AANZE KUMPIGA JIWE MWANAMKE HUYU. WATU HAO BADO WANGE ENDELEA KUMUADHIBU MWANAMKE NA HAKUNA AMBAE ANGEJUA KWAMBA WANA DHAMBI YOYOTE. KILICHO WAFANYA WAKIMBIE NI KUONA TAARIFA ZAO JUU YA ARDHI KUPITIA MAANDISHI YA YESU. KWA MAANA NYINGINE NI KWAMBA YESU ALI ANDIKA JUU YA ARDHI HIYO PASSWORD NA KUPITIA PASSWORD HIYO ARDHI YENYEWE IKAYAFUNUA KWA MAANDISHI MADHAMBI YA WATESI WALE.


So ukiweka nadhiri ya kumwaga damu ya mnyama ni lazima uitimize kabla haujafa vinginevyo utakuwa umeacha deni kubwa sana la kiroho kwa watoto na wajukuu zao kwa sababu wao pia ni damu katika damu yako na ni mifupa katika mifupa yako.


Kama katika maisha yako umewahi kuweka nadhiri ya kumwaga damu ya mnyama endapo jambo lako fulani litafanikiwa basi hakikisha unatimiza nadhiri hiyo ukiwa hai. Ukimwaga damu, damu hiyo itapeleka taarifa ardhini kwamba tayari umetimiza nadhiri yako.

Ardhi ni kiumbe hai. Inasikia, inatamka n.k.

Watu wa imani fulani ya kale, wana amini kwamba sayari hii ya dunia tunayo ishi mimi na wewe hapo zamani za kale za enzi hizo ilipata kuwa kiumbe hai mfano wa viumbe hai unao wafahamu wewe. Siku moja kiumbe hicho kikafa, kilipo kufa kikaoza, kilipo oza kikatoa funza wa aina mbalimbali. Sasa hao funza ndio viumbe mbali mbali waliopo juu ya ardhi kama vile binadamu, wanyama, mimea, wadudu, ndege, samaki, nakadhalika.

Mfano wake ni BINADAMU anapo kufa si anaenda kuzikwa kaburini ? akienda kuzikwa kaburini si anatoa funza? wale funza si wanaishi ? chanzo cha uhai wao si ni maiti ? basi vivyo hivyo ndivyo ulivyo binadamu.

Ndio maana una ambiwa kwenye maandiko kwamba MWANADAMU U MAVUMBI WEWE, KWA MAANA KATIKA MAVUMBI YA ARDHI NDIPO ULIPO TWALIWA..
 
Vipi kuhusu kubikiri nalo ni agano!? Au tusubiri tamko la mkalimani
Yes ni agano. Ile damu iliyo mwagika baada ya tendo inatamka juu ya ardhi kwamba wewe ulie mbikiri mwanamke huyo ndio mume halali wa mwanamke huyo ambae unatambulika katika ulimwengu wa rohoni.

Ukioa mwanamke ambae sio bikra jua kwamba umeoa mwanamke ambae sio mke wako
 
Yes ni agano. Ile damu iliyo mwagika baada ya tendo inatamka juu ya ardhi kwamba wewe ulie mbikiri mwanamke huyo ndio mume halali wa mwanamke huyo ambae unatambulika katika ulimwengu wa rohoni.

Ukioa mwanamke ambae sio bikra jua kwamba umeoa mwanamke ambae sio mke wako
Hili ni kweli kabisa.
 
Unatumia maandiko kupotosha. Hii ni ibada ya kishetani.
Mwanakondoo alishachinjwa kwaajili yetu/ Yesu alimwaga damu pale msalabani kwaajili yetu.

Ili kufuta laana na uuovu wa aina yoyote tunapaswa kutubu na kusafishwa kwa Damu ya Yesu.
 
Unatumia maandiko kupotosha. Hii ni ibada ya kishetani.
Mwanakondoo alishachinjwa kwaajili yetu/ Yesu alimwaga damu pale msalabani kwaajili yetu.

Ili kufuta laana na uuovu wa aina yoyote tunapaswa kutubu na kusafishwa kwa Damu ya Yesu.
But still bado damu za wanyama zinafanya kazi kama kawaida . Hazijapteza nguvu za kiagano " covenant power". Ni kanuni ambayo haiwezi kuvunjika.
 
Hivi mungu bado anapenda kuku, mbuzi, kondoo na vitu kama hivyo? Mungu na waganga wa kienyeji wana tofauti gani?

Mambo ya dini ni mambo ya kitapeli.
 
Hivi mungu bado anapenda kuku, mbuzi, kondoo na vitu kama hivyo? Mungu na waganga wa kienyeji wana tofauti gani?

Mambo ya dini ni mambo ya kitapeli.
hupendi kufikiria. kama huna uwezo wa kufahamu uliza
 
Nin matokeo yake sasa?

Je ni ufahari kuwabikiri wanawake wengi??

Na je matokeo yake ki roho na kimwili ni yapi?
Yes ni agano. Ile damu iliyo mwagika baada ya tendo inatamka juu ya ardhi kwamba wewe ulie mbikiri mwanamke huyo ndio mume halali wa mwanamke huyo ambae unatambulika katika ulimwengu wa rohoni.

Ukioa mwanamke ambae sio bikra jua kwamba umeoa mwanamke ambae sio mke wako
 
kuna semester moja wakati nipo chuo ilikuwa ngumu sana kwangu,nikajiapiz kwa rafiki yangu(in joking way) kwamba nikichomoka bila supplementary nitachinja kuku ninywe supu kujipongeza, bt sikufanya hivyo... 😂
 
But still bado damu za wanyama zinafanya kazi kama kawaida . Hazijapteza nguvu za kiagano " covenant power". Ni kanuni ambayo haiwezi kuvunjika.
Ukija kwa namna hii ntakuelewa.

Damu yoyote ina nguvu za kiroho, ila kwa Wakristo haturuhusiwi kumwaga au kutumia damu ya kiumbe chochote kwa lengo la kufanya ibada kwani Yesu alishamwaga damu pale msalabani kwaajili yetu.
 
Back
Top Bottom