Operesheni dhidi ya magari mabovu kuanza Juni 6, 2021

Operesheni dhidi ya magari mabovu kuanza Juni 6, 2021

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, ameelekeza Makamanda wa Polisi nchini kufanya operesheni dhidi ya magari mabovu ambayo hayapaswi kuwepo barabarani rasmi kesho, ili kuwahakikishia usalama watumiaji wa vyombo vya moto na kuepuka ajali za barabarani.



ig%20s.jpg

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro
IGP Sirro amesema hayo leo wakati wa kikao kazi cha kufanya tathmini, mafanikio na changamoto ambapo pia ameelekeza kufanyika kwa operesheni ya mwezi mmoja kwa nchi nzima ili kubaini mianya ya uhalifu na wahalifu.

“Nimeelekeza operesheni ya usalama barabarani, kuna makosa ya barabarani yameanza kujitokeza kama mnavyoona ajali iliyotokea Mbeya, Shinyanga, operesheni dhidi ya magari mabovu nayo itaanza kesho, nawaambia ma RTO, wakuu wa matraffik mikoa yote kufanya operesheni dhidi ya magari mabovu ambayo hayatakiwi kuwepo barabarani” amesema IGP Sirro

Awali akitoa tathimini za operesheni ya wiki moja iliyofanyika jijini Dar es Salaam, IGP Sirro amesema wamefanikiwa kukamata silaha za moto pamoja na wahalifu waliokuwa wakijihusisha katika matukio mbalimbali ya kihalifu.

“Wananchi wa Dar es Salaam wametoa ushirikiano mkubwa sana kwa jeshi la polisi tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, silaha nyingi zimekamatwa wahalifu wengi wamekamatwa, nimeongea na wenyeviti wa mtaa na watendaji Kata wote wa Dar es Salam, tumekuwa na mafanikio makubwa nafikiri wana Dar es Salaam wameona, leo tunahitimisha operesheni lakini tunaanza operesheni nyingine tena ya mwezi mzima na ni nchi nzima” amesema IGP Sirro

Hata hivyo IGP Sirro ameendelea kuwaasa wahalifu waliotoka kutokujihusisha na uhalifu wowote kwani Jeshi la Polisi halitosita kuwachuulia hatua za kisheria mara watapojikita katika kufanya uhalifu.
 
gari bovu ni gari ambalo likoje? wataangalia nini kujua ubovu wa gari ilhali lipo barabarani? hakuna gari bovu linalotembea
 

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, ameelekeza Makamanda wa Polisi nchini kufanya operesheni dhidi ya magari mabovu ambayo hayapaswi kuwepo barabarani rasmi kesho, ili kuwahakikishia usalama watumiaji wa vyombo vya moto na kuepuka ajali za barabarani.



ig%20s.jpg


IGP Sirro amesema hayo leo wakati wa kikao kazi cha kufanya tathmini, mafanikio na changamoto ambapo pia ameelekeza kufanyika kwa operesheni ya mwezi mmoja kwa nchi nzima ili kubaini mianya ya uhalifu na wahalifu.

“Nimeelekeza operesheni ya usalama barabarani, kuna makosa ya barabarani yameanza kujitokeza kama mnavyoona ajali iliyotokea Mbeya, Shinyanga, operesheni dhidi ya magari mabovu nayo itaanza kesho, nawaambia ma RTO, wakuu wa matraffik mikoa yote kufanya operesheni dhidi ya magari mabovu ambayo hayatakiwi kuwepo barabarani” amesema IGP Sirro

Awali akitoa tathimini za operesheni ya wiki moja iliyofanyika jijini Dar es Salaam, IGP Sirro amesema wamefanikiwa kukamata silaha za moto pamoja na wahalifu waliokuwa wakijihusisha katika matukio mbalimbali ya kihalifu.

“Wananchi wa Dar es Salaam wametoa ushirikiano mkubwa sana kwa jeshi la polisi tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, silaha nyingi zimekamatwa wahalifu wengi wamekamatwa, nimeongea na wenyeviti wa mtaa na watendaji Kata wote wa Dar es Salam, tumekuwa na mafanikio makubwa nafikiri wana Dar es Salaam wameona, leo tunahitimisha operesheni lakini tunaanza operesheni nyingine tena ya mwezi mzima na ni nchi nzima” amesema IGP Sirro

Hata hivyo IGP Sirro ameendelea kuwaasa wahalifu waliotoka kutokujihusisha na uhalifu wowote kwani Jeshi la Polisi halitosita kuwachuulia hatua za kisheria mara watapojikita katika kufanya uhalifu.
Gari bovu linawezaje kutembea barabarani? Wanatafuta upigaji na nasikia mgao wake huenda mpaka ngazi ya juu kabisa
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Gari mbovu ni ipi. Gari mbovu zimepaki majumbani au kwenye magareji. Huyo traffic lazima anipe majibu yakuniridhisha pasi na shaka kuwa gari yangu ni mbove ili hali iko barabarani
 

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, ameelekeza Makamanda wa Polisi nchini kufanya operesheni dhidi ya magari mabovu ambayo hayapaswi kuwepo barabarani rasmi kesho, ili kuwahakikishia usalama watumiaji wa vyombo vya moto na kuepuka ajali za barabarani.



ig%20s.jpg


IGP Sirro amesema hayo leo wakati wa kikao kazi cha kufanya tathmini, mafanikio na changamoto ambapo pia ameelekeza kufanyika kwa operesheni ya mwezi mmoja kwa nchi nzima ili kubaini mianya ya uhalifu na wahalifu.

“Nimeelekeza operesheni ya usalama barabarani, kuna makosa ya barabarani yameanza kujitokeza kama mnavyoona ajali iliyotokea Mbeya, Shinyanga, operesheni dhidi ya magari mabovu nayo itaanza kesho, nawaambia ma RTO, wakuu wa matraffik mikoa yote kufanya operesheni dhidi ya magari mabovu ambayo hayatakiwi kuwepo barabarani” amesema IGP Sirro

Awali akitoa tathimini za operesheni ya wiki moja iliyofanyika jijini Dar es Salaam, IGP Sirro amesema wamefanikiwa kukamata silaha za moto pamoja na wahalifu waliokuwa wakijihusisha katika matukio mbalimbali ya kihalifu.

“Wananchi wa Dar es Salaam wametoa ushirikiano mkubwa sana kwa jeshi la polisi tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, silaha nyingi zimekamatwa wahalifu wengi wamekamatwa, nimeongea na wenyeviti wa mtaa na watendaji Kata wote wa Dar es Salam, tumekuwa na mafanikio makubwa nafikiri wana Dar es Salaam wameona, leo tunahitimisha operesheni lakini tunaanza operesheni nyingine tena ya mwezi mzima na ni nchi nzima” amesema IGP Sirro

Hata hivyo IGP Sirro ameendelea kuwaasa wahalifu waliotoka kutokujihusisha na uhalifu wowote kwani Jeshi la Polisi halitosita kuwachuulia hatua za kisheria mara watapojikita katika kufanya uhalifu.
Daaa! Mikoani ni majanga makubwa sana!
 
Fursa hiyo...

Ushauri usikose kutembea na 5000

Ova
 
Wanakagua mpaka sensor mbovu kuna gari ya boss wangu ina rain sensor na parking sensor mbovu🤣🤸🐒
 
Back
Top Bottom