wanathiimba wenzangu, tukubali tu, tujipange kwa msimu ujao, takataka nyingi saana za kuondolewa simba, eneo la katikati limechoka, ukweli ambao watu wanaukataa kila siku, midfilder zetu zipo zipo tu, usahihi wa pasi mdogo, akipiga pasi 10, 5 anapatia 5 anakosea na katika hizo 5 hakuna ya kushambulia ni changamoto kwa kweli, niliwahi kusema msimu upo mwanzoni, tunashinda kwa sababu ya uwezo binafsi wa kina chama na phiri pale mbele.
Bado hatuna midfild wa ziada benchi, benchi letu nafasi ya midfild huwa kama hakuna mtu, hawazidi wawili, wengine kiasili ni mabeki..
Benchi yupo boko,sakho,banda, kenedy, nyoni nafasi za mbele ni wengi, hivyo midfild zetu uchwara zikifeli tu, hakuna namna inabidi azike babu erasto au mkude(morali yake ya upambanaji imeshuka)
Kale ka nelson okwa tulikadharau ila ni kamidfild kisheti, kanapiga pasi anafatilia pasi yake, anaugawa uwanja, anatembea na timu, anapiga pasi za kumiliki mpira(kusambaza upendo), anapiga pasi za mashambulizi, bahati mbaya walikuwa wanampanga namba 10 ufanisi wake ukawa mdogo, nasi pia viongozi uvumilivu hawana, mwishowe akaja sawadogo, bora ya mimi nisiye na mazoezi kuliko sawa dogo mwenye mazoezi
Jingine hivi phiri hajapona majeruhi au kakosea nini hasa, yaani kocha anaona boko bora kuzidi... staajabu ya musa uone ya firaauni.