Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama alimtelekeza mtoto wake na hajapata malezi ya wazazi hapo sawa inakuwa ngumu kuwakumbuka...lakini kama wazazi waliangaika na wew kwa namna yoyote...ni vzuri kuwakumbuka hata kwa kidogo utakacho jaliwa....kumbuka mzazi anapokushukuru anakuombea zaidi na anakufungulia milango ya baraka zaidi...Point sana Mkuu, yaani nimekupenda sana, kweli yaan wazazi wetu hawa waache tu wabaki kuwa wazazi ila kuna mambo mengine aiseeh hapana hata kama wametuzaa ila too much, unakuta kakutekeleza miaka kibao umehustle wee ukafanikiwa badae wanaanza ooh maneno kibao
Sasa pn hana pesa afanyajee,sio lazima halaf inategemeaa na moyo wa mtu!!!
mi na wazazi wangu tunaelewana vizuri sana,wamenipa elimu,na bado wananisaidia na kunikumbuka,na pia mi nawasaidia pale napokuwa na uwezo,sometimes nawasaidia hata bila wao kuniambia maana mapungufu mengine mtu unayaona tu hata bila kuambiwa.Daah! Sijaamini kama we ndo unaongea hayo maneno..... Hakika kazi ipo hapa.!!!!! Hivi wewe uhusiano wako na wazizi wako upo poa kwaeli??!!!! Hivi we unaona huyo mzee hapo angeweza kumpa mtaji gani ye mwenyewe anaitaji mtaji.
We unaona maisha anayoishi Namsoma hapa mjini ni sawa wazizi wake kuishi kama inavoonekana hapo?? DAh yani nina maswali mengi kweli kwako but nachoka tu kuandika mana hata sina uhakika kama hata utanielewa maana unaonesha hulewi hadi bakora wewe.
Yaaaakkkhhhh..... Ngoja niishie hapa nsije tapika mie.
Sasa tuhitimishe hakuna mtu anayejuwa back ground yao.wapo wazazi wanatelekeza watoto wao wakishaona kuwa ana kipato ndio anamsogelea na kuanza kulalamika.naamini wazazi wanaojuwa wajibu wao kwa watoto wao hawalalamiki hadharani.
Uko sahihi mimi ni mmoja pia niliotelekezwa na mshua nikiwa na miaka 2 tu pamoja na dada zangu.
Sasa hivi simu zinaingia kwa kasi kueleza wana shida wengine wanajitambulisha baba wadogo ata sijawai kuwaona.
Hata kama kusomesha wadogo zake si jukumu lake sidhani kama kuna binadam atapenda kuona familia yake bado inateseka kwa njaa au ata ada ya shule ya kata hawawezi kumudu hali ya kuwa yeye anabadilisha magari mjini na kuhudumia wasanii ata kama wazazi hawakukusomesha.
Kukuleta duniani na kukulea pekee ni jambo kubwa.
Shangaa eti matatizo yake anamlaumu mwanae kati ya baba na mtoto nani alitangulia kuiona dunia?yeye kama ujana wake hakutengeneza maisha,mwanae sio lazima amsaidie na yeye mtoto ana familia yake.Nawashangaa sana wazazi ambao huwa wanawalaumu watoto wao eti wamesahaulika.
Utakuwa hajamsomesha hata mtoto,hajampa hata mtaji wa kutafuta maisha,leo mtoto akitoka baada ya kumpa support zaidi anabaki kupiga tu kelele eti ametelekezwa
Shangaa eti matatizo yake anamlaumu mwanae kati ya baba na mtoto nani alitangulia kuiona dunia?yeye kama ujana wake hakutengeneza maisha,mwanae sio lazima amsaidie na yeye mtoto ana familia yake.
Mimi ndo huwa nasema wazazi ni lazima wawasaidie watoto wao,na tunawasaidia watoto wetu ni kwa ajili yao na familia zao.Sisi wazazi tunatakiwa kuandaa uzee wetu,inshort msaidie mtoto kwa ajili yake mwenyewe,kumsaidia mwanao ni lazima maana hatulazimishwi kuzaa.Mtoto nae ipo siku atakuwa baba nae atawajibika hivyo hivyo,huyu mzee anaelalamika namshangaa sana.umeongea logic mkuu, sijui watu wanalalamika kitu gani, suala la kuwasaidia wazazi ni muhimu hatujakataa ila sio kihivyo kama alicheza faulo ujana wake imekula kwake, analalamikana nn
Wazazi wengine hawana shukrani labda anataka kuishi maisha ya kifahari wkt ustaadhi nae ana majukumu yake.naona kuna wabaya wake ustaadhi wanataka kumdhalilisha