Uchaguzi 2020 Padre wa Kanisa Katoliki aliyeomba Ubunge huko Kagera kupitia CCM asimamishwa rasmi kuendelea na wito

👌
 
Tamaa Iliua Fisi.
Mtaka Yote Kwa Pupa Hukosa Yote.
😁😃😄😅😂
 
Mungu Ni Mwema Wakati Wote
Kwa Nyakati Mbalimbali Ataabudiwa Katika Roho Na Kweli
 
Ipi ifuatwe Katiba ya nchi inayo mpa mwananchi Hakj ya kuchagua na kuchaguliwa, au Katiba ya Kanisa Katoliki inayo weka Mipaka?!
Ukiingia ndani sanaaaaa yani namaanisha ndani sanaaaaa utagundua kuwa katiba ya katoliki inanguvu na inaheshimika kuliko katiba ya nchi ila ndio hadi uingie ndan sanaaaa
 
Na hiyo ni Kawaida sana, Hata wale wenye Michepuko Kiroho wamejiondoa kwenye Hiyo taaluma na hata wanaitamani siasa kama yule wa Kagera yule Mnyarwanda ambaye kucha anitukuza Chadema badala ya Mungu.
 
Km kichwa kinavyojieleza,Kwa mujibu wa barua ya Askofu Rwoma wa Jimbo Katoliki la Bukoba,amesimamishwa kazi kwanza kutokana na kukiuka taratibu za Kanisa Katoliki kushiriki mambo ya Kisiasa kwenye Uchaguzi mkuu wa Mwaka huu,ambapo inasemekana pia alishindwa ktk kura za maoni za Ubunge-CCM,Aidha inasemekana kuwa alikuwa ameshamwandikia Askofu wake kuhusu kuacha Upadre.Tumwombee ili ajitafakari upya,Inawezekana ni ibilisi amempitia,na km yupo humu JF basi namshauri kuwa Km Wana Kanisa bado tunamhitaji,ajirudi akamwombe msamaha Askofu wake kwa niaba ya Kanisa,naamini atarudi tena ktk utume.Mungu mwenye nguvu akamguse ili aweze kujirudi.Hii ni barua ya Askofu wake inayomsimamisha Upadre.
 
Nyoko unadhani kirahisi hivyo?
 
Mkuu kwani ukitumia lugha nzuri kuna ubaya?.Hapo kuna mambo mawili,mosi aliandika barua ya kuacha Upadre kwa hiari yake,pili aliamua kugombea ubunge pasipo kibali cha Askofu wake,Ktk barua hii Askofu anarejea ktk sheria za Kanisa kuwa kwa kugombea ubunge anamsimamisha Upadre,hivyo barua ya Askofu imejikita hasa kwenye kujihusisha na siasa,kwa lugha nyingine bado ana muda wa kujitafakari na kubadilisha gia akiwa angani.
 
Tanzania haina Kadinali bado. Ruwaichi ni Askofu mkuu. Pia bado Pengo hajaagwa kwa misa takatifu!
Kanisa Katoliki la Tanzania bado linaye kardinali, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo. Ukardinali ni title ya kudumu kama Padre au Doctor, hata akistaafu madaraka yake anabaki na daraja yake hiyo kama ilivyo, na haitwi 'kardinali mstaafu', kama ambavyo hujawahi kusikia title ya 'dokta mstaafu'. Alichostaafu Kardinali Pengo ni uongozi wa jimbo kuu la Dar es salaam, ambao amekabidhi kwa Askofu Mkuu Yuda Tadei Ruwa'ichi.
Katika itifaki ya kanisa katoliki, bado Kardinali Pengo yuko juu ya wakleri wote ki-hairakia (hierarchy), akifuatiwa na maaskofu wakuu, maaskofu, maaskofu wasaidizi na kuendelea kwa mfuatano huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…