Padri Kitima: Viongozi wa dini mkiendelea kukaa kimya juu ya matukio ya watu kuuawa maovu haya yataendelea nchi hii

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Tanzania, Padre Charles Kitima awavaa viongozi wa dini kwa kushindwa kukemea maovu yanayoendelea nchini humo hasa kupotezwa kijana Soka na wenzake, kuuawa kwa Mzee Kibao, awakemea wanaosema wasichanganye dini na siasa, awataka viongozi kujua mifumo yote mibovu na kutaka ifanyiwe mabadiliko kama ambavyo Deusdetith Soka alivyokuwa anafanya.

"Soka alikuwa anatetea demokrasia, kuchambua mifumo mibovu, haina ubaya wowote, unaweza ukazidisha ni wazi asa kama ni kijana tena si anajifunza ni kumlea si kumpoteza, sasa ameuawa na nani?inaweza ikawa ni majambazi, tusimzingizie mtu" - Padre Kitima.

Soma pia: Mwaka 2018 na Nyaraka 3 za Viongozi wa Dini juu ya Mustakabali wa Nchi yetu


Your browser is not able to display this video.


Video: Jambo TV
 
halafu eti mtu anapewa PhD ya heshima ya uongozi!
 
Mbona kuna ukimya sana kuhusu Soka. Yupo wapi?

Uchunguzi wa haraka wa Mzee Kibao umeishia wapi?
 
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania, Padre Dkt. Charles Kitima, akionyesha kushangazwa na kitendo cha viongozi wa Dini kuwa kimya katika kukemea vitendo vya mauaji na kuteka watu vinavyoendelea nchini.
Your browser is not able to display this video.
 
actualy,
hata kanisa katoliki likiendelea kuhubiri chuki na migawanyiko kwa hisia za kisiasa, waamini wake watachoka na watagawanyika na hivyo kanisa kupasuka

unafiki sio kitu kizuri katika imani
 
Kwa hili nawaheshimu sana TEC waambie watu wanachopaswa kusikia sio wanachotaka kusikia haya ndiyo mahubiri yaliyo bora na yenye kujenga
 
Huo ndio ukweli, wa
Huo ndio ukweli, wawatetee wananchi dhidi ya wauaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…