Pakistan na siasa za aina yake, uongozi huko ni jasho na damu

Pakistan na siasa za aina yake, uongozi huko ni jasho na damu

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Hili taifa miaka yote tangu kuanzishwa kwake huwa liko katika migogoro ya kisiasa.

Mawaziri wake wakuu rasmi wote 18 waliowahi kuingia madarakani hakuna aliyewahi kumaliza awamu yake ya uongozi.

Lazima moja kati ya kuuwawa, kupinduliwa, kuondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani au kujiuzulu na kukimbia ofisi mwenyewe!

Imran Khan waziri mkuu maarufu sana nayo yamemkuta hayo hayo na sasa jeshi linataka kumpiga pini asirudi kwenye siasa tena.

Marais wake wote nao ilikuwa hivyo hivyo kama yaliyowakuta mawaziri wakuu kabla ya kupunguza madaraka ya Ofisi ya Rais na kumfanya kuwa ceremonial tu mwaka 2010.

Jeshi na Idara ya Usalama ya Taifa wanapewa billion za dola kila mwaka na Marekani kupambana na ugaidi ila wako na misuguano kila wakati na Marekani kwamba hawafanyi kazi yao na badala yake wanaotoa hifadhi kwa magaidi wengi. Uhusiano ulikuwa mbaya zaidi ilipokuja kugundulika Osama Bin Laden alikuwa anaishi umbali wa nusu maili tu kutoka chuo kikuu cha jeshi la Pakistan na Marekani wakafanya operation ndani ya nchi yao bila kuitaarifu serikali ya Pakistan.

Pakistan pamoja na kuwa taifa la kidini ndio kitovu cha biashara ya Opium inayolimwa Afghanistan ambayo inayotumika kutengeneza dawa za kulevya za Heroin na Morphine.

Wao pia kama majirani zao na mahasimu wao India wanamiliki silaha za nuclear pamoja na kuwa ni taifa la hovyo sana.
 
Dini yenyewe mashaka matupu , sitasahau walipomuwasha risasi waziri mkuu Benazir Bhuto 2007
 
Hamna nchi inayoongozwa na watu wa hii dini na ikatulia..... Ni mwendo wa misukosuko tu.
 
Hili taifa miaka yote tangu kuanzishwa kwake huwa liko katika migogoro ya kisiasa.

Mawaziri wake wakuu rasmi wote 18 waliowahi kuingia madarakani hakuna aliyewahi kumaliza awamu yake ya uongozi.

Lazima moja kati ya kuuwawa, kupinduliwa, kuondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani au kujiuzulu na kukimbia ofisi mwenyewe!

Imran Khan waziri mkuu maarufu sana nayo yamemkuta hayo hayo na sasa jeshi linataka kumpiga pini asirudi kwenye siasa tena.

Marais wake wote nao ilikuwa hivyo hivyo kama yaliyowakuta mawaziri wakuu kabla ya kupunguza madaraka ya Ofisi ya Rais na kumfanya kuwa ceremonial tu mwaka 2010.

Jeshi na Idara ya Usalama ya Taifa wanapewa billion za dola kila mwaka na Marekani kupambana na ugaidi ila wako na misuguano kila wakati na Marekani kwamba hawafanyi kazi yao na badala yake wanaotoa hifadhi kwa magaidi wengi. Uhusiano ulikuwa mbaya zaidi ilipokuja kugundulika Osama Bin Laden alikuwa anaishi umbali wa nusu maili tu kutoka chuo kikuu cha jeshi la Pakistan na Marekani wakafanya operation ndani ya nchi yao bila kuitaarifu serikali ya Pakistan.

Pakistan pamoja na kuwa taifa la kidini ndio kitovu cha biashara ya Opium inayolimwa Afghanistan ambayo inayotumika kutengeneza dawa za kulevya za Heroin na Morphine.

Wao pia kama majirani zao na mahasimu wao India wanamiliki silaha za nuclear pamoja na kuwa ni taifa la hovyo sana.
Nilikuwa natazama documentary fulani jamaa wa CIA anakwambia, whatever happens in Pakstan has two or three story versions.
Alikuwa anatoa kisa fulani ambapo jamaa wa alqaeda alikamatwa huko na jeshi la pakstan akakabidhiwa kwa wamarekani. Story official waliyopewa inatofautiana na mashuhuda. Yani inaelekea jamaa walikuwa naye siku nyingi tofauti na walivyowaambia wamarekani.
Sema Imran Khan inaelekea raia wanamkubali sana.
 
Hamna nchi inayoongozwa na watu wa hii dini na ikatulia..... Ni mwendo wa misukosuko tu.
Oman, Qatar, UAE mbona kumetulia? Hata Brunei kumetulia na watu wanakula maisha vizuri kabisa. Hata Saudi Arabia ukiondoa uhasama wake na Syria ila amani fresh tu.
 
Nilikuwa natazama documentary fulani jamaa wa CIA anakwambia, whatever happens in Pakstan has two or three story versions.
Alikuwa anatoa kisa fulani ambapo jamaa wa alqaeda alikamatwa huko na jeshi la pakstan akakabidhiwa kwa wamarekani. Story official waliyopewa inatofautiana na mashuhuda. Yani inaelekea jamaa walikuwa naye siku nyingi tofauti na walivyowaambia wamarekani.
Sema Imran Khan inaelekea raia wanamkubali sana.
Jeshi halimtaki tena karibu na mamlaka kwa sababu alishaonyesha nia madhubuti ya kuliondoa katika siasa, ugomvi utakuwa mbaya zaidi wafuasi wake wakikomaa. Mwaka jana alipigwa risasi ya mguu katika maandamano.
 
Jeshi halimtaki tena karibu na mamlaka kwa sababu alishaonyesha nia madhubuti ya kuliondoa katika siasa, ugomvi utakuwa mbaya zaidi wafuasi wake wakikomaa. Mwaka jana alipigwa risasi ya mguu katika maandamano.
Yes, mkuu maana inaelekea ukienda against jeshi basi kwisha habari yako.
Wanaweza kumuua kama hadi kala shaba ga mguu.
Jeshi likishaonja madaraka kuondoka mazima huwa ngumu kama Myanmar
 
Back
Top Bottom