Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Serikali ya Pakistan imeanzisha sheria mpya ya uhalifu wa mtandaoni ambayo inaweza kuwafanya watumiaji wa mitandao ya kijamii kufungwa hadi miaka mitano jela kwa kuchapisha "habari za kughushi " kuhusu jeshi, mahakama au maafisa wa umma.
Sheria hiyo iliidhinishwa na baraza la mawaziri la Waziri Mkuu Imran Khan na kupitishwa haraka kuwa sheria na Rais Arif Alvi.
Hata hivyo wakosoaji wanasema sheria hiyo ni sehemu ya hatua za kubinya uhuru wa kujieleza katika taifa hilo.
Tume ya Haki za Kibinadamu ya Pakistan, imeitaja sheria hiyo kuwa kinyume cha kidemokrasia.
Adhabu ya juu pia imeongezwa kutoka miaka mitatu hadi mitano na watuhumiwa hawatapewa dhamana, kwa maana hiyo mshitakiwa atasubiri kusikilizwa kwa kesi yake gerezani. Muungano wa Shirikisho la Wanahabari wa Pakistan umeapa kupinga marekebisho hayo mahakamani.
DW
Sheria hiyo iliidhinishwa na baraza la mawaziri la Waziri Mkuu Imran Khan na kupitishwa haraka kuwa sheria na Rais Arif Alvi.
Hata hivyo wakosoaji wanasema sheria hiyo ni sehemu ya hatua za kubinya uhuru wa kujieleza katika taifa hilo.
Tume ya Haki za Kibinadamu ya Pakistan, imeitaja sheria hiyo kuwa kinyume cha kidemokrasia.
Adhabu ya juu pia imeongezwa kutoka miaka mitatu hadi mitano na watuhumiwa hawatapewa dhamana, kwa maana hiyo mshitakiwa atasubiri kusikilizwa kwa kesi yake gerezani. Muungano wa Shirikisho la Wanahabari wa Pakistan umeapa kupinga marekebisho hayo mahakamani.
DW