Pakistan yapiga marufuku matangazo ya mikutano ya Imran Khan

Pakistan yapiga marufuku matangazo ya mikutano ya Imran Khan

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
1661163732464.png

Mamlaka ya udhibiti wa vyombo vya habari vya utangazaji ya Pakistan, PEMRA, imezipiga marufuku televisheni nchini humo kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mkutano wa waziri mkuu wa zamani Imran Khan aliopanga kuufanya hii leo.

Marufuku hiyo ilitolewa jana jioni, ikiwa ni siku ambayo Khan alifanya mkutano mjini Islamabad. Khan alitumia mkutano huo kuwakosoa maafisa wa polisi na mahakama juu ya kukamatwa kwa mmoja wa viongozi wa chama chake.

Serikali imesema katika katazo lake kwamba Khan anatoa madai yasiyo na msingi na kueneza kauli za uchochezi. Tangu aondolewe madarakani kupitia kura ya kutokuwa na imani naye, nyota huyo wa mchezo wa Kriketi amefanya mfululizo wa maandamano ya kuipinga serikali.

Khan anatarajiwa kufanya mkutano mwingine leo jioni katika mji jirani na Islamabad.
 

Mamlaka ya udhibiti wa vyombo vya habari vya utangazaji ya Pakistan, PEMRA, imezipiga marufuku televisheni nchini humo kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mkutano wa waziri mkuu wa zamani Imran Khan aliopanga kuufanya hii leo.

Marufuku hiyo ilitolewa jana jioni, ikiwa ni siku ambayo Khan alifanya mkutano mjini Islamabad. Khan alitumia mkutano huo kuwakosoa maafisa wa polisi na mahakama juu ya kukamatwa kwa mmoja wa viongozi wa chama chake.

Serikali imesema katika katazo lake kwamba Khan anatoa madai yasiyo na msingi na kueneza kauli za uchochezi. Tangu aondolewe madarakani kupitia kura ya kutokuwa na imani naye, nyota huyo wa mchezo wa Kriketi amefanya mfululizo wa maandamano ya kuipinga serikali.

Khan anatarajiwa kufanya mkutano mwingine leo jioni katika mji jirani na Islamabad.
Huyu mzee wamzibiti vizuri anataka kuharibu utulivu wa nchi.
 

Mamlaka ya udhibiti wa vyombo vya habari vya utangazaji ya Pakistan, PEMRA, imezipiga marufuku televisheni nchini humo kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mkutano wa waziri mkuu wa zamani Imran Khan aliopanga kuufanya hii leo.

Marufuku hiyo ilitolewa jana jioni, ikiwa ni siku ambayo Khan alifanya mkutano mjini Islamabad. Khan alitumia mkutano huo kuwakosoa maafisa wa polisi na mahakama juu ya kukamatwa kwa mmoja wa viongozi wa chama chake.

Serikali imesema katika katazo lake kwamba Khan anatoa madai yasiyo na msingi na kueneza kauli za uchochezi. Tangu aondolewe madarakani kupitia kura ya kutokuwa na imani naye, nyota huyo wa mchezo wa Kriketi amefanya mfululizo wa maandamano ya kuipinga serikali.

Khan anatarajiwa kufanya mkutano mwingine leo jioni katika mji jirani na Islamabad.
Naona wamedhamiria kumnyoosha.
 
Tangu aende kumuona Putin na kumpiga nae selfie ndio ulikuwa mwisho wake wa kutawala Pakistan.

Muda siyo mrefu atapata fatal accident
 
Back
Top Bottom