Pale unaona abiria mwenzako kwenye daladala wanakimbilia kutoka mlangoni na madirishani

Usher-smith MD

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2015
Posts
9,558
Reaction score
12,335
Nimshukuru Mungu kwa kulinda leo πŸ™πŸΎπŸ™πŸΎπŸ™πŸΎ

Leo hii saa 4 usiku nipo siti ya mwisho kabisa kwenye daladala ya kutokaea Kongowe kwenda Mbagala Rangi 3 kwenye kilima kile baada ya mto kufika Rangi 3 Ghafla naona abiria wenzangu wanakimbilia mlangoni, wengine wanatokea madirishani wengine wanaruka mlangoni.

Nami nikatoka nduki kwenda mlangoni ila sikufanikiwa kutoka maana dereva wa daladala alikuwa anarudi reverse.

Ndio nachungulia mbele naona Malori mawili yanatumbukia moja mtalo wa kulia lingine kushoto na bajaji moja mbele yetu mtalo wa kulia.

Kumbe Lori moja limefeli breki likawa inarudi nyuma. Dereva wa Lori la pili akarudi nyuma kukwepa ndio kuingia mtaloni.

Kama wale madereva waliingizwa malori yao mtaloni makusudi ili wasitusombe magari ya nyumba Mungu awabariki maana sijui ingekuwaje leo.

Yule dereva Bajaji pole yake nadhani hamna aliyeumia kwenye Bajaji.

Asante Mungu, naomba nifike salama leo nyumbani bado naungaunga daladala hadi Pugu usiku huu πŸ™πŸΎπŸ™πŸΎπŸ™πŸΎ
 
Nami nikatoka nduki kwenda mlangoni ila sikufanikiwa kutoka maana dereva wa daladala alikuwa anarudi reverse.
Ndio nachungulia mbele naona Malori mawili yanatumbukia moja mtalo wa kulia lingine kushoto na bajaji moja mbele yetu mtalo wa kulia.
Mbona enzi za malori ya Scania, Leyland, Benz, Fiat ajali za namna hii hazikuwepo
 
Kwa taarifa yako hapo mto Mzinga ni jambo la kawaida, kupita salama si kawaida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…