Palestina wachukua uamuzi wa kiume, wakataa kilemba cha ukoka

Palestina wachukua uamuzi wa kiume, wakataa kilemba cha ukoka

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Waziri wa mambo ya nje wa Palestina Riyad al-Maliki amekataa kuchukua uenyekiti wa jumuiya ya nchi za kiarabu unaozunguka ikiwa ni kupinga kitendo cha baadhi ya nchi za kiarabu kurudisha uhusiano na Israel taifa linalokalia ardhi zao na kuwanyima haki za kuishi.

Amesema kuna heshima gani kwa sisi kuongoza jumuiya ambayo tutakapokuwa mwenyekiti na wao wanaongeza kasi kurudisha uhusiano na adui yetu.

Hatua hiyo ya palestina imekuja sambamba na msimamo wa rafiki mwengine wa karibu wa Palestina,nchi ya Qatar kutoa msimamo wake wa kulaumu jumuiya ya kimataifa ya kutokuikemea Israel iliyoshindwa kutekeleza maazimio yote ya Umoja wa Mataifa kuhusiana na Palestina na wakati huo huo ikiendelea na uvunjaji zaidi wa haki za wapalestina na huku wakiendelea kuwavunjia majumba yao na kuteka ardhi finyu iliyobaki mikononi mwa wapalestina.Kauli hiyo imetolewa hapo juzi na kiongozi wa Qattar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani kwenye kikao cha 75 cha baraza kuu la UN.
1600850296192.png
 
Kutangaza kuifuta Israel kwenye uso wa duniani was one of the biggest mistakes ever!

Kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila hilo kutekelezeka;

na kwa kuwa ardhi ile alipewa Ibrahim kuwa miliki yake na kizazi chake milele;

na kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila yodi wala nukta moja ya Torati kutanguka;

hivyo basi, wenye akili wamegundua kuendelea kushupaza shingo ni kujilisha upepo.

Ni busara Palestina ikaungana na waarabu wenzie wenye nia njema kutafuta amani na Israel kwa faida yao wenyewe na vizazi vyao kwani hayo wanayoyatamani na kuyataka hayatokaa yatimie hadi kiama!
 
Palestina yenyewe ishachokwa kitambo ndio wakati wake wakutokomezwa. Hana ubavu wa Kushindana na Arabs Country pia Palestina ni Omba omba tu.
 
Wanataka kuifuta Israel katika uso wa dunia; hayo mengine sijui kama wataelewa.
Imposibooo, ila hili tatizo litadumu Milele!!!
Take my word, hata ulimwengu wote wa SIGN peace agreement. Palestine pippo watapambana hadi...
 
... kutangaza kuifuta Israel kwenye uso wa duniani was one of the biggest mistakes ever!

Kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila hilo kutekelezeka;

na kwa kuwa ardhi ile alipewa Ibrahim kuwa miliki yake na kizazi chake milele;

na kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila yodi wala nukta moja ya Torati kutanguka;

hivyo basi, wenye akili wamegundua kuendelea kushupaza shingo ni kujilisha upepo.

Ni busara Palestina ikaungana na waarabu wenzie wenye nia njema kutafuta amani na Israel kwa faida yao wenyewe na vizazi vyao kwani hayo wanayoyatamani na kuyataka hayatokaa yatimie hadi kiama!
Unaleta hadithi za kusadikika??? Mzee baba!
 
... kutangaza kuifuta Israel kwenye uso wa duniani was one of the biggest mistakes ever!

Kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila hilo kutekelezeka;

na kwa kuwa ardhi ile alipewa Ibrahim kuwa miliki yake na kizazi chake milele;

na kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila yodi wala nukta moja ya Torati kutanguka;

hivyo basi, wenye akili wamegundua kuendelea kushupaza shingo ni kujilisha upepo.

Ni busara Palestina ikaungana na waarabu wenzie wenye nia njema kutafuta amani na Israel kwa faida yao wenyewe na vizazi vyao kwani hayo wanayoyatamani na kuyataka hayatokaa yatimie hadi kiama!
Kauli ipo pale pale na wao wwnyewe mpaka ww shabiki unalielewa iko day ifafika
 
Mungu wa Yakobo aibariki sana Israel. Neno lake litasimama milele na milele. Amen.
Kumbe kuna Mungu wa ngapi? Kuna Mungu wa Wahindi.. Mungu Wa Wafrika. Kuna Mungu wa wazungu. Wachina wa waKorea wa waarabu wa Jua wa mwezi na wawanyama! Eeeeh pole Mungu..wee
 
Back
Top Bottom