Pamba Jiji yapata ajali

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Basi la wachezaji wa Pamba Jiji FC limepata ajali katika eneo la Bahi mkoani Dodoma majira ya saa 11 alfajiri wakati kikosi hicho kikiwa safarini kutoka Bukoba kuelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mchezo wa Kombe la CRDB Federation dhidi ya Kiluvya United Machi 11, 2025.


Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo imesema chanzo cha ajali hiyo ni kugongwa na lori hivyo kupelekea mshtuko kwa baadhi ya wachezaji.

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetuma salamu za pole kwa timu hiyo kufuatia ajali hiyo.
 
Inaonekana walikuwa kwenye mwendo mkubwa
 
Huu umasikini ni mbaya sana. Timu kama ile ilitakiwa isafiri kwa ndege toka Bukoba. Kama timu haina ndege zake basi ichukue ndege za kukodi zipo. Timu inasafiri umbali kwa basi, are they sirious?
 
Huu umasikini ni mbaya sana. Timu kama ile ilitakiwa isafiri kwa ndege toka Bukoba. Kama timu haina ndege zake basi ichukue ndege za kukodi zipo. Timu inasafiri umbali kwa basi, are they sirious?
Team inasafirisha watu kwa Special Hire 😃
 
Hii sasa ndo dharula yenye uwezo wa kughairisha mechi


Siyo wale "mbuzi" waliopelekwa pale uwanja wa taifa.

Pole kwa timu nzima na familia zao
 
Hii si ile pamba ya enzi za kina george masatu, nico bambaga, paul rwechungura, madata lubigisa, hii inaitwa pamba jiji, ile iliitwa pamba "tp lindanda". Wangeipa jina jingine tu na ile original ifufuliwe
 
Huu umasikini ni mbaya sana. Timu kama ile ilitakiwa isafiri kwa ndege toka Bukoba. Kama timu haina ndege zake basi ichukue ndege za kukodi zipo. Timu inasafiri umbali kwa basi, are they sirious?
Hilo nalo neno, ndege huwa hazipati ajali japo kuna timu moja Amerika kusini walikufa wachezaji wote akabaki mmoja, na Zambia vivyo hivyo ndege ilianguka baharini alibaki mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…