Pambano la Mwakinyo laahirishwa, mkanda uliokuwa unapiganiwa haukuletwa ulingoni

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Usiku wa vitasa wa leo utakuwa na mapambano nane, huku main card ikiwa ni Bondia wa Tanzania, Hassan Mwakinyo akizichapa na bondia Kutoka Ghana, Patrick Allotey ambalo ni pambano la kupambania ubingwa wa WBO, Litakuwa la Round 10

Mapambano ya utangulizi ni

1. Jamal Kunoga VS Abdallah Mahumba
Rounds: 6
Winner: Jamal Kunoga

2. Johnson Kiwia Vs Kennedy Ayoo
Rounds: 6
Winner: Kennedy Ayoo

3. Yusuphu Metu Vs Maisha Samsom (Super walter weight)
Rounds: 6
Winner: Yusuph Metu

4. Shaban Kaoneka Vs Jaylaan Muhammad
Rounds: 6
Winner: Shabaan Kaoneka

5. Amir Matumla(TZ) Vs Reagan Pacho(DRC),
Superwalter WBO
Rounds: 10
Winner: Amir Matumla.

6. Jongo Hamad Jongo Vs Alphonce MchumiaTumbo
Rounds: 6
Winner: Jongo Jongo

7. Haruna Swanga Vs Ashraf Suleiman
Round: 10
Winner: Haruna Swanga, kwa KO Round ya pili.

Ashraf Suleiman ambaye ameshindwa kwa KO amesema masuala ya kifedha na kucheleweshwa kwa pambano ni moja kati ya vitu vilivyofanya ashindwe. Hata hivyo amesema akikutana naye tena ulingoni atampiga. Pambano hili lilikuwa la heavy weight wakishindania mkanda wa TPBRC wa uzito wa juu.

8. Hassan Mwakinyo dhidi ya Patrick Allotey
Pambano kati ya Mtanzania, Hassan Mwakinyo dhidi ya Patrick Allotey la kuwania Ubingwa wa Afrika mkanda wa WBO halijafanyika kwasababu mwakilishi wa WBO Afrika, SAMIR CAPTAN hakufika ulingoni.


Pia soma:
Kamisheni ya ngumi za kulipwa Tanzania mtatuambia nini kuhusu pambano la Mwakinyo?
 
Mkuu pambano linaanza saa ngap
 
Uyo mghana anaonekana ni mtoto mchele mchele
 
Nimepumzika nyumbani nacheki TV. Mara baada ya kuhamahama channel nikakuta stesheni inaonesha ngumi.
Binafsi napenda sana mchezo huu tangu enzi zile za mwenye ngumi zake Mike Tyson.
Kuulizia main fight naambiwa ni makinyu na alotei.
Namwombea kwa Mungu bondia wetu anaewakilisha tanzania lolote limpate kwenye mpambano huu.
 
Si mulitangaza humu kwamba pambano limefutwa duu
 
Jamani live Kwa internet nachekia wapi pambano...naona link
Asnteee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…