Pamoja na mziki wao kuwa tofauti je kati ya Michael Jackson na Bob Marley nani alikubalika zaidi ulimwenguni

Mwanaume yoyote wa ukweli lazma amtangulize Bob Marley ndio afate wacko jacko. Otherwise utakuwa James delicious tuu
....... Hapa tunazungumzia perfomance nzima za wakali hawa katika nyaja ya mziki bila kutazama utofauti wa rangi, jinsia, dini, race wala chochote kile.

....... Hapa tunazungumza mambo ambayo ni halisia, yaani ule ukweli kabisa wa mambo ktk mziki wa waimbaji hao wawili hapa duniani.

....... Michael Jackson alikuwa ni mtu mwingine na endapo asingetofautiana na watu ambao walimsuka tangu akiwa kijana na akafa ktk heshima yake ya kimziki basi huenda mpaka sasa watu wangekuwa wanaingia ukumbini kwa kiingilio ili tu kusikilza nyimbo zake huku wakivuta picha ya Michael Jackson pale jukwaani.
 
Mkuu umeongea mengi ya kusimumua, ukipata muda naomba utumwagie na matukio makubwa na Michael Jackson.
 
Inatosha mkuu
 
Asiyekugongea LIKE ana matatizo.

Nimependa hapo uliposema Google ilistak kwa ajili msiba wa Michael.
 
Hebu kasikilize wimbo wa bob unaoitwa Redamption song.(kama sijakosea,unahusu uhuru wetu watu weusi).Nipo tayari kwa marekebisho wakuu.
Dah mkuu umenikumbusha "emencipate yourself from mental slavery, non but ourself can free our minds, have no fear for the atomic energy, cause non of them can stop the time..."
 
Mkuu rudi kasome upya...Mziki wa Bob Marley na wa Michael upi umesikilizwa zaidi duniani! Unachekesha sana. MJ ni mshereheshaji tu jukwaani na Bob ni philosopher. Mashairi ya Bob yanaishi. Leo hii nikikuambia uandike hata aya moja ya wimbo wa MJ yenye maana huwezi/huijui/haipo. Yule ni dancer tu.
 
Kwa mfano nini Bob aliimba ambacho ni darasa katika maisha ya kila siku, Buffalo Soldier?
Mkuu uko mbali na dunia hii, ni bora kukaa kimya kuficha ujinga. Tafuta mashairi ya Buffalo soldier, kama hujui kingereza tafuta mtu akutafsirie.
 
Mkuu unaakili sana. Nashukuru Mungu kwa kukupa muda wa kuandika yote haya. Kwa mwenye akili mada hii itakuwa imefungwa hapa.
 
Marley naye ana nafasi yake kubwa sana ktk muziki ila TAFADHARINI, M.J ni zaidi ya kila mwanamuziki duniani. Hamna mjadala hapo.
 
Mkuu wape na ile ' Ride Natty Ride' hapa alitabiri ugonjwa wa ukimwi.
 
Wote Wakali..Kila mmoja kwa nafasi yake kutokana na aina ya muziki..

Ila kwa kua mwisho wa siku mtoa hoja anataka jibu la "Nani zaidi"...Hapa inabidi kila mtu ajifanyie Litmus Test, kwa kujiuliza:

1. Mara nyingi husikia nyimbo za nani kati yao.

2. Mara ya mwisho kusikia nyimbo zao, ilikua ni ya nani kati yao.

...
Hapo utapata jibu mujarrab kabisa..

Kwa upande wangu, kwa vigezo tajwa...Bob is the Best.
 
Bob aliwahi kutunga mstari wa nyimbo akiwa jukwani pale Zimbabwe..kwenye concert ya Uhuru wa Zimbabwe lilitokea tafrani mabomu yakavurumushwa watu wakakimbia then Bob pekee akabaki jukwaani huku akiimba bila back vocal singer wala guitarist. Wanaomjua wanakwambia Bob alikuwaga hana kitu kinaitwa uoga ndio maana alipopandikizwa kansa alitakiwa akatwe kidole ili aishi lakini yeye akaopt kukubali kufa miezi kadhaa ijayo mbele.

Pia Kwenye ambush in the night alikaa tu kwenye kiti zikapigwa risasi kama 30 lakini iliishia kumjerui moja tu mkononi mwake na kesho yake akaenda kwenye tamasha kubwa zaidi la smile Jamaica akasimamisha vita vya wenyewe kwa wenyewe pale Jamaica na mahasimu wawili kisiasa wakaungana then peace and prosperity ya Jamaica ikazaliwa tena...hadi hapo wajamaica wanamuheshimu sana Marley. Very brave. Fearless, full of love, and respect.

Anyways, tuendelee na story ya Zimbabwe.

Then hali ilipotulia wakarudi jukwaani Bob akaongeza mstari ukisema hivi.."Now we see who is the real revolutionary coz I wanna be treated by mercenary." Mstari ukisema kwamba tumeona nani ana kiu ya Mapinduzi na yeye ana haki ya kuonekana kama askari wa kukodiwa na wengine waliokimbia ni waoga wa kudai Uhuru na haki zao.

Nyerere akabaki kapigwa butwaa tu. Anashangaa mvuta bangi akimkosha kwa uzuri wa kutosha.
 
Alipomaliza kuimba ile Africa Unite, Nyerere(Mtu aliyeheshimika sana duniani) alinyanyuka na kumtafuta Bob kumpa mkono.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…