Pamoja na Tanzania kununua ndege kwa matrilioni, samaki kutoka Mwanza, Tanzania, wanasafirishwa na ndege kutoka Rwanda na Ethiopia

Zikisafirishwa na dreamliner mnaanza oh ndege gani inaanza kusafirisha nyama ya mbuzi sijui nini; hivi nyie makamanda uchwara wa ufipa akili zenu zimekaaje lakini?
Mwanzo nilijua jamaa ana point,lakin baada ya kusoma maelezo yako nimekubaliana na maelezo yako.Mimi pia nina shida ya kufanyia kazi kila jambo analoamua JPM lakini baadae namuelewa.

Nadhani shida kubwa ni historia ya shirika,Kuna maeneo wametengeneza jina baya ,hivyo lazima kuwe na muda wa hali hiyo kupita.
 
Kwa kipindi cha wiki mbili tumeshuhudia Rwandair ikisafirisha minofu ya samaki kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza kwenda ulaya. Kwa nini tusitumie ndege zetu za ATCL ambazo zime-park tu? Charity begins at home!
 
Kwa kipindi cha wiki mbili tumeshuhudia Rwandair ikisafirisha minofu ya samaki kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza kwenda ulaya. Kwa nini tusitumie ndege zetu za ATCL ambazo zime-park tu? Charity begins at home!

ATCL bado hawajapata kibali cha kusafiri kwenda Ulaya.
 
Shirika la ATCL lina kibali cha kufika huko?

 
Maendeleo Hayana Chama Tujadili Kuhusu Miradi Hii Mikubwa ya Ndege na SGR Reli !

May 22, 2020

MRADI WA SGR RELI MPYA DSM - DODOMA -TABORA - ISAKA - MWANZA
Mpaka sasa serikali haijajitokeza kutueleza manufaa ya reli hii kwa uchumi wa ndani mfano kusafirisha makaa ya mawe kwenda ktk viwanda vikubwa vilivyopo ili kutumika kama nishati na hivyo reli kuchangia ongozeko la umeme viwandani


Video : Source : TRC RELI TV

Mfano wa pili kuongeza ajira za ndani kwa kusafirisha pamba toka Tabora kwenda mfano kiwanda kikubwa cha nguo A-Z Arusha ili Tanzania itengeneze nguo na kuachana na kuagiza mitumba au kusafirisha zao ambalo halijaongezwa thamani wala kuwatengenezea waTanzania ajira yaani pamba ghafi nje.

Mifano ni mingi lakini hatujasikia mikakati zaidi ya kusifia ujenzi kwa asilimia na treni ktk kipande kidogo kinachowezekana kukamilika cha SGR reli kuwa na kasi kubwa.
 
May 22, 2020
Mwanza, Tanzania

Fursa: Ethiopian Airlines Kusafirisha Minofu
Shirika lingine la ndege la Afrika limepata fursa ya kupewa kazi ya kusafirisha samaki kwenda soko la ulaya
Hii ni baada ya Rwandair kuwa shirika la kwanza Afrika Mashariki kusafirisha minofu ya samaki aina ya sagara toka Tanzania kwenda ulaya na kwa vile mzigo ni mwingi imebidi Ethiopian Airlines pia iingie kupiga kazi.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara amesisitiza viwanda 17 vya samaki Mwanza kuzalisha samaki waliotayarishwa kwa viwango vya kimataifa amesema Injinia Stella Manyanya wakati akishuhudia ujio wa Ethiopian Airlines uwanja wa ndege Mwanza, Tanzania.

Source : Mwananchi digital
 
Wewe kama mnunuzi, Utaingia mkataba na Airline company ambayo haina cargo flight ata moja? RwandAir anazo cargo flights kwahiyo case ya kuwa kwanini atcl haibebi izo fish ni kuwa mnunuzi ameamua kutumia RwandAir kwa vile yeye anangalia flexibility na reliability ya hio airline anayotaka ibebe mizigo yake btw atcl bado ni mchanga japo anakua kwa kasi kubwa na kuna sehemu bado hajawa licenced kutua na pia hana cargo flights.

The likely imekuwa kubwa ya RwandAir kusecure hilo deal mana pia na route za ulaya kama Brussels
 
Kwa hio hapo aliyeingia huo mkataba ni hao jamaa wa huko Brussels na Rwandair?
 
May 21, 2020
Mwanza, Tanzania

ONE - STOP - CENTRE, MWANZA AIRPORT TANZANIA


Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amesema kuanzishwa kwa Kituo cha Pamoja (One Stop Centre) katika uwanja wa ndege wa Mwanza kutasaidia kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara na kurahisisha usafirishaji wa mizigo. Mongella aliyasema hayo Mei 19, 2020 wakati akishuhudia usafirishaji wa shehena ya pili ya minofu ya samaki kiasi cha tani 20 kwenda nchi za Italia na Ubelgiji kwa kutumia ndege ya shirika la ndege la Rwanda kutokea uwanja wa ndege wa Mwanza.
Source : BM TV TANZANIA
 
Hivi tunakwama wapi?
Dreamliner IPO

Airbus IPO

Bombardier zip

Hii inakuwaje? Halafu tunashangilia!

ATCL mnakwama wapi? Tanzania mnakwama wapi?

Ndege yako inavibali vya kwenda nchi zote duniani? Ukijibu ili nitag kama hauna jibu yamaza na kama haujui mambo uliza


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hivi tunakwama wapi?
Dreamliner IPO

Airbus IPO

Bombardier zip

Hii inakuwaje? Halafu tunashangilia!

ATCL mnakwama wapi? Tanzania mnakwama wapi?
Siku dreamliner imebeba samaki mliongeaaaaaaa, hadi midomo ikapinda, zimebeba ndege za rwanda napo mnaongea tu. Hivi kipi chema machoni mwenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunakwama hapo ulipokwama.
Hivi tunakwama wapi?
Dreamliner IPO

Airbus IPO

Bombardier zip

Hii inakuwaje? Halafu tunashangilia!

ATCL mnakwama wapi? Tanzania mnakwama wapi?

Sent using amfifiro
 
Lakini mi nafikili huwezi pewa tenda ya kubeba mzigo wakati usafiri wa kubebea huo mzigo hauna,hivyo lazima tu mwenye nao atakula shavu kwa kua yeye usafiri umepark sehemu unaonekana kuliko wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…