The Supreme Conqueror
JF-Expert Member
- Feb 13, 2017
- 458
- 1,280
- Thread starter
-
- #21
Ahahahah..waliopindua si CCM wenyewe?
..wana-CCM ambao hawajaridhika ndio wanaopaswa kuchukua hatua.
..waige mfano wa Chadema ambao hawakuridhika na mambo fulani ktk chama chao wakaamua kuchukua hatua.
Umenena vyema lakini nina pata mashaka baada ya Mama 2030 hali itakuwaje labda tungoje uchaguzi ndani ya Chama 2027 kwanza.CCM ndio dola ya Tanzania for the last 60 years to date. Hao jamaa wana nguvu 100 times kuwazidi CHADEMA. Wana mizizi yao kwenye vyombo vya usalama. Hivyo suala la CCM kuvunja katiba si sawa na endapo CHADEMA watavunja katiba.
Suala la CCM linapaswa kushughulikiwa kwa level za juu za nchi mkuu..
Those guys have created precedence that others could use in the future to do the same sh!t and use that case as a defence by giving a reference "mbona wao walifanya hivi January 2025"
Nchi hii inaelekea pabaya sana. Ninadhani (please God Forbid) mambo yanaweza kuja kuwa mabaya sana zaidi ya yale ya Kenya mwaka 2007, tena engineers wanaweza wakatokea humo humo CCM..
Nani alimuua Magufuli?Nyaraka ziwekwe wazi hata hapa Tanzania ili tujue:-
1. Nani alimuua Sokoine?
2. Nani alimuua Kolimba?
3. Nani alimuua mzee Kibao?
4. Nani alimuua Membe?
Mkuu mbona Mungu alimtumia Lucifer kujenga Imani zetu kupitia Ayubu?Kinachokera katika Uzi huu ni huko kumtaja Mungu (ambaye wengine tunamsujudia) Kisha kumuhusisha huyo mnafiki na mfitini lissu. Hv kweli M/Mungu anaweza kuwa na jambo lake halafu akalipitishia kwa mhalifu.
Kwani haukuona tangazo rasmi la Makamu?Nani alimuua Magufuli?
Katika hatua iliyoshangaza wengi, Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa agizo maalum la kuwekwa hadharani kwa taarifa za siri zilizofichwa kwa miongo kadhaa.
Kuhusu mauaji ya Rais John F. Kennedy (JFK), mdogo wake Robert F. Kennedy (RFK), na kiongozi mashuhuri wa haki za binadamu, Martin Luther King Jr.
Agizo hili limeibua hisia mchanganyiko kwa Wamarekani na ulimwengu mzima, likifungua ukurasa mpya wa mjadala wa historia ya taifa hilo.
Rais Trump, ambaye anajulikana kwa misimamo yake isiyotabirika na uwazi wa hali ya juu.
Amesema wazi kuwa umma wa Marekani unastahili kujua ukweli wa kilichotokea katika matukio haya ya kihistoria yaliyobadilisha mwelekeo wa taifa.
“Watu wana haki ya kujua. Hakuna sababu ya kuficha taarifa hizi kwa zaidi ya nusu karne,” alisema Trump.
Akisisitiza kuwa kufichuliwa kwa taarifa hizi ni hatua muhimu ya kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao.
Mauaji ya Rais John F. Kennedy
Mnamo Novemba 22, 1963, ulimwengu ulitikiswa pale Rais John F. Kennedy alipouawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya gari lake huko Dallas, Texas.
Tukio hilo lilitokea wakati wa msafara wa rais, na hadi leo, bado linabaki kuwa moja ya matukio yanayoibua maswali mengi yasiyo na majibu ya moja kwa moja.
Ripoti rasmi ya Warren Commission, iliyochapishwa mwaka 1964, ilihitimisha kuwa Lee Harvey Oswald ndiye aliyemuua Kennedy akiwa peke yake.
Hata hivyo, miaka mingi baada ya ripoti hiyo, nadharia nyingi za njama ziliibuka, zikidai kuwa kulikuwa na mkono wa watu wenye nguvu serikalini, CIA, au hata makundi ya kihalifu kama Mafia.
Agizo la Trump linatarajiwa kufichua nyaraka ambazo zinaweza kufuta au kuthibitisha nadharia hizi.
Kifo cha Mdogo wa JFK, Robert F. Kennedy
Robert F. Kennedy (RFK), aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Marekani na baadaye mgombea wa urais, naye aliuawa mnamo Juni 5, 1968.
Muda mfupi baada ya kutoa hotuba ya ushindi katika hoteli ya Ambassador huko Los Angeles, California.
Mauaji yake yalifanywa na Sirhan Sirhan, ambaye alikamatwa na kufungwa jela maisha.
Hata hivyo, nadharia zimeibuka zikidai kuwa Sirhan hakuwa pekee aliyehusika, na kwamba kulikuwa na njama kubwa ya kumzuia RFK kufikia urais kwa sababu ya msimamo wake wa kipekee dhidi ya vita na sera za kibaguzi.
Trump amesisitiza kuwa kuwekwa wazi kwa nyaraka hizi kutasaidia kuelewa kama kweli kulikuwa na njama au ni mkasa wa mtu binafsi.
Martin Luther King Jr, Kifo cha Mwanamapinduzi
Martin Luther King Jr., shujaa wa haki za binadamu na mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani, aliuawa kwa kupigwa risasi mnamo Aprili 4, 1968.
Akiwa kwenye balcony ya hoteli ya Lorraine huko Memphis, Tennessee.
James Earl Ray alikamatwa na kuhukumiwa kwa mauaji hayo, lakini kama ilivyokuwa kwa JFK na RFK, nadharia zinadai kwamba kulikuwa na mkono wa vyombo vya serikali katika kifo cha MLK.
Martin Luther King Jr. alikuwa tishio kwa mfumo wa kibaguzi uliokuwepo wakati huo, kutokana na harakati zake za kupinga ubaguzi wa rangi na vita vya Vietnam.
Trump ameeleza kuwa kufichuliwa kwa nyaraka hizi ni njia ya kuwapa heshima marehemu King na maelfu ya watu walioungana naye katika mapambano dhidi ya ukandamizaji.
Wengi wanasema kuwa Trump amechukua hatua hii si tu kwa ajili ya kuwaheshimu viongozi waliouawa, bali pia kwa sababu ya dhamira yake ya kuonyesha uwazi wa serikali.
Wengine, wanahisi kuwa Trump anatafuta kujijengea umaarufu zaidi kisiasa kwa kuchokoza masuala mazito yanayogusa historia ya taifa.
3.bado tunasubiri uchunguzi wengine taarifa zipo wazi labda kama unajua kitu tujulishe na siye.Nyaraka ziwekwe wazi hata hapa Tanzania ili tujue:-
1. Nani alimuua Sokoine?
2. Nani alimuua Kolimba?
3. Nani alimuua mzee Kibao?
4. Nani alimuua Membe
😄😄😄😄😄Mkuu mbona Mungu alimtumia Lucifer kujenga Imani zetu kupitia Ayubu?
Nadhani ndipo anapoelekea huko huku ni zuga tuNani alikuwa nyuma ya aliyetaka kumuuwa yeye ?? Aweke wazi pia
Mkuu mleta hoja ni kufukua makaburi yaani kujua nani alimua au walishirikiana kumua Kennedy Raisi,Kennedy mwanasheria mkuu,na wanaharakati Martin Luther King.Mh! sidhani kama inaweza kuwa rahisi hivyo!, Huyu mzee toka akoswekoswe ile shaba amewaka sana! aangalie kama wakati ule hawakutia nguvu ktk kumuondosha sasahivi wanaweza wakaongeza!.
Matukio ya Martin na Kennedy bado yananguvu na yakiwekwa hadharani yanaweza kuleta mabadiriko yoyote kisiasa!, sasa sidhani kama wale vipepeo wapo tayari kwa hilo!.
Na nani alimuua Magufuli.Nyaraka ziwekwe wazi hata hapa Tanzania ili tujue:-
1. Nani alimuua Sokoine?
2. Nani alimuua Kolimba?
3. Nani alimuua mzee Kibao?
4. Nani alimuua Membe?
Mwalimu Nyerere Aliwahi kutamka Kwamba "Bila Nchi kupanga na kusimamia uchumi wake yenyewe na kwa Uaminifu basi kungeruhusu mamlaka za serikali kunyakuliwa, kutumikia, kunufaisha na kulinda matakwa ya kikundi kidogo kwa “maangamizi” dhidi ya Mwananchi wa Kawaida....na Vikundi Hivyo ni vya kuogopa Kama Ugonjwa wa Ukoma!Mkuu mleta hoja ni kufukua makaburi yaani kujua nani alimua au walishirikiana kumua Kennedy Raisi,Kennedy mwanasheria mkuu,na wanaharakati Martin Luther King.
Mleta hoja katelemka au kaelezea vizuri kilichotokea USA na nia ya Raisi Trump kuweka report hizo open to the public.
Lakini anochokilinganisha kwa Tanzania hakipo wazi,wala havifanani na USA.Kibaya zaidi uchangiaji mwingine unaonyesha uvamizi wa hoja as offside road comments.
Wakati mwingine achukuwe muda kuchunguza na kulinganisha jambo ili asiitwe kituko.
Kesi ya P.Diddy nadhani hiyo nayo ilitajwa tajwa sana2 Pac kama hayupo kwenye list huu ni ujinga
Hitlafu katika moyo,tatizo alilokuwa nalo kwa miaka kadhaa kabla ya kuwa Rais. Asante..Nani alimuua John Pombe Magufuli?
KLMYAngalia hili nyumbu jingine la lissu, cdf anaingilia ya ccm?!!!!
JWTZ wanapaswa kuingilia kati..Umenena vyema lakini nina pata mashaka baada ya Mama 2030 hali itakuwaje labda tungoje uchaguzi ndani ya Chama 2027 kwanza.
Mwalimu Nyerere Aliwahi kutamka Kwamba "Bila Nchi kupanga na kusimamia uchumi wake yenyewe na kwa Uaminifu basi kungeruhusu mamlaka za serikali kunyakuliwa, kutumikia, kunufaisha na kulinda matakwa ya kikundi kidogo kwa “maangamizi” dhidi ya Mwananchi wa Kawaida....na Vikundi Hivyo ni vya kuogopa Kama Ugonjwa wa Ukoma!
Vyombo vya dola huwa haviingilii mambo ya ndani ya vyama labda itokee uvunjivu wa amani na usalamaJWTZ wanapaswa kuingilia kati..
Katika nchi ya chama kimoja kama Tanzania, katiba ya CCM ni sawa na katiba ya nchi ndio maana Mwenyekiti wa CCM ndiye Rais wa nchi na amiri Jeshi mkuu, na moja kati ya majukumu ya JWTZ ni kuhakikisha katiba inafuatwa, sema hao major generals wa Jeshi ni makada pia ya CCM kwa sababu zamani ilikuwa haiwezekani kujiunga na chombo cha usalama kama hauna kadi ya TANU/CCM..Vyombo vya dola huwa haviingilii mambo ya ndani ya vyama labda itokee uvunjivu wa amani na usalama