Kumbuka hakuna spika alieweza kusimamia bunge la wawakilishi lililokuwa na mvutano mkubwa kama mh.pandu kificho miaka ya 2001Hajakutana na watu wenye hoja nzito za kuiyumbisha ccm... lazima atapata jazba then tutaona uzuri na ubaya wake
Hajakutana na makubwa huyoo
Safi sana!!! umeeleweka sana.Umejibu kipengere kimoja tu. Hujaweka vigezo vyovyote ulivyotumia kuhitimisha maoni yako. Uongozi pia ni contingency ( unategemea mahali, aina ya watu unaowaongoza na wakati) Baraza la wawakilishi na Bunge la Jamhuri wa Tanzania) ni vitu viwili tofauti kwa maana ya watu na changamoto zake. Nikisikiliza mijadala ya Baraza la wawakilishi nikalinganisha na ile ya Bunge la Jamhuri ni kama naota ndoto. Linawafaa wenyewe. Hoja nyepesi mno na ndiyo maana hata mtu mwenye Diploma analiweza. Waliposema wanataka kutunga Katiba yao, hakuna aliyeweza kuona kama wanavunja Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Leo baada kuvunja ndipo wanaona maana ya kuwa na bendera wimbo wao waTaifa kuwa kumbe ilikuwa ni kuvunja Muungano. Kiongozi wa Baraza la wawakilishi ni huyohuyo unayemwita mwenye Hekima. Hekima maana yake ni kutatua migogoro bila ya kuleta athari zaidi kama Mfalme Seleiman wa kwenye Biblia. Alitatua tatizo la wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto bila ya kupoteza uhai wa mtotowala kuumiza yeyote baina ya wanawake hasimu
kweli kabisa...angepata wakina tundu lisu, mnyika, msinga n.k.. kule kuna yaheeee na shekhe, na kuheshmiana sanaaa.
Bado maccm hawajamnyoshea kidole! Subiri utaona!
CCCCM ni Msitu wa Vipaji na Hekima. Chadema waliona ni Haramu kumteua Mh. Pandu Mwenye Diploma ya Sheria na kumuacha Mh. Prof Mahalu eti kwa kuwa ana elimu ya Zaidi, lakin waliona ni halali kumteua Form Six Failure Mbowe Kugombea Urais na Kumuacha Prof. mwesiga Baregu 2005.
hakika katika kutafakari maspika mbalimbali waliowahi kusimamia bunge letu kwa haki busara na *usawa* kati ya s.sitta a.makinda p.msekwa hakika sijawahi iona *hekima ya ajabu* aliyonayo mh.p.kificho,ukizingatia yeye si msomi sana elimu yake ni ya kidato cha 6 na diploma,au ni nani awezaye pinga na asiyeliona hili?
Usomi ni nini?
CC
Mungi@Yericko Nyerere@Ben Saanane