Panga pangua ya mashirika ya umma hebu tuangalie kwa darubini

Panga pangua ya mashirika ya umma hebu tuangalie kwa darubini

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Hii panga pangua ya mama kuhusu mashirika ya umma inatia shaka. Kwanza tujiulize ni mashirika gani ya biashara yanaendeshwa na serikali. Mengi yalikwisha binafsishwa zamani kabisa enzi ya mkapa.
Kwenye hii awamu binafsi naona ni wapiga dili watupu. Mashirika mengi yaliyobakia serikalini yale ya kudhibiti 'regulatory' bodies sasa unayatishia kubinafsisha au kuyaacha yafe kama hayawezi kujitegemee wakati yenyewe yanafanya kazi za kiserikali tu?

Kuna maeneo tuliona hatuwezi kuachia sekta binafsi kwa sababu yanahusika na uhuru wetu au ni muhimu lakini hakuna muwekezaji anataka kubeba hiyo risk. Sasa serikali ikija na lawama kwamba shirika kama TPDC eti litaachiwa life kama haliwezi kujiendesha hiyo ni akili gani. Hapo sikutaka kufifisha harakati za kutafuta mafuta na gesi au kudhibiti uingizaji wa mafuta nchini? Ukiangalia shirika kama TTCL ni shirika muhimu sana kwa umma lakini makampuni binafsi yanataka life ili kusiwe na uwekezaji wa umma kwenye eneo hilo. Tuliona awamu ya tano juhudi ya kuimarisha ttcl na stamico hata kulikomboa shirika la ttcl kwenye ubinafsishaji bandia na kukomboa hisa zake kwenye airtel zilizokua zimeporwa.

Ajabu ni kutishiwa TTCL kutelekezwa ife kama haiwezi eti kujiendesha. Tunajua kila wakati ttcl kwenye ushindani inakuja na vifurushi vya bei ya chini waziri wa sasa Nape amekua akiingilia eti wapandishe kwa kua ushindani wao sio fair kwa kampuni zingine za simu. Huo ni uingiliaji wa ajabu sana kwa waziri. Ukienda huko hazina unakuta msajili wa mashirika na hisa za serikali kwenye mashirika mtu alitemwa na jpm samia kamrudisha. Kwa kweli ni mashaka matupu.

Hili la kufikiri sekta binafsi ndio ya kuachiwa kila kitu ni hatari sana. Sekta binafsi wanaweza kujijali wao tu lakini sio kufanya kazi ya kuendeleza nchi. Kwanza sekta binafsi yetu bado ni kama mawakala tu wa biashara kubwa kimataifa. Serikali isikwepe majukumu yake kwa lengo la ubinafsi wa watendaji wake kama wanavyotaka kufanya kwa bandari.
 
Mkuu, hoja inaweza kuwa nzuri na inayojadilika ILA uandishi umenifanya nishindwe kusoma.

Ni uvivu au ni kutokujua kweli, matumizi punctualities, space, paragraphing n.k?
 
Hii panga pangua ya mama kuhusu mashirika ya umma inatia shaka. Kwanza tujiulize ni mashirika gani ya biashara yanaendeshwa na serikali. Mengi yalikwisha binafsishwa zamani kabisa enzi ya mkapa.
Kwenye hii awamu binafsi naona ni wapiga dili watupu. Mashirika mengi yaliyobakia serikalini yale ya kudhibiti 'regulatory' binafsi wanaweza kujijali wao tu lakini sio kufanya kazi ya kuendeleza nchi. Kwanza sekta binafsi yetu bado ni kama mawakala tu wa biashara kubwa kimataifa. Serikali isikwepe majukumu yake kwa lengo la ubinafsi wa watendaji wake kama wanavyotaka kufanya kwa bandari.
Una hoja sana.
Kuna jambo linatafutwa hapa, Nchi inapigwa kote kote wahuni wameshika hatamu.
Wanataka Mashirika yafanye Manunuzi bila PPRA kuingilia kati.
Wanataka Mashirika yaajiri wenyewe bila Sekretarieti ya ajira kuingilia kati.
Wanataka Mashirika yakope benki bila Hazina na Waziri wa Fedha kuingilia.
Wanataka mashirika wajipangie Mishahara bila UTUMISHI kuingilia kati.
Wanataka Wakuu wa Idara na Vitengo na kupandishana vyeo wafanye wenyewe.
Nk
Nk
Nk
Jamani Nchi yetu imekosa Uongozi thabiti, Wahuni wanaharibu Nchi tushutuke tunaliwa mapemaaaa. Yaaani PSSSF watakuja kukopa Trilioni 300 tuje kustuka majengo yooote yamekuwa ya Makaburu au Mchina. Eee Mungu huu moto unaoichoma Tanzania ni zaidi ya ule wa SODOMA NA GOMOLA tuponyeeee.
 
Hii panga pangua ya mama kuhusu mashirika ya umma inatia shaka. Kwanza tujiulize ni mashirika gani ya biashara yanaendeshwa na serikali. Mengi yalikwisha binafsishwa zamani kabisa enzi ya mkapa.
ama mawakala tu wa biashara kubwa kimataifa. Serikali isikwepe majukumu yake kwa lengo la ubinafsi wa watendaji wake kama wanavyotaka kufanya kwa bandari.
TTCL
 
State regulatory bodies kama wadhibiti watabaki na hao ni muhimu ila mashirika yanayofanya biashara ndo ynaweza kukumbana na rungu kali ..

Hayo ya biashara nje na wadhibiti yaliundwa kwa dhumuni la awali la kufanya biashara ili kupata faida ,hata tufanyaje lazima watu warudi kweny lengo serikali haiwezi kufumbia macho hilo jambo itakuwa inajitafuna .

Ninachotambua mimi ,hayo mashirika yatafanyiwa syndicate haswa yenye mamlaka zinazofanana kwa karibu Mfano PURA na PBPA

Kibaya ninachoona ni ile yatakuwa independent kwa sana yatakuwa yanaendeshwa bila serikali kuyacontrol.
 
Una hoja sana.
Kuna jambo linatafutwa hapa, Nchi inapigwa kote kote wahuni wameshika hatamu.
Wanataka Mashirika yafanye Manunuzi bila PPRA kuingilia kati.
Wanataka Mashirika yaajiri wenyewe bila Sekretarieti ya ajira kuingilia kati.
Wanataka Mashirika yakope benki bila Hazina na Waziri wa Fedha kuingilia.
Wanataka mashirika wajipangie Mishahara bila UTUMISHI kuingilia kati.
Wanataka Wakuu wa Idara na Vitengo na kupandishana vyeo wafanye wenyewe.
Nk
Nk
Nk
Jamani Nchi yetu imekosa Uongozi thabiti, Wahuni wanaharibu Nchi tushutuke tunaliwa mapemaaaa. Yaaani PSSSF watakuja kukopa Trilioni 300 tuje kustuka majengo yooote yamekuwa ya Makaburu au Mchina. Eee Mungu huu moto unaoichoma Tanzania ni zaidi ya ule wa SODOMA NA GOMOLA tuponyeeee.
Kama wataruhusiwa kufanya biashara ikiwa serikali inataka labda gawio kiasi fulani kama performance target ya mashirika hayo lazima watakuwa na ulaji mwingi na uwajibikaji vile vile.

Wao wanajua wafanye nn ili kupata gawio na watatafuna kweli hizo pesa haswa mishahara na posho nene.
 
Umenena vema kabisa. Mengi ya yanayoitwa mashirika ya umma kwa sasa ni taasisi za udhibiti. Kazi hiyo duniani kote inafamywa na serikali.

Kuna mashirika ya kibiashara machache ambayo tangu hapo awali tuliona ni uendawazimu kuyabinafsisha kwazababu ni ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi. Shirika kama TANESCO, TPA, TRC, TAZARA, Vyuo vikuu N.K

Sasa awamu hii kwakweli naanza kuona ni wazi hakuna vision. Tunajaribu chochote kisha tuone kama kitafanikiwa au la. Damage wanayoifanya akina Nape na akina Makamba itachukua miaka mingi kuja kurecover.

Pumzika kwa amani JPM, you had a clear vision, just like Mkapa.
 
Umenena vema kabisa. Mengi ya yanayoitwa mashirika ya umma kwa sasa ni taasisi za udhibiti. Kazi hiyo duniani kote inafamywa na serikali.

Kuna mashirika ya kibiashara machache ambayo tangu hapo awali tuliona ni uendawazimu kuyabinafsisha kwazababu ni ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi. Shirika kama TANESCO, TPA, TRC, TAZARA, Vyuo vikuu N.K

Sasa awamu hii kwakweli naanza kuona ni wazi hakuna vision. Tunajaribu chochote kisha tuone kama kitafanikiwa au la. Damage wanayoifanya akina Nape na akina Makamba itachukua miaka mingi kuja kurecover.

Pumzika kwa amani JPM, you had a clear vision, just like Mkapa.
Hapo tanesco TRC TAZARA kuna kitu hawa wahuni wanatafuta.
 
Sasa serikali ikija na lawama kwamba shirika kama TPDC eti litaachiwa life kama haliwezi kujiendesha hiyo ni akili gani.
Kama ni regulator si yupo PURA ndio anahusika na upstream market ya uchimbaji gesi na mafuta sasa hao TPDC haiwezekani waendeshwe kwa ruzuku wakati Kuna miradi wanafanya na in fact hata bomba la gesi Wana hisa 10% na pia Wana kampuni ya subsidiary inayosambaza gesi na pia kufanya exploration za gesi na mafuta!! Kama hayo Mapato hayawatoshi basi hawana faida Bora ifungwe tu serikali ibaki na PURA kama regulator.

Kwa hili namuunga mkono Mama Samia haiwezekani kampuni hazina tija mfano NIDA kuchapisha tu vitambulisho wameshindwa huku wanalipwa mshahara Kila mwezi Sasa wanafanya kazi gani? Si Bora waambiwe tu watalipwa kutokana na namba ya vitambulisho wanavyotengeneza otherwise ofisi zifungwe na hiyo kazi ifanywe na immigration tu.
 
regulatory' bodies
Usichanganye Regulatory bodies na mashirika yaliyo chini ya serikali mfano Tanzania Commercial Bank inamilikiwa na serikali though sio regulator!! Sasa wasipoleta faida je ya Nini kusubiria dezo ya ruzuku?

Hizi taasisi wakiambiwa wajitegemee mishahara ndio utaona watakavyokua serious!! Ila kwakuwa wanajua pesa inatoka hazina whether wazalishe or not hawana Cha kupoteza..
 
Serikali ina akili kuliko wewe mwwnanchi.
Kama shirika lako likifa na ajira yako inakufa.
Haiwezekani mtu aliyehujumu Unguja ahanishiwe Morogoro.
Hii tuliipigia kelele Rais kasikia
Serikali inatumia billions of money kujiendesha. Mashirika yasiyo na tija yatafutwa na mengine kuunganishwa soon.
 
Sekta binafsi wanaweza kujijali wao tu lakini sio kufanya kazi ya kuendeleza nchi
Mfano TTCL inajali vipi raia wa kawaida wakati hata vocha au network haivuki mijini? Hao customer care wao unaweza piga simu masaa 4 wasipokee? Ila sekta binafsi inatafuta faida so lazima wawajali wateja Ili wawavutie zaidi.

Kingine bei ya vifurushi ipo kisheria kuwa MB 1 itauzwa say 10 Tsh so hata TTCL wangetaka kushusha Bado sheria haiwaruhusu so Wala sio maelekezo ya Nape ila ni sheria ilipitishwa na bunge Ili kuongeza Mapato.

Hata hiyo NIDA angepewa mtu binafsi kuchapisha vitambulisho kwa makubaliano ya kulipwa based on the number of copies anachapisha, niamini Kila mTanzania angekua na NIDA Tayari.
 
Mengi ya yanayoitwa mashirika ya umma kwa sasa ni taasisi za udhibiti. Kazi hiyo duniani kote inafamywa na serikali.
Msichanganye, mfano Baraza la uwezeshaji kiuchumi ni regulator? TBC? TCB? TTCL? yapo mashirika mengine hata kazi zao hazieleweki yana over lap!! So ni Bora tu yafutwe au yajiendeshe yenyewe period.
 
Kama ni regulator si yupo PURA ndio anahusika na upstream market ya uchimbaji gesi na mafuta sasa hao TPDC haiwezekani waendeshwe kwa ruzuku wakati Kuna miradi wanafanya na in fact hata bomba la gesi Wana hisa 10% na pia Wana kampuni ya subsidiary inayosambaza gesi na pia kufanya exploration za gesi na mafuta!! Kama hayo Mapato hayawatoshi basi hawana faida Bora ifungwe tu serikali ibaki na PURA kama regulator.

Kwa hili namuunga mkono Mama Samia haiwezekani kampuni hazina tija mfano NIDA kuchapisha tu vitambulisho wameshindwa huku wanalipwa mshahara Kila mwezi Sasa wanafanya kazi gani? Si Bora waambiwe tu watalipwa kutokana na namba ya vitambulisho wanavyotengeneza otherwise ofisi zifungwe na hiyo kazi ifanywe na immigration tu.
TPDC walikuwa wanawadai TANESCO zaidi ya trillion za kuwauzia gas; huyo Samia ndio kalifuta hilo deni lao.

Yaani serikali isababishe hasara kwa kampuni moja halafu waruhusu wengine kujitapata faida tena ya uongo.

TANESCO inatumia billioni 250 kununua umeme wa makampuni binafsi na inalipa on time hayo madeni na bado inaalika wawekezaji wa kununua kwao hata pale bwawa la Nyerere litakapoisha. Huko ni kujiongezea expenditure.

Halafu aina hela ya kuilipa TPDC japo billion 100 kwa mwaka wakati wanatumia gas yao kuzalishia umeme na kuuza.

It’s just pathetic una encourage taasisi za elimu kujitegemea wakati wanatoa merit good; kuwaacha hao wajiendeshe kwa nchi maskini na vyuo vyenyewe uchwara bila ya subsidisation sioni hivyo vyuo vikivutia quality lecturer wala kuwa na mazingira mazuri ya elimu considering wanafunzi wa vyuo hivyo wengi ni familia za kawaida.

Hiko ni kutupa hela zaidi kuwagharamia wanafunzi watakaopata mikopo wakati kiwango cha elimu yenyewe kitakuwa below.

Hakuna lolote la maana wanalofanya zaidi ya kumjaza huyo mama upepo tu na cinema zao.
 
Serikali kuendesha mashirika ni uzwazwa uliopitwa na wakati
Inatakiwa imiliki infrastructure halafu iuze huduma zake kwa mashirika binafsi yashindane kutoa huduma!
Mfano
Tanesco ivunjwe na kuwa National Energy ambayoinazalisha umeme wa Hydro, Fossil fuels au Solar na kuuza unit kwa makampuni binafsi yatakayoshindana kutafuta wateja kwa kuuza umeme kwa gharama nafuu.
TRC ivunjwe na kuitwa National Rail, iwe inamiliki njia na vituo vya treni, halafu inatoza makampuni binafsi kupewa contract za kuleta treni na kuendesha huduma za usafirishaji wa treni.
TTCL pia ivunjwe na kuitwa National Telecom - imiliki infrastructure zote za mawasiliano na kuuza huduma za simu, na mtandao kwa makampuni binafsi tatakayoshindana kupata wateja kwa gharama nafuu
The list goes on and on.....

Na hii inaipa serikali uwezo kusimamia gharama anatozwa mwananchi na makampuni binafsi kwa kuwa na uwezo wa kupunguza gharama zake na kuweza kuwatolea macho makampuni yatakayo kuwa na gharama kubwa wakati wanauziwa huduma na serikali kwa ghrama ndogo, huu ndio mfumo wa nchi zilizoendelea.

Ni ujinga mwingi kwa serikali kung'ang'aniakufanya biashara na wananchi.
 
Halafu aina hela ya kuilipa TPDC japo billion 100 kwa mwaka wakati wanatumia gas yao kuzalishia umeme na kuuza.
Gesi sio ya TPDC, they only own 10%. Then huwezi taka Tanesco ilipe hayo matrilion wakati serikali ya Bara na Zanzibar zinadaiwa mabilioni ya bili za umeme and goes on and on so akisamehe deni ni sababu na wao Tanesco wamesamehe deni etc. So hizo intergovernmental transactions zinaji off set zenyewe sababu ni mwili mmoja tu.
Hakuna lolote la maana wanalofanya zaidi ya kumjaza huyo mama upepo tu na cinema zao.
Naona umekazania TPDC, hivi taasisi kama hizi zinafanya kazi almost Moja, why then ziendelee kula ruzuku na mishahara ya bure bila kuwa na tija? Why zisiunganishwe ziwe mbili kama sio Moja?

1. National Development Corporation
2. National Economic Empowerment Council
3. Tanzania National Business Council
4. Tanzania Trade Development Authority.

Mbona Vodacom au Tigo zinaingiza faida why not TTCL? ni sababu ya ruzuku so wanajua liwe liwalo mishahara ipo tu!! Mbaya zaidi TTCL wanauzia mpaka internet hayo makampuni binafsi, yanawakodishia minara na pia mkonge wa Taifa upo chini ya TTCL ila Cha ajabu haingizi faida whilst anaowauzia ndio wanaingiza faida!!

Taasisi za Elimu, afya na regulators pekee ndio zipewe mishahara ya hazina, wengine wote wabuni miradi wajiendeshe kama private sector.

Wakati wa mabadiliko ni Sasa, ikiwezekana na NIDA nayo ivunjwe na majukumu yake yapelekwe chini ya SUMA JKT utaona tofauti!!
 
Gesi sio ya TPDC, they only own 10%. Then huwezi taka Tanesco ilipe hayo matrilion wakati serikali ya Bara na Zanzibar zinadaiwa mabilioni ya bili za umeme and goes on and on so akisamehe deni ni sababu na wao Tanesco wamesamehe deni etc. So hizo intergovernmental transactions zinaji off set zenyewe sababu ni mwili mmoja tu.

Naona umekazania TPDC, hivi taasisi kama hizi zinafanya kazi almost Moja, why then ziendelee kula ruzuku na mishahara ya bure bila kuwa na tija? Why zisiunganishwe ziwe mbili kama sio Moja?

1. National Development Corporation
2. National Economic Empowerment Council
3. Tanzania National Business Council
4. Tanzania Trade Development Authority.

Mbona Vodacom au Tigo zinaingiza faida why not TTCL? ni sababu ya ruzuku so wanajua liwe liwalo mishahara ipo tu!! Mbaya zaidi TTCL wanauzia mpaka internet hayo makampuni binafsi, yanawakodishia minara na pia mkonge wa Taifa upo chini ya TTCL ila Cha ajabu haingizi faida whilst anaowauzia ndio wanaingiza faida!!

Taasisi za Elimu, afya na regulators pekee ndio zipewe mishahara ya hazina, wengine wote wabuni miradi wajiendeshe kama private sector.

Wakati wa mabadiliko ni Sasa, ikiwezekana na NIDA nayo ivunjwe na majukumu yake yapelekwe chini ya SUMA JKT utaona tofauti!!
397713C7-9090-4D49-BDB0-CF0A931899C8.jpeg


Vipi mwaka ulioisha TANESCO imepata revenue kutoka visiwani takribani billioni 107 ina hela ya kulipa ‘cost of sales’ ya manunuzi ya umeme kwa watu kama Dowans zaidi ya 207 billion ila aina hela ya kutambua gas usage na kulipa TPDC na yenyewe ipate income na working capital za kuanzisha ata biashara ya vituo vya mafuta na storage.

TPDC inaweza kuwepo na PURA wana shughuli tofauti TPDC ina deal na mid stream and downstream, only that it is poorly funded na inahujumiwa.

6B40711D-3DEE-440B-A688-7EE9FC253C69.jpeg


Moreover mwenye hisa Songas ni TPDC na hapati mapato yoyote ya mauzo ya gas, ila TANESCO asie na hisa ndio inapokea gas sales income za tsh 30.2 how is TPDC going to survive kama waziri anaweza hamisha mapato ya mashirika hili ku-boost hesabu za shirika analotaka yeye.

Huko mid stream TPDC ina shughuli gani kama hakuna biashara yoyote inafanya.

Kwanza TANESCO imepata vipi hayo mapato ya Gas income; ni hivi hiyo statement yao ni very dodgy hawa wametengeneza faida ndogo sana hata hiyo kodi wamelipa si zaidi ya tsh 2 billioni baadae watakwambia hiyo tsh 97 billion ya tax liability ni deferred tax na kufutwa juu kwa juu tu ni watu tu wanaomchezea sinema huyo mama. Not to discredit any effort za management to modernise shirika lakini hamna kitu pale tangible kibiashara ya faida ni story tu.

Hayo mashirika mengine ya kibiashara ya au taasisi zao zinazo pwayapwaya shida ni uwezo wa management. Mfano TTCL last I checked sehemu kubwa ya mapato yao inapotea kwenye administration expense za salary and wages. Wanawaajiri mara tatu ya private sector yet wana revenue ndogo kushinda washindani wao.

Sasa if you gonna have a large expense bill kushinda wapinzani wako halafu wewe ndio mwenye mapato kidogo, bado ufisadi hiyo faida utaitoa wapi. Lini umesikia TTCL inafikiria kufanya rationalisation ndio kwanza hawana habari. Tells you weledi wa kushindana kibiashara kwenye soko sio priority yao no wonder it has the least number subscribers on the market.

Same ukienda NIDA kila siku humu JF tu watu wanalalamikia bureaucracy ya kupata vitambulisho so wateja wapo wakupata hizo hela; management is not interested. Hayo mambo hayahitaji makongamano sijui retreat ni simple highlight matatizo ya shirika toa onyo fire; mengi yanaendeshwa na incompetent people so are the technocrat huko mawizarani including msajili wa hazina.
 
Mbona Vodacom au Tigo zinaingiza faida why not TTCL?
Hawana ubunifu wao walitangulia kuwepo kwenye soko hata kabla ya hao Voda, tigo na wengine

Tatizo kubwa la mashirika yetu upigaji na yanaendeshwa kimazoea

Wakajifunze China jinsi SOEs (mashirika ya umma) yanapiga kaz na kukuza uchumi wa nchi. Hawacheki na Mkurugenzi au bodi ya wakurugenzi wazembe au wala rushwa ni ngome maisha au hukumu ya kifo
 
Hawana ubunifu wao walitangulia kuwepo kwenye soko hata kabla ya hao Voda, tigo na wengine

Tatizo kubwa la mashirika yetu upigaji na yanaendeshwa kimazoea

Wakajifunze China jinsi SOEs (mashirika ya umma) yanapiga kaz na kukuza uchumi wa nchi. Hawacheki na Mkurugenzi au bodi ya wakurugenzi wazembe au wala rushwa ni ngome maisha au hukumu ya kifo
Tatizo la mashirika ya serikali ni kuwa wafanyakazi wa hayo mashirika ni wafanyakazi wa serikali...

Yatakiwa mashirika yajiendeshe kwa pesa yao, yakipata hasara yapunguze wafanyakazi
 
Back
Top Bottom