Papa Francis alaani kuchomwa kwa Quran

Papa Francis alaani kuchomwa kwa Quran

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
POPE-AMERICA-MAGAZINE-1752271-scaled.jpg


Kiongozi wa Kanisa Katoliki Dunaini, Papa Francis, amelaani kwa matamshi makali vitendo vya kuchomwa kitabu kitakatifu kwa Waislamu, Qur'an.

Papa Francis pia ametoa wito wa kuheshimiwa kwa vitabu vitakatifu vya dini kama njla ya kuonesha heshima kwa Watu wanaoviamini, katika mahojiano na gazeti la Al-Ittihad linalochapishwa huko Falme za Kiarabu, Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki amesema amechukizwa na matendo hayo na kupinga juhudi zozote za kuruhusu matukio hayo kuwa sehemu ya uhuru wa maoni.

Kauli ya Papa Francis inakuja kufuatia kitendo cha wiki iliyopita ambapo Mtu mmoja alichoma Quran Tukufu kwenye Miji mkuu wa Sweden, Stockholm, na kuibua hasira kutoka Mataifa kadhaa duniani.

Ingawa Mamlaka za Sweden zimekuwa zikikataa maombi ya maandamano ya kuipinga Quran, Mahakama za nchi hiyo zimepinga katazo hilo zikisema zinaingilia uhuru wa Watu kujieleza.

Chanzo: Millard Ayo
 
Waislamu walikuwa wanaaingizwa mtegoni ili ajenda itimie hongereni kwa kuwa watulivu kutoshindana na wajinga.
 
Mnyaazi huwa wanaweweseka kama vitabu vyao vikichomwa.

Aya na wal wanao futa app zao za Quran kwenye simu na wao inakuwaje?
 
Waislamu msipende kuingia mitego ya watu wajinga.
Kichaa kakimbia na nguo zako ukimkimbiza uçhi mtaonekana vichaa wawili wanakimbia,chutama tafuta nguo zingine
 
Papa yeye ndio kasikia uchungu hahahahaha...
 
Papa Ajue kuwa katika uislam kila siku ya swala kulaani wasio Muslim lazima ni sehemu ya ibada so asije akadhani Kuwa na rafiki na uislam unamuweka salama ajue siku akiwa weak atalaruliwa kama fisi analia vile.

Mtume wao aliwaambie non muslim ukiona anakuzidi nguvu omba amani ila ukipata nguvu pigana nae.

Vita vya Muslim na Roman uislam ulishindwa wakaomba amani, Egypt na Israel vita ilipigwa Egypt akawa hoi akaomba Amani ila tunavyoelekea Egypt akipata nguvu zaidi vita itarejewa upya.

So Papa ajue hilo mzee njia mbili mbili anapuliza kupunguza nguvu za moto hapo hapo anachochea
 
We ulitaka afurahie ili uanze kumsingizia habari za upinde,kachezA na akili zenu wanafiki.
Koran haiukushuswa hicho ni kitabu Wasomi wa Kiislam wanasema Koran ipo Moyoni kama kuharibiwa zishafukiwa kwenye matetemeko kibao na mafuriko na kuteketea kwa moto lakini koran zinachapishwa kila siku na wapiga pesa kwa njia za dini... so mtu anayelaani ujinga huu ni mjinga pia na kama sio mjinga alaani kila koran inapoteketea acheni kutupigia kelele...
 
Koran haiukushuswa hicho ni kitabu Wasomi wa Kiislam wanasema Koran ipo Moyoni kama kuharibiwa zishafukiwa kwenye matetemeko kibao na mafuriko na kuteketea kwa moto lakini koran zinachapishwa kila siku na wapiga pesa kwa njia za dini...

Dini ni imani tu wala hazina mashiko wajanja wanazitumia kunufaika.
 
Papa Ajue kuwa katika uislam kila siku ya swala kulaani wasio Muslim lazima ni sehemu ya ibada so asije akadhani Kuwa na rafiki na uislam unamuweka salama ajue siku akiwa weak atalaruliwa kama fisi analia vile... Mtume wao aliwaambie non muslim ukiona anakuzidi nguvu omba amani ila ukipata nguvu pigana nae...
Vita vya Muslim na Roman uislam ulishindwa wakaomba amani, Egypt na Israel vita ilipigwa Egypt akawa hoi akaomba Amani ila tunavyoelekea Egypt akipata nguvu zaidi vita itarejewa upya.. So Papa ajue hilo mzee njia mbili mbili anapuliza kupunguza nguvu za moto hapo hapo anachochea
Nikukumbushe TU, Israel si Taifa la kiikristo.

Screenshot_20230515-172320.jpg
 
Quran si ni yake kanunua kwa pesa zake sasa nini tena.
 
Papa Francis alaani uchomaji moto wa Qurani.jpeg

Papa Mtakatifu amekirihishwa na tabia ya kuchoma kitabu kitakatifu cha waislamu : Picha :AP

Papa Francis alisema kuchomwa kwa kitabu kitakatifu cha Waislamu, Quran, kumemkasirisha na kwamba alilaani kuruhusu kitendo hicho kama aina ya uhuru wa kujieleza.
"Kitabu chochote kinachochukuliwa kuwa kitakatifu kinapaswa kuheshimiwa kuheshimu wale wanaokiamini," Papa alisema katika mahojiano katika gazeti la Umoja wa Falme za Kiarabu la Al Ittihad, lililochapishwa Jumatatu.
"Ninahisi kukasirishwa na kuchukizwa na vitendo hivi. Uhuru wa kujieleza kamwe usitumike kama njia ya kuwadharau wengine na kuruhusu jambo hilo kukataliwa na kulaaniwa."
Mwanaume mmoja aliichana na kuichoma moto Quran katika mji mkuu wa Uswidi Stockholm wiki iliyopita, na kusababisha kulaaniwa vikali na mataifa kadhaa, ikiwemo Uturuki ambayo uungaji mkono wake Uswidi unahitaji kuingia katika muungano wa kijeshi wa NATO.
Wakati polisi wa Uswidi wamekataa maombi kadhaa ya hivi karibuni ya maandamano dhidi ya Qur'ani, mahakama zimepinga maamuzi hayo, ikisema kuwa yanakiuka uhuru wa kujieleza.
Siku ya Jumapili, kundi la Kiislamu la mataifa 57 lilisema hatua za pamoja zinahitajika ili kuzuia vitendo vya kudhalilisha Quran na sheria za kimataifa zitumike kukomesha chuki za kidini. chanzo.https://www.trtafrika.com/sw/world/papa-francis-alaani-uchomaji-moto-wa-qurani-13877160
 
Back
Top Bottom