Papa Francis amuunga mkono Mpinga Kristo

Papa Francis amuunga mkono Mpinga Kristo

Nimekuuliza aliyasema lini...? Wapi..? Alimwambia nani..?
Mbona kwenye catholic credibke sources hamna..?

Halafu nijibu maswali nilyokuuliza hapo juu chap..! Tusipotezeane muda
Soma link hii, "Pope
Nimekuuliza aliyasema lini...? Wapi..? Alimwambia nani..?
Mbona kwenye catholic credibke sources hamna..?

Halafu nijibu maswali nilyokuuliza hapo juu chap..! Tusipotezeane muda
Nimetoa link. Nairudia, ukienda huko utapata majibu ya maswali yako. Pope Francis goes public in support of RFID implantstion. " Ukisoma utapata majibu ya maswali yako yote. Kumbuka hata hivyo kwamba mimi nimeleta tu taarifa ambayo tayari iko kwenye mtandao na he has been quoted as saying.
 
Mleta mada ni Msabato. Wao ndiyo hujifanya kuwa wanafahamu mambo ya unabii sana na ni wafafanuzi wakubwa wa vitabu vya Ufunuo na Daniel. Kanisa zima lilianzishwa kutokana na vuguvugu la kutabiri kurejea kwa Yesu kule Marekani. Baada ya utabiri huo kushindikana na Yesu kutorejea hasa mwaka 1844, walikokotoa mahesabu ya kitabu cha Daniel upya wakatabiri tena wakashindwa. Tangu hapo Kanisa hili halijaachana na mambo ya unabii, kutabiri tabiri na conspiracy theories. Kila tukio jipya liwe natural au la hupitishwa katika chekecho la unabii; na unabii wa vitabu vya Daniel na Ufunuo ndiyo central theme.

Papa ni mtu wa muhimu sana kwa Waadventista Wasabato. Wanaamini kuwa Pope ndiye mpinga Kristo na mmiliki wa ile namba tata 666 na kwamba siku za mwisho kanisa katoliki litarudia hadhi yake liliyokuwa nayo hapo zamani wakati ule likitawala dunia na kuwapitishia hukumu za kifo akina Galileo Galilei. Wanaamini kuwa wao pekee ndiyo washika amri sahihi za Mungu na ndiyo pekee watakaokwenda mbinguni. Na wale wahafidhina hawali nyama, kunywa kahawa au chai, samaki wasio na magamba, wanyama wasio na kwato na sheria nyingine za Kumbukumbu la Torati hasa zinazohusu siku ya Sabato. Siku ya Sabato hawaruhusiwi hata kupika! Kwa hiyo wokovu unafungamanishwa na sheria hizi za Musa jambo ambalo linapingwa na Wakristo wengi (Damu ya Yesu ndiyo ilimaliza kila kitu msalabani na mtu hataikosa mbingu eti tu kwa vila alikula samaki asiye na magamba!)

Wanatheolojia wengi na wachambuzi wa Biblia huwachukulia Wasabato kama aina mojawapo ya cult za Kikristo zilizofanikiwa sana. Badala ya kuamini Biblia pekee, wanaamini pia maandishi mengi (karibia vitabu 600) vya mama mmoja Mmarekani aitwaye Ellen G. White. Huyu wanamtambua kama nabii wao na baadhi ya vitabu vyake kama Pambano Kuu (The Great Controversy) vina hadhi kubwa sana kanisani. Pia wanaamini kuwa Yesu hakumaliza kazi ya kutukomboa msalabani bali kuanzia mwaka 1884 aliingia Patakatifu pa Patakatifu (Holly of Hollies) huko mbinguni ili kuendelea kututetea mbele ya Mungu Baba kuhusu dhambi zetu tunazoendelea kuzitenda hapa duniani.

Ova!
 
Mleta mada ni Msabato. Wao ndiyo hujifanya kuwa wanafahamu mambo ya unabii sana na ni wafafanuzi wakubwa wa vitabu vya Ufunuo na Daniel. Kanisa zima lilianzishwa kutokana na vuguvugu la kutabiri kurejea kwa Yesu kule Marekani. Baada ya utabiri huo kushindikana na Yesu kutorejea hasa mwaka 1844, walikokotoa mahesabu ya kitabu cha Daniel upya wakatabiri tena wakashindwa. Tangu hapo Kanisa hili halijaachana na mambo ya unabii na kutabiri tabiri. Unabii wa vitabu vya Daniel na Ufunuo ndiyo central theme.

Wasabato wanaamini kuwa Pope ndiye mpinga Kristo na mmiliki wa ile namba tata 666. Wanaamini kuwa wao pekee ndiyo washika amri sahihi za Mungu na ndiyo pekee watakaokwenda mbinguni. Na wale wahafidhina hawali nyama, kunywa kahawa au chai, samaki wasio na magamba, wanyama wasio na kwato na sheria nyingine za Kumbukumbu la Torati hasa zinazohusu siku ya Sabato. Kwa hivyo wokovu unafungamanishwa na sheria hizi za Musa jambo ambalo linapingwa na Wakristo wengi (Damu ya Yesu ndiyo ilimaliza kila kitu msalabani na mtu hataikosa mbingu eti tu kwa vila alikula samaki asiye na magamba!)

Wanatheolojia wengi na wachambuzi wa Biblia huwachukulia Wasabato kama aina mojawapo ya cult za Kikristo zilizofanikiwa sana. Badala ya kuamini Biblia pekee, wanaamini pia maandishi mengi (karibia vitabu 600) vya mama mmoja Mmarekani aitwaye Ellen G. White. Huyu wanamtambua kama nabii wao na baadhi ya vitabu vyake kama Pambano Kuu (The Great Controversy) vina hadhi kubwa sana kanisani. Pia wanaamini kuwa Yesu hakumaliza kazi ya kutukomboa msalabani bali kuanzia mwaka 1884 aliingia Patakatifu pa Patakatifu (Holly of Hollies) huko mbinguni ili kuendelea kututetea mbele ya Mungu Baba kuhusu dhambi zetu tunazoendelea kuzitenda.

Ova!
Sasa huu si ukichaa??

Chemtrail
 
Soma link hii, "Pope
Nimetoa link. Nairudia, ukienda huko utapata majibu ya maswali yako. Pope Francis goes public in support of RFID implantstion. " Ukisoma utapata majibu ya maswali yako yote. Kumbuka hata hivyo kwamba mimi nimeleta tu taarifa ambayo tayari iko kwenye mtandao na he has been quoted as saying.
Wewe hiyo link umehakikisha ni credible mpka uilete hapa..? Sisi kukupinga sio kwamba hatutaki kusoma uzi wako ila tumegundua ulichokileta ni uzushi wa mitandanaoni...

Sasa maana wewe mpaka utuletee hapa inamaanisha umesoma, umeelewa ndio maana ukawrza kuandika kwa kingereza na kuleta hapa..

Sasa kama hayo yote uliyaweza kwanini ushindwe kinijibu maswali niliyokuuliza..? Au na wewe ni mbumbumbu unayebebwa na porojo za mitandaoni...?
 
a287cdca7ecd8e65121a56970b04ef61.jpg


Nimekumbuka movie moja ya The Physicist. Dr alikataliwa kumfanyia mtu operation miaka ya Middle Ages kwa sababu viongozi wa kanisa waliamini ni kinyume na Mungu kumpasua mtu.

I mean; sometimes imani zinaweza kutufanya kuwa wajinga na kukataa kubadilika.

Pia kama ina faida na manufaa kwanini tuzuie kwa kuona ni mwisho wa dunia na ushetani? Kwanza sio kila mtu ni mkristu na sio kila mtu ana dini hiyo inayotazama mwisho wa dunia kihivyo. So haiwezekani kukataa jambo mtazamo wa dini moja ambayo haina facts bali ni conspiracies tu.

Hizi conspiracy zinachanganya watu na kujaza watu ujinga wa kufikiri. Kila kitu mnaona 666.
 
Zamani mlikuwa mnasema waislam ndio wapinga kristo. Siku hizi naona mmeanza kutafutana mchawi kati yenu wenyewe. Na bado, ngoma bado mbichi hii. Hadi kiyama kifike tutashuhudia mengi hasa watakaokuwepo. Hata ATM machine zonavoingia walisema ni alama ya mnyama hata ATM kadi wakasema alama ya mnyama. Duuu alama za mnyama ni nyingi. Wasabato wao huwa wanasema jina la papa kwa kirumi ni alama ya mnyama!!!

Nawaambia tena nawaambia; acheni kuhangaika na alama za mnyama bali haingaikieni kuwa wachamungu wa kweli. Nawaambia, hakika ni uchamungu pekee ndio utawaokoa na makucha ya huyo mnyama.
 
Ni upuuzi kuukimbia ukweli. Face it and make the appropriate decision.Mbona nimetoa link. Go to that one link na utashangaa how your eyes will be opened. But be courageous because the foundation of your faith will be shaken.
Tunataka video clip inayomuonesha papa akisema hayo unayosema, hatutaki ujinga sisi. Hata simu za mkononi zinavoingia kuna watu walisema ni alama ya mnyama!!!
 
Unacho ongea hakina mantiki kwa kuwa mimi sio shoga na wala sitakuwa shaken. Halafu unashangaza, mbona I have just reported what he said, why the fuss. He felt kwamba it is the right time for us to know. Nilichofanya ni kukuletea ujumbe alio ongea na waumini wengine Vatican ambao na wewe una haki ya kuujua. Kama yeye hakuona kwamba ni siri, kwa nini wewe uuone siri. Ni ajabu sana.
Lete ushahidi kuwa microchip ni alama ya mnyama ikiwa unasema kweli. Tuletee ushahidi mtu aliewekewa microchip kisha ikamtoa majipu mwili mzima. Hatupendi ujinga sisi.
 
Mkuu kumbe umepakua kutoka google? umeona sasa ulivyo ingizwa chaka? Google ni universal yaani hata Pumba watu zito kule hivyo source ya information inatakiwa iwe official link. sio uchafu wawa huni tu huko google!!
Asichokijua ni kuwa hata mm naweza andika pumba zangu na ukigoogle unazipata.
 
Hakuna sababu ya kuhamaki. Kwanza ungekuwa na busara ungenishukuru. Mimi sipati faida yeyote kuleta taarifa hii, I am just helping you to make an imformed decision. Hata hivyo kama unataka kupata taarifa kamili
Google"Pope Francis goes public in support of the RFID implantation. " Kwanza taarifa hii is just a tip in the iceberg, mambo makubwa zaidi na ya kushangaza yatatokea katika kanisa la Katoliki katika siku za hivi karibuni!


Mkuu kuwa mvumilivu, watu tuko tofauti sana. Mwingine hajui kitu chochote ktk thread lkn lazima a-comment tena kwa ukali na kashfa badala ya kupita kimyakimya.

Vv
 
Katika hali ya kushangaza, Papa Francis amejitokeza hadharani kuunga mkono matumizi ya vichipu vya RFID, yaani Radio Frequency Identification kwa wanadamu. Amesema tekinolojia hii inaleta matumaini makubwa katika kutatua matatizo mengi ya wanadamu na hivyo kuboresha ustawi wao.

Matamshi haya yanakuja huku akijua msimamo wa kiimani wa makanisa mengi ya Kikristo na hata kanisa Katoliki lenyewe. Makanisa mengi ya kikristo yanaamini kwamba RFID chipping ni alama ya mnyama au Shetani kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Ufunuo. Tukio hili kufuatana na imani ya makanisa haya, linaashiria mwisho wa dunia.

Katika kitabu cha Ufunuo13 msitari wa 16-18 tunasoma maneno haya, 16Naye alimlazimisha kila mtu, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, huru na mtumwa, kupokea chapa katika mkono wake wa kulia au paji la uso, 17 ili kila mtu asiweze kununua au kuuza mpaka awe na hiyo chapa, ambalo ndilo jina la huyo mnyama au namba ya jina lake. 18 Hii inahitaji hekima, kama mtu ana ufahamu aitafute namba ya huyo mnyama, kwa sababu ni namba ya kibinadamu. Namba yake ni 666.

Kwa wale wachunguzi watakubaliana na mimi kwamba namba hii inatumika sana siku hizi.Wapo ambao wanaitumia kwa uwazi kwenye bidhaa. Wanamuziki wa Rock hasa nchi za Ulaya na Marekani nao wanaitumia sana, lakini wengi wanatumia kwa siri, kwa hiyo inahitaji umakini mkubwa kuweza kujua kwamba ni 666. Hata logo ya Olympic ina namba 666. Matumizi ya namba hii kwenye barcodes ni wazi kidogo!

Katika hotuba yake ya kila wiki Vatican, Papa alizungumzia juu ya imani aliyonayo kwenye tekinolojia ya RFID. Aliwahakikishia waumini wake kwamba hakuna athari zozote za kiroho au kiafya zinazoweza kutokana na matumizi ya vichipu vya RFID. Hata hivyo inafahamika kwamba yapo matatizo makubwa ya kiafya yanayoweza kutokana na matumizi ya vichipu vya RFID vinapochoka, ikiwa ni pamoja na maumivu makali mwilini na majipu mwili mzima.

Aliendelea kwa kusema wamechunguza maandiko vizuri na hivyo wanaweza kusema kwamba hakuna ushahidi wowote unao-onyesha kwamba vichipu vya RFID ambacho kinawekwa mwilini kina muwakilisha Shetani. Nadhani alisahau Ufunuo 13:16-18! Aliongeza kusema RFID ni baraka kutoka kwa Mungu mwenyewe ambayo ameileta kwa wanadamu.

Aliwaomba wauminu wa Kanisa Katoliki waipokee baraka hii kwa moyo mmoja. Alimalizia kwa kusema kuanzia sasa itakuwa lazima kwa kila mfanyikazi wa Vatican kuwekewa kichipu cha RFID.

Kusoma zaidi:Google "Pope Francis goes public in support of RFID implantation. "
Hatushangai huyo Papa ni mpinga kristo so kukubali hizo chip ni kawaida tu akubali ili maandiko yatimie
 
Back
Top Bottom