Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 577
- 2,595
Katibu Mkuu wa Vatican, Kadinali Pietro Parolin, kwa niaba ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis ametuma salamu za rambirambi kwa watu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia ajali mbaya ya ndege ya Precision Air iliyosababisha watu 19 wapoteze uhai.
Papa Francis ametoa hakikisho la kuwa karibu kiroho kupitia sala kwa watu wote waliokumbwa na mkasa huu hasa kwa familia na wahanga wote.
Anaziombea roho za marehemu zipate pumziko la milele, majeruhi wapone haraka na anawaombea wajazwe nguvu wote wanaohusika kwenye uokozi na matibabu ya majeruhi.
Zaidi ya yote, Papa anaomba faraja na amani ya Mwenyezi Mungu itawale kwa ndugu jamaa na marafiki wote waliokumbwa msiba huo mkubwa.
Papa Francis ametoa hakikisho la kuwa karibu kiroho kupitia sala kwa watu wote waliokumbwa na mkasa huu hasa kwa familia na wahanga wote.
Anaziombea roho za marehemu zipate pumziko la milele, majeruhi wapone haraka na anawaombea wajazwe nguvu wote wanaohusika kwenye uokozi na matibabu ya majeruhi.
Zaidi ya yote, Papa anaomba faraja na amani ya Mwenyezi Mungu itawale kwa ndugu jamaa na marafiki wote waliokumbwa msiba huo mkubwa.