PAPA Fransis Amteua Mtawa Mwanamke wa Kwanza Kwenye Jopo La Uongozi wa Vatican,Wahafidhina wa Dini Wabaki Midomo Wazi

PAPA Fransis Amteua Mtawa Mwanamke wa Kwanza Kwenye Jopo La Uongozi wa Vatican,Wahafidhina wa Dini Wabaki Midomo Wazi

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
My Take
Papa Fransis ameivunja mwiko wa kuwabagua wanawake kwenye masuala ya Uongozi wa kidini huko Vatican Kwa kumteua Mtawa wa kwanza mwanamke kwenye Jopo la Uongozi.

VATICAN : KIONGOZI mkuu wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amemchagua Simona Brambilla kuwa miongoni mwa viongozi wakuu katika moja ya ofisi kuu kwenye makao makuu ya kanisa hilo mjini Vatican.

Uteuzi huo unamfanya Simona kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo wa kihistoria na kuashiria hatua kubwa ya Papa Francis ya kuwapa wanawake nafasi za uongozi na kuongoza majukumu muhimu ya kanisa hilo, nafasi ambayo haijawahi kutokea huko nyuma.

Uteuzi huo wa kihistoria wa Brambilla umethibitishwa na vyombo vya habari huko Vatican, ambavyo viliandika kichwa cha habari vikisema "Mtawa Simona Brambilla ndiye kiongozi wa kwanza mwanamke hapa Vatican".

Papa Fransis alimchagua Simona siku ya Jumatatu na kutangazwa na vyombo vya habari leo alhamisi tarehe 9 Januari 2025.

Chanzo: Dw
 
Haa ha ha; Aliko Dangote mbona hapigi gambe na hana mke? Hi imekaaje? MO wa hapa bongo nae, hanywi pombe na ana kademu kamoja tu, nae vipi? Salim Said Bakhresa? Nauliza tu kuchangamsha uzi
Kuna watu kwel pombe hawagusi nakubaliana na ww.

Kwenye mademu tatofautiana na wewe kidogo, kama hupo kwenye circle yao ya karibu ni ngumu kujua
 
Back
Top Bottom