Soloma TV Online
Senior Member
- Jun 26, 2023
- 104
- 291
Mchezaji wa Kimataifa wa Senegal na Timu ya Simba Pape Ousmane Sakho amewasilisha maombi kwenye Uongozi wa timu ya Simba ya kuomba kuondoka ili akatafute changamoto nje ya nchi.
Ousmane Sakho aliyebakiwa na mwaka mmoja wa kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi ana OFA nyingi barani Ulaya na zilizowekwa wazi ni za timu mbili za daraja la pili katika Taifa la Ufaransa. Timu hizo ambazo ofa zao ziko mezani kutoka Ufaransa ni pamoja na Grenoble na Stade Malherbe Caen.
Iwapo timu ya Simba watafunika juu ya ombi hilo ni wazi Sakho ataitumikia timu hiyo kwa kipindi kilichosalia kisha ataondoka kama mchezaji huru na Simba kutoambulia chochote.
Ousmane Sakho aliyebakiwa na mwaka mmoja wa kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi ana OFA nyingi barani Ulaya na zilizowekwa wazi ni za timu mbili za daraja la pili katika Taifa la Ufaransa. Timu hizo ambazo ofa zao ziko mezani kutoka Ufaransa ni pamoja na Grenoble na Stade Malherbe Caen.
Iwapo timu ya Simba watafunika juu ya ombi hilo ni wazi Sakho ataitumikia timu hiyo kwa kipindi kilichosalia kisha ataondoka kama mchezaji huru na Simba kutoambulia chochote.