KWELI Passport ya Tanzania haikubaliki kutumika kama Kitambulisho cha taifa (National ID)

KWELI Passport ya Tanzania haikubaliki kutumika kama Kitambulisho cha taifa (National ID)

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Kuna mijadala mingi inayosema kuwa Passport yetu ya Tanzania haikubaliki kama proof of ID je ni kweli?

E26997EE-FB64-4652-AE81-B7C7766DFD75.jpeg
 
Tunachokijua
Katika kutafuta ukweli wa jambo hili, JamiiForums imefanya mawasiliano na Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Mrakibu wa Uhamiaji, Paul John Mselle ambaye amesema;

Passport siyo Kitambulisho, ni hati ya safari anayopewa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa madhumuni ya kusafiri nje ya nchi. Pia, ni utambulisho wake akiwa nje ya nchi kuwa ni raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vitambulisho vipo vya aina nyingi na tofauti, kuna kitambulisho cha Utaifa, kitambulisho cha Mpiga Kura n.k, huwezi kufananisha passport na kitambulisho kwa sababu vitambulisho vipo vya aina tofauti tofauti.

Aidha, passport kwa madhumuni yake haitolewi kama Kitambulisho, lakini katika matumizi yake inaweza kutumika kama Kitambulisho.

Passport ya Tanzania kwa mujibu wa Sheria ya passport hutolewa kwa dhumuni la safari, haitolewi kwa matumizi kama ya kitambulisho kwa Mtanzania. Akiwa hapa nchini, Mtanzania anaomba passport kwa ajili ya safari.

Kama atataka Kitambulisho akiwa hapa nchini basi akachukue kitambulisho cha NIDA au cha kazi, hizi ndivyo vitamtambulisha.

Mselle amemaliza kwa kusema dhana ya Kitambulisho ni pana sana, pia dhana ya passport ni pana sana, lakini zinaweza kutumika kwa kubadilishana pale inapobidi.
Mbona magabacholi na wasomali hata wakenya wanazo? Sisi ni watu wa hovyo tusiojithamini na kuthaminiana mbali na utaifa wetu. Tungekuwa tunajitambua, hawa magabacholi wasingetokea kuwa matajiri wakati wakitubagua na kutudharau kama kuku.
 
Passport sio Kitambulisho cha Utaifa maana ili upate NIDA lazima uwe above 18

Ila Passport hata mtoto mchanga anapewa
Inabidi NIDA kibadirishe Jina kisiwe kitambulisho cha Taifa bali kiitwe kitambulisho cha utu uzima maana vip kuhusu huyu under 18 yeye anatambulika kama nani?

Nimawazo yangu tu usichukulie serious sana
 
Kuna wakati watu wanakataliwa kwenda kitambuliaho cha mpiga kura kwasababu mara nyingi huwa vunatolewa kisiasa zaidi
Katika jamii niliopo vitambulisho vya mpiga Kura hata changu vimekosewa jina kwahiyo mara nyingi tunahitajika na other supporting IDs kwa michakato mbalimbali
 
Passport sio Kitambulisho cha Utaifa maana ili upate NIDA lazima uwe above 18

Ila Passport hata mtoto mchanga anapewa
Matokeo ya kuishi in a shithole country, passport inatakiwa kiwe sehemu ya utambulisho na NIDA ilitakiwa kwa watoto wawe na number yake kwenye birth certificate, mzazi anaporuhusiwa kutoka kujifungua ni LAZIMA awe na birth certificate yenye ID NUMBER
 
Kuna mijadala mingi inayosema kuwa Passport yetu ya Tanzania haikubaliki kama proof of ID je ni kweli?
Kila kitambulisho kina mahala pake. Passport ni kwa ajili ya kutoka nje ya nchi, na unapokuwa nje hicho ndicho kitambulisho chako. Kitambulisho cha NIDA ni cha ndani na kinahitajika wakati ukiendesha mambo yote ya kisheria.

Hiki ni kithibitisho kuwa wewe ni raia. Kitambulisho cha mpiga kura kinakuruhusu wewe kuwa mpiga kura wa jimbo fulani la kura, na siyo popote TZ. Hiki unakipata kama una kitambulisho cha NIDA.

Pia passport unaipata ukiwa na kitambulisho cha NIDA.

Cheti cha udereva ni kithibitoisho mwenye nacho kasomea na kufuzu udereva.

Bado kuna kitambulisho cha mlipa kodi, kitambulisho cha kazi, na vitambulisho vingine chungu nzima (cheti cha ubatizo).
 
Mbona magabacholi na wasomali hata wakenya wanazo? Sisi ni watu wa hovyo tusiojithamini na kuthaminiana mbali na utaifa wetu...
Umaskini wako unaongeza mwenyewe, badala ya kutafuta umekaa unalalamika! Unataka hao unawaita Magabhacholi wakugawiye mali zao.

Wewe umekaa ukidhamini na kusifia ngono badala ya kutafuta sasa unalalamika. Wake up, before it is too late.
 
Serikali yetu sikivu iziambie Taasisi zote Nchini zikubali Passport yetu iwe proof of ID.
 
Kwani mtoto mchanga hana utaifa? Utaifa ni wa yeyote aliyezaliwa na wananchi wa taifa fulani. Kuna miitu mizima kama migabacholi inayovyo vitambulisho vya kitaifa wakati si watanzania.
Kitambulisho cha taifa ni kwa mkazi yeyote wa tz sio lazima awe raia wa tz
 
Matokeo ya kuishi in a shithole country, passport inatakiwa kiwe sehemu ya utambulisho na NIDA ilitakiwa kwa watoto wawe na number yake kwenye birth certificate, mzazi anaporuhusiwa kutoka kujifungua ni LAZIMA awe na birth certificate yenye ID NUMBER
Actually, ile notification number anayopewa mtoto wakat wa kupewa cheti cha kuzaliwa ilipaswa kuwa ndo ID yake moja kwa moja unless aukane uraia. Sijui tunakwama wapi
 
Umaskini wako unaongeza mwenyewe, badala ya kutafuta umekaa unalalamika! Unataka hao unawaita Magabhacholi wakugawiye mali zao. Wewe umekaa ukidhamini na kusifia ngono badala ya kutafuta sasa unalalamika. Wake up, before it is too late.
Wewe usiwe rofa.Namba ninayo ila kitambulisho sina kila nikienda kuchukua naambiwa niwe na sms kutoka kwao au niwe nimepigiwa?

Issue hapa muhusika wa juu awajibishwe aletwe mwingine huyo atakuwa makini na kazi yake.

Haiwezekani passport ninayo, National ID sina, Kuna uzembe wa hali ya juu mahali fulani hapo ila mtu mkuu hapo kalala hajui au anadanganywa ,au mtu ana cheti cha kuzaliwa hadi leo hana cheti cha Nida,ana namba tu toka Mhe. Dr. Magufulu atutoke na hata kabla tunaishi Kwa namba za Nida tu.Ukipoteza siku yako kwenda utaambiwa ulitumiwa sms au ulipigiwa mpaka unakuja,hivi inaingia akilini toka 2020 bado havijakamilika hata nusu yake?

vinashughulikiwa vipi hivyo au ulaji wa mtu?

Hapo Mama ang'oe mtu na kutoa agizo kali. Vipi Askali na wanajeshi ambao bado wana namba za Nida bila vitambulisho kwa miaka Toka Enzi za Mhe hayati Dkt. Magufuli.

Hii sio kweli watu wanakula mishahara ya bure.

Ajira ni pamoja na kutimiza maagizo Kwa wakati, ikishindwa jiengue mwenyewe sio mpaka Rais aongee ndio ujifanye unafuatilia jambo Kwa nguvu ya ajabu.

Kabla nguvu nyingi ni kugonga glass tu na kujipongeza
 
Back
Top Bottom