Pata elimu kidogo kuhusu makato CRDB

Pata elimu kidogo kuhusu makato CRDB

Siyo kubisha mkuu. We mwenyewe si umesema wamerekebisha makato sijui February? Mie naongea kitu nilichokiona. Labda kama wamerekebisha. Nilikuwa nikiangalia salio, kisha nikicheki e-statement nakuta nimekatwa. Sasa kama wamerekebisha mie sikujua hilo.
Acha uongo we jamaa...

kuangalia salio/mini-statement kupitia CRDB App hakunaga makato siku zote.
 
Mie baada ya kuona nakatwa nikawa nimeacha kuona salio. Nadhani mara ya mwisho kucheki salio ilikuwa mwaka jana sikumbuki vizuri ilikuwa mwezi upi. Mie ni mteja wao huu mwaka wa 11.
Cheki ulivoanza kubadili gia angani.
Kama hujui kitu uliza kwanza.

CRDB App haijawahi kuwa na makato upande wa kuangalia salio. Hata kucheki mini-statement ya mwezi mzima ni bure!
 
Mkuu we unatumia App ipi? Hii hii SimBanking app ama nyingine? Kama unatumia SimBanking na unadhani ni free basi utakuwa unakatwa ila hujijui kama unakatwa. Ukisha log in pale mwanzoni huwezi kuona balance directly. Mpaka u-click kile kijicho. Ukisha click tu tayari unakuwa umekatwa. Uwe unafuatilia balance yako utaona hayo makato. Kale kajicho hakapo kwa bahati mbaya. Na ili watukate kiulaini hawakwambii kwamba ku-click pale kutapelekea kukatwa. Wanakuacha ukatwe vizuri.
Kwanini unakua liongo hivi?
 
Acha uongo we jamaa...

kuangalia salio/mini-statement kupitia CRDB App hakunaga makato siku zote.
Mkuu sipo hapa kubisha wala kujifanya mjuaji. Siyo utamaduni wangu huu. Naomba tu tuendelee kufahamishana vizuri.

Hiyo jana wadau waliposema kuangalia salio ni bure ilibidi nifanye hivyo. Niliangalia salio kama mara 5 hivi kupata confirmation. Wakati naangalia salio kwenye hiyo account nilikuwa na balance ya Tsh 3449.12. Wakati huo sikukatwa na salio likabaki lilivyo. Baada ya saa kama 5 hivi baadae nikacheki tena na nikakuta salio langu ni zero.

Wakati huu ulipotoa jibu lako hili, nikaangalia tena nikakuta nina negative balance ya (Tsh -438.89). Nikawa nimejaribu kuomba statement ya mwezi mzima na naambiwa kuwa nina insufficient balance na hivyo siwezi kupata statement.

Sipo hapa kupika maneno wala kuleta ubishi usio na tija maana siyo utamaduni wangu.

1. Mkuu, with all due respect, nakuomba uelezee ni nini tafsiri ya maelezo hayo niliyotoa.
2. Je, hizo taarifa za kuwa ukiangalia salio kupitia App ni bure ulizipata wapi, ni ofsin kwao ama huwa unaangalia tu nakuondoka. Kisha hufanyi ku-trace tena account yako?

My take: Nadhani wewe na wadau wengine mnaosema hizo huduma ni bure (kuangalia salio na kuomba statement, achana na zile automatic statements za kila mwezi) huenda mtakuwa na akiba ya kutosha kwenye account zenu hivyo kikikatwa hicho kiasi kidogo mnadhani hakuna impact yoyote.

Kama siyo sahihi nachodhani, basi huenda kuna namna account yangu haipo sawa, na natakiwa kufuatilia, maana nakosa hizo huduma ili ziwe bure kama walivyo watu wengine.

Ahsante.

NB: Siwezi ku-screen shot hapa account yangu, ningeambatanisha na ushahidi.
 
waongo wanadai ukifungua account ya nmb bonuce account free sio kweli upande wa ATM Card wanataka makatoo
 
Aisee tunashukuru huu uzi unatufungua macho sana hizi bank zinatakiwa ziishtakiwe sio kwa sababu wanakata ila kwa sababu hawasemi ukweli kwa mteja mwisho wa siku ni kama wanakuibia kimya kimya. Ni sawa kununua dawa bila leaflet. Bank wanafanya uhalifu mkubwa na wizi kwa kuwa hawasemi ukweli kwa wateja. hivi hatuna vitengo sijui vya kulinda wateja Tanzania? nchi nyingine wangelipa kila walichochukuwa sababu hawakusema ukweli kutwa wanatangaza tumia bure. wezi wakubwa hawa mbwa
Tena kama Hawa NMB ndiyo wezi sana, wanakwambia kadi ya Chap chap Haina makato Kumbe ni wizi mtupu ukitumia ndani ya miezi mitatu tuu wanaanza kulima kama kawaida.
 
Internet banking kuwa bure it means uwe na application ya benki husika in your phone. Then hakikisha una bundle, fungua hyo app e.g NMB mkononi app, alaf angalia salio lako
Hqpana internet banking ile ya kwee app,
Unatumia http websites kuingia kwenye akaunt yako, kwa hiyo unaweza kuipata kwenye simu au computer or anything that can access interet
 
Maswali ya msingi kabla sijakuelezea makato...
a) Kipi Bora kutoa hela kupitia kwa Wakala, ATM au Ndan ya benk (Over the counter)?

b) Kipi Bora kuangalia salio kupitia kwa Wakala, NMB mobile/CRDB Simbanking, ATM au Ndan ya!
benk (Over the counter) au internet Banking?

c) Kama umemaliza kutoa hela ATM je kuna haja ya Kuomba resiti ya Salio au uangalie kupitia Simbanking? Kipi bora?

d) Je, ikienda kwa wakala kutoa hela zikagoma kutoka kwa sababau ya salio Dogo Wakala akakwambia akuangalizie salio, Je, unajua ni kiasi gan wanakata pia ukiunganisha na kutoa utakatwa kiasi gani?

e) Je, unaijua faida na hasara ya internet banking?

I. GHARAMA ZA KUANGALIA SALIO

Kwa njia ya :-
a) ATM NMB shs 360, CRDB shs 354/=

b) Simbanking NMB 400, CRDB 400/=
c) Kwa wakala NMB shs 2000, CRDB 2000/=

d) Teller/Over the counter NMB shs 400, CRDB 500/=

e) Internet banking NMB Free, CRDB Free

II. KTOA HELA (CASH WITHDRAWALS )

a) ATM
i. shs 1000-20,000 NMB shs 1100, CRDB 1300/=
ii. shs 20,001-50,000 NMB shs 1200, CRDB 1300/=

iii. shs 50,001-100,000, NMB shs 1300, CRDB 1300/=

iv. shs 100,001-200,000, NMB shs 1400, CRDB 150,000-600,000 ni 1500/=

v. shs 200,001-400,000 NMB shs 1500, CRDB 1500/=

b) Kwa teller/Over the counter mfano
kutoa 400,000/= utachajiwa 4000 CRDB, NMB 4000/=

c) Kwa Wakala
i. 10,000-19999 NMB shs 1200/=

ii. 20,000-49,999 NMB shs 1500/=

iii. 50,000-99,999 NMB shs 2200/=

iii. 100,000-199999 NMB shs 3500/=

iv. 200,000-399999 NMB shs 4500/=
v. 400,000-599999 NMB shs 6300/=

Kuna tabia
hii watu wengi wanapenda kuifanya. Unaenda kwa wakala kutoa mathalan 4000,000/= ktk akaunti yako kuna 405,000/= lazima hela itagoma, Wakala atakuuliza tuangalie salio? Ukijibu tu ndio ataangalia salio na ktk akaunti yako utakatwa 2000 kama ni CRDB na kama ni NMB utakatwa almost 1500 hapo atakwambia una Salio la shs 402,000/= basi itabidi utoe sh 397,000/=

Ndg yangu kama una huduma ya internet banking angalia salio lako free kisha mwambie kiasi cha kutoa.

Pia kama umetoa hela ATM usiwe na tabia ya kuchukua risiti, angalia salio lako kupitia internet banking ni free. Kwa wanachuo wanaokaa offcampus mathalan unataka kutoa 400,000/= ukitoa kwa wakala utakatwa 6300/= ila kwenye ATM ingekatwa 1500/= tu, unaonaje kama ungepanda haisi shs 200 chapu ukaenda ndan ukatoa na kurudi 200 ukawa umetumia gharama 1900/ kulikokukatwa 6500/=?

Maisha ni budget, so do at your own Risk

imeandaliwa na Big Phil
Uzi kabambe
 
Maswali ya msingi kabla sijakuelezea makato...
a) Kipi Bora kutoa hela kupitia kwa Wakala, ATM au Ndan ya benk (Over the counter)?

b) Kipi Bora kuangalia salio kupitia kwa Wakala, NMB mobile/CRDB Simbanking, ATM au Ndan ya!
benk (Over the counter) au internet Banking?

c) Kama umemaliza kutoa hela ATM je kuna haja ya Kuomba resiti ya Salio au uangalie kupitia Simbanking? Kipi bora?

d) Je, ikienda kwa wakala kutoa hela zikagoma kutoka kwa sababau ya salio Dogo Wakala akakwambia akuangalizie salio, Je, unajua ni kiasi gan wanakata pia ukiunganisha na kutoa utakatwa kiasi gani?

e) Je, unaijua faida na hasara ya internet banking?

I. GHARAMA ZA KUANGALIA SALIO

Kwa njia ya :-
a) ATM NMB shs 360, CRDB shs 354/=

b) Simbanking NMB 400, CRDB 400/=
c) Kwa wakala NMB shs 2000, CRDB 2000/=

d) Teller/Over the counter NMB shs 400, CRDB 500/=

e) Internet banking NMB Free, CRDB Free

II. KTOA HELA (CASH WITHDRAWALS )

a) ATM
i. shs 1000-20,000 NMB shs 1100, CRDB 1300/=
ii. shs 20,001-50,000 NMB shs 1200, CRDB 1300/=

iii. shs 50,001-100,000, NMB shs 1300, CRDB 1300/=

iv. shs 100,001-200,000, NMB shs 1400, CRDB 150,000-600,000 ni 1500/=

v. shs 200,001-400,000 NMB shs 1500, CRDB 1500/=

b) Kwa teller/Over the counter mfano
kutoa 400,000/= utachajiwa 4000 CRDB, NMB 4000/=

c) Kwa Wakala
i. 10,000-19999 NMB shs 1200/=

ii. 20,000-49,999 NMB shs 1500/=

iii. 50,000-99,999 NMB shs 2200/=

iii. 100,000-199999 NMB shs 3500/=

iv. 200,000-399999 NMB shs 4500/=
v. 400,000-599999 NMB shs 6300/=

Kuna tabia
hii watu wengi wanapenda kuifanya. Unaenda kwa wakala kutoa mathalan 4000,000/= ktk akaunti yako kuna 405,000/= lazima hela itagoma, Wakala atakuuliza tuangalie salio? Ukijibu tu ndio ataangalia salio na ktk akaunti yako utakatwa 2000 kama ni CRDB na kama ni NMB utakatwa almost 1500 hapo atakwambia una Salio la shs 402,000/= basi itabidi utoe sh 397,000/=

Ndg yangu kama una huduma ya internet banking angalia salio lako free kisha mwambie kiasi cha kutoa.

Pia kama umetoa hela ATM usiwe na tabia ya kuchukua risiti, angalia salio lako kupitia internet banking ni free. Kwa wanachuo wanaokaa offcampus mathalan unataka kutoa 400,000/= ukitoa kwa wakala utakatwa 6300/= ila kwenye ATM ingekatwa 1500/= tu, unaonaje kama ungepanda haisi shs 200 chapu ukaenda ndan ukatoa na kurudi 200 ukawa umetumia gharama 1900/ kulikokukatwa 6500/=?

Maisha ni budget, so do at your own Risk

imeandaliwa na Big Phil
kitu ambacho sijaelewa, kwa balance ya kama 20m wamekata karibia 165,000 kama monthly charges. si bora kuweka nyumbani tu, au nimeibiwa?
 
Back
Top Bottom