Simba msimu huu haikulenga kusajiri kwa kushindana katika mashindano ya Clab bingwa Afrika.
Ni Shiboub peke yake ndiye mchezaji mpya wa kigeni mwenye kiwango cha kusajiriwa Simba kwa ligi ya mabingwa Afrika.
Lakini ifahamike kuwa Simba kwa Sasa ni Kampuni na inajiendesha kibiashara.
Inawezeka malengo ya msimu huu ni kukuza biashara ndani ya Clabu, hivyo usajiri umezingatia kukuza vyanzo vya Mapato na kutengeneza faida, Kama ilivyokuwa kwa timu ya Asernal wakati fulani.
Ukimwacha Shiboub wachezaji wapya wa kigeni waliosajiriwa msimu huu wanaviwango vya chini wakilinganishwa na wachezaji wa ndani, akina Ajibu , au Rashidi Juma, Ndemla, Mzamiru, Mkude, au Miraji.
Ndio maana mapema ikatolewa na UD Songo ambayo nayo ishafungwa na Platinum ya Zimbabwe.
Msimu huu ni wa kufurahia swaga za akina Fraga, Santos, Wilka, Kanda, Kahata na wengineo na watakapo cheza na Polisi Moshi. na kutengeneza faida.
Tugange yajayo.
Yajayo ya Mshambuliaji wa kwenye benchi, mbrazili Wilka emarson.