Paul Clement ashauriwe, Asaidiwe, aombewe!

Paul Clement ashauriwe, Asaidiwe, aombewe!

Nikiri wazi mimi ni mmoja wa watu wanaompenda na kumfuatilia kwa karibu sana muimbaji wa Injili Paul Clement,
Toka enzi zile akiwa na glorious mpaka sasa akiwa solo artist..

Kwa hakika kijana huyu ana kipaji cha hali ya juu mno.
Lakini kwa miaka ya hivi karibuni toka aanze kuimba live amekuwa akizidisha mno kuyumbisha sauti yake kwa "minor" zisizokuwa na ulazima wowote na kupelekea kuharibu nyimbo zake yeye mwenyewe.

Ni wakati sahihi wa waimbaji wakongwe kukaa na kijana huyu na pasipo kumuonea aibu wamchane Ili arudi katika sauti yake halisi.
Anazidisha mbwembwe mnoo.
Kwa walioangalia au kuhudhuria Christmas carols ya tar 19 pale milimani city basi wataungana na mimi kuwa mmojawapo ya show mbaya Zaidi ilikua ni ya Paul,
Binafsi nakuombea urudi tena katika uimbaji wako kama Identity Yako acha kuiga iga wahuni.

Nakuombea.
Nilikuwepo,niliondoka ndo yeye anaimba!
In shot,sijawahi kuwa fan wake,huwa simuelewi
 
Sisi tuliokuwepo hatujaona tatizo shida moja ya paul hajui kuichangamsha hadhira yaani hana vibes nimehudhulia concert ambazo amehudumu kama 3 hiyo ndo shida yake kubwa niliyoiona
Hahaa,hata kuvaa bado! Asaidiwe
 
Back
Top Bottom