Paul Makonda atishia kuwataja wanaolipa watu 'Kumtukana Rais Samia mitandaoni', wamo Mawaziri

Huyo ni chizi.

Alipokuwa kwenye nafasi ya uongozi alishindwa kuwashughulikia ndio sasa ataweza.

Jinga sana.
 
Paul anatisha kama Hamas dadeki 🐼
Tupo huku Jordan tunaandaa makambi ya wakimbizi NDANI ya masaa 48 Iran itafanya kile kijeshi tunaita 'an imminent attack' ndani ya ardhi ya wazayuni!

Nilipata bahati ya kumuhoji msemaji WA jeshi la Israel jana Usiku, kasema wao kama Taifa lenye nguvu endapo tu Iran itadondosha makombora ndani ya jiji la Teraviv basi watavilenga Vinu viwili ndani ya Iran vikiwemo vile vya Bushehr na Arak.

Nimeuliza je, vipi mitambo ya Natanz, Fordow, esfahan, Bonab na ule mtambo mkubwa wa Parchin uliojengwa na mainjinia kutoka Urus?

Msemaji WA jeshi alisema kwa Maandalizi yaliyopo na yanayojulikana Iran italengwa kwa kutumia ndege za stealth aina ya F 35 hivyo Lazima walenge mzingo wa Arak na Bushehr ambapo teknolojia kubwa imetumika na sehemu kubwa ya.mitbo Hiyo ipo chini ya ardhi!

Uwenda Wakati wowote pakaibuka vita kubwa kabisa kuwahi kutokea kwani leo tulimfata Yasin Nasrara Mkuu wa kamandi ya Hezbollah inayodhaminiwa na Iran alikiri kuwa tayari washaelekezwa kujiweka tayari kwa vita kubwa nw nzito.

Wakuu wa majeshi wa Marekani na Uingereza wamekutana kwa Siri nchini Oman kujadili namna ya kuivamia Iran.
 
..huenda kuna ombwe ktk uongozi, na Makonda ameamua kulijaza.
Nadhani huyu alitisha sana viongozi wakati wa JPM, ni Bingwa wa Fitna, ana uwezo wa kufanya lolote kama tunavyojua.

Fitna ya uongo madawa ya kulevya , si uliona wakati huo SSH akiwa VP, Mjaliwa PM walikuwa kimyaa
Fitna kwa Sirro akiwa kanda maalum, nani alikemea
Akina VP, PM, NWM n.k. wanamuogopa huyu bingwa wa Fitna. Lakini pia aliyempa madaraka hawezi kumdhibiti!! ???
 
Inatisha sasa. Kuna hofu anayo aliyemteua. Kuna vitu anamhitaji na anaamini Paul atamsaidia lakini historia inanifanya kuamini kuna vitu anahofia vitatokea akienda kinyume nae.
 
Ufalme uliofitinika kamwe hauwezi kusimama wenyewe. Inabakia kuwa ni sawa tu na dimbwi la tope la kambare, huku kila mmoja akiwa ana sharubu zake zenye kumfananisha na wenzake.

Hakuna tena mamlaka rasmi za kudhibiti taarifa nyeti za mpenyezo wala maadili ndani ya chama wala serikali. Kamishina wa Mkoa tu anawapiga mkwara mabosi wake, tena mbele ya mabosi wake wakuu. Hakuna "formal span of communications" kwa watawala zaidi ya uwepo unajidhihirisha wa "over - dependence of grapevine"?

Asipodhitiwa anaenda kuiabisha mamlaka ya uteuzi. Anazo zote "job description & job jurisdiction" akiwa katika nafasi aliyopewa dhamana ya kuishika. Lakini hata wiki moja haijapita anaanza kutafuta kiki kwa nguvu akiwa ofisi mpya na kuanza kuparamia mambo yasiyoparamika.

Pengine ni mwana mpendwa kwa mama, kama ilivyokuwa kwa baba. Asili ya kawaida ya hali ya maji ni ukimiminika, ubarafu na umvuke ni mazingira yanayotokana na ulazima wa muda tu!
 
Kumbe rais ni mama yake ?

Sema ccm wameshusha sana standard ya uongozi nchi hii.
 
Inatisha sasa. Kuna hofu anayo aliyemteua. Kuna vitu anamhitaji na anaamini Paul atamsaidia lakini historia inanifanya kuamini kuna vitu anahofia vitatokea akienda kinyume nae.
Kwa madudu aliyofanya huyu bwana wakati wa JPM hakuwa mtu wa kufikiriwa katika uongozi
Hata ndani ya CCM hakubaliki, viongozi wenzake hakubaliki tena wakiwemo waandamizi lakini bado!!!

Ukiacha Fitna, hajawahi kufanya jambo lolote likafanikiwa, sasa kwanini mtu anayenyooshewa vidole bado apewe dhamana kubwa!!

Mleta mada kazungumza vizuri sana kwamba Arusha ni makao makuu ya EAC, ni Mji wa Utalii mkubwa Tanzania, ni kituo cha madini makubwa na kitovu cha uchumi wa utalii na Mazao. Tulitegemea Mkuu wa Mkoa huo awe na uwezo wa kukabiliana na changamoto zitokanazo, sasa tunasikia akilumbana na watu wa mitandaoni

Alitakiwa ajielekeze katika mambo yanayoleta Dollar, kutangaza Utalii na madini na kutumia fursa ya uenyeji wa EAC kuleta tija na si kulumbana na wana mitandaoni. Yaani ni low IQ lakini bado anapewa dhamana. sidhani kama yeye ni tatizo! no!
 

Sijawahi kumuelewe huyu jamaa. Kama kweli anazo hizo taarifa, kwanini anazisema hadharani wakati ni sensitive kiasi kikubwa sana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…