Pawn Shops nchini Tanzania

Mbona zipo sana sema mitaji ni midogo
 
Mbona zipo sana sema mitaji ni midogo
Kwa hiyo sheria inaruhusu uwepo wake mkuu!

Kwanini unadhani wenye mitaji mikubwa hawawekezi huko?
 
Kwa hiyo sheria inaruhusu uwepo wake mkuu!

Kwanini unadhani wenye mitaji mikubwa hawawekezi huko?
Kwa sababu wabongo wengi hawana vitu ya thamani.Na wakija na vitu vyao wanakuwa na lengo la kuviuza na sio kuweka dhamana.So unakuta kitu cha laki mtu anataka umpe 90 au gari ya Milioni 10 mtu anataka milioni 8 wakati katika pawn shops unapewa maximum 30% ya actual value ili usishidwe kugomboa ila ukishindwa unapoteza yote.So ndo maana kuna watu wana yard za magari ya watu ambao wamekopa na kuyapaki.
 
Ila lengo la pawn sio kuuza mkuu. Ni kuweka kwa muda.
.ukishindwa kurejesha pesa ndiyo mali yako inauzwa.

Mara zote kama umekuja na gari ya mil 10 nitakupa mkopo wa robo ya gari lako na interest ndogo.

Ukirudisha pesa unachukua chombo chako...

Haujanijibu la sheria. Je hayo maduka uliyosema yanafanya hii kazi...yana leseni ya hii kazi?
 
Hapo ndipo swali langu lilipokuwa Monk..

Kwanini sasa sheria hairuhusu au hakuna wateja?

Nafikiri hakuna mtu amewaza kufanya hicho kitu kwa huo mtindo. Wengi wamejikita kwenye ukopeshaji kwa muundo wa vikoba, saccos na hizo za riba.

Lakini uwekezaji wake ni mkubwa kidogo, hasa kuwa na ghala la kuhifadhi hivyo vitu na ulinzi wake mishahara na pia mchakato wa kujihakikishia kwamba bidhaa sio ya wizi na mmiliki ndio mwenyewe halisi anaekuja kukiweka hicho kitu dhamana inaweza kuwa usumbufu.

Ila naamini ni eneo zuri likifanyiwa upembuzi kuwekeza.

Mathalani mtu anashida ya haraka kama 300,000 na ana kitu chake cha thamani kuliko kuumiza kichwa anaenda pale mara moja, wanamalizana mambo ya nyaraka sifikirii itafika lisaa limoja unaenda kutatua matatizo yako.

Jamaa wanawweza kuhitaji thamani ya kitu iwe juu kuepusha kuuziwa vitu kijanja kisha wakakosa wakumuuzia.
 
Sijawai kuona Tanzania japo nahisi kitu hiki kinafanyika sana
 
Ila wanachofanya kina Kimaro Mapua huku mtaani ni hicho hicho tofauti ni urasmi tu, na wao hulenga zaidi Magari maana wengi wao huwa pia ni Madalali wa Magari.....na Wenye Mamlaka hawawezi kuruhusu maana watakwambia hiyo inaingia kwenye lile kundi la 'mikopo umiza'.
 
Okay nimeielewa sasa. Nadhani zipo lakini si rasmi.
 
Kwa Maduka ambayo ni halali sina uhakika kama yapo lakini biashara ya Pawn watu wanaishi nayo sana mjini....hata utake million ngapi...inathaminishwa Mali tu unapewa kiasi cha pesa.
Ila bahati mbaya tetesi zinasema hawa Madon wakikukopesha pesa zao huwezi zirudisha hivyo hupelekea kupoteza Mali kwa bei chee...wadai ni wazee wa ndumba nyingi...ukikopa hupati hela mpaka deadline ipite ndo unapata hela huku ukiwa umedhapoteza Mali kiroho safi...Don anauza anapiga hatua...
 
Kumbe hii pawn shop Haina tofauti sana na hii mikopo ya kuweka kitu Kama dhamana..!! 🤔..tatizo kuruhusiwa kisheria kumbe..
 
Kumbe hii pawn shop Haina tofauti sana na hii mikopo ya kuweka kitu Kama dhamana..!! 🤔..tatizo kuruhusiwa kisheria kumbe..
Kuna ishu ya usalama wa kifaa chako pia, maana kumuachia ni jambo moja na kuja kurudishiwa kifaa chako tena kikiwa salama pale unapomaliza deni ni jambo lingine.
 

zipo kariakoo hapo kibao .
ila kwa tanzania inaweza kukutoa kwenye reli maana polisi watakufilisi .sheria zetu bado
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…