PCCB wafungua kesi dhidi ya Lugumi na Jeshi la Polisi, IGP na Katibu wa Wizara waitwa Bungeni Dodoma

PCCB wafungua kesi dhidi ya Lugumi na Jeshi la Polisi, IGP na Katibu wa Wizara waitwa Bungeni Dodoma

Lugumi, Standard Bank, Azania bank nk wametakatisha fedha, mashitaka yao ni yale yale ya akina Shose.
 
Shanba la bwana kheri, mbuzi waliokula mazao ni wa bwana kheri, akida ni bwana kheri. HAKUNA KESI HAPO
 
Abiria Tanzania.jpg
 
Waziri wa Mambo ya ndani Charles Kitwanga amekana kuhusika kabisa na kampuni ya Lugumi ambayo kwa sasa inakabiliwa na kashfa nzito ya rushwa na uhujumu uchumi ambayo ilipewa tenda ya kufunga vifaa vya kuchukulia alama za vidole kwenye vituo vyote vya polisi kwenye Wilaya zote nchini na kushindwa kukamilisha tenda hiyo.

Juhudi mbalimbali zinazofanywa kuujua ukweli wa sakata hili umepelekea taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini(TAKUKURU) kutoa tamko la kuifungulia kesi mahakamani kampuni hii ya Lugumi pamoja na jeshi la polisi na kufanya uchunguzi wa kina wa sakata hili.

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC) imewaita bungeni IGP pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ambapo watakuwa na kikao leo bungeni Dodoma na baadae baada ya kikao hicho ndipo wataweza kuongea na waandishi wa habari kuhusu suala hili.

Kigugumizi cha kukabidhi taarifa ya utekelezaji wa mkataba na Lugumi; inatosha kutilia mashaka mkataba huo. Namsikitikia katibu mkuu wa wizara hiyo ambaye ni mgeni hapo wizarani sasa CV yake inachafuliwa kwa mkataba ulioingiwa na watu wengine kabisa! Wa kubeba msalaba huo ni Said Mwema, Mangu na mawaziri wao waliopita, wawekwe kitanzini!
 
Watasema swala liko mahakamani ili lisijadiliwe bungeni halafu Kesi itaondolewa na DPP mchezo kwisha na Watanzania tunavyosahau kwa haraka tukihoji tu... Wanazua ule Mchongo wa Escrow ya Stanbic kisha Lugumi anawekwa kando tukihoji Ile wanarudi na hukumu ya EGMA tunasherehekea baada ya miezi miwili jamaa wanaenda kufagia posta kisha yanakuwa huru. Basi mwaka unakuwa umeisha tunajipanga kwa season nyingine na nchi ndo inakuwa inasonga hivyo.

Haya ndio JPM amesema hataki kuyaona yanatokea kwenye serikali yake. Mtu akishakamatwa na vizibiti, upelelelezi wa nini tena? Kula na majizi sahani moja tu. Hakuna kupoteza muda, tumeshachelewa sana tena sana tu. Ni bora kufanya maamuzi na kuchukua hatua za haraka badala ya kujifanya unaruhusu mafisadi yapindishe sheria
 
PCCB hawana jino la kwenda mahakamani, wao wakichunguza hupeleka faili kwa DPP ambaye huamua kufungua kesi mahakamani.

Ndo maana tunataka katiba ibadilishwe..........huu urasimu huu juu ya wezi na wahujumu uchumi wa nini?..
 
Wanajamvi tupunguze mihemko na matarajio kwa kutanguliza siasa. Serikali ya Dr Magufuli si ya kisiasa ila ya kiutendaji kwa kufuata sheria. Hapa Kazitu# tafsiri yake ni vitendo. Kwa hivyo katika mlolongo wa kutafuta ukweli, kwa kila tendo nje ya utaratibu, haki itatendeka kupitia vyombo halali vilivyopo kisheria kwa sasa. Lakini wengi wetu humu tunajifanya wapelezi, waendesha mashitaka, na mahakimu kwa wakati mmoja, du!!
 
Yaani Jeshi la Polisi kushitakiwa na TAKUKURU??
Na Jeshi la polisi likikaidi kwenda mahakamani, ni kina nani watatumwa waende wakalikamate hilo jeshi la Polisi? Polisi haohao??

Si jeshi litakaloshitakiwa ila baadhi ya wana-jeshi la polisi ambao walihusika na kufanikisha ubaya wowote utakaojulikana. Kumbuka kwamba walipewa majukumu na mamlaka (authority) kwa dhamana ya wananchi, na hivo wanahitajika kuwajibika (be held accountable) pale wanapotumia madaraka pasi kujali maslahi mapana ya kitaifa.

Pia, waliofanya hayo si jeshi lote kama lilivyo, ila hao wachache, na hivo watatofautishwa na kuchukuliwa hatua kama watu wengine waliowajibishwa. Jeshi linabakia kuwa muhimili muhimu ambapo sidhani kama litashitakiwa wakili gani atalitetea iwapo mwanasheria mkuu anahusika na taasisi zote mbili, yaani PCCB na TPF.
 
Habari zenu familia ya JF. Hii kampuni sio ngeni miongoni mwenu. Utakumbuka kampuni hii ilishinda tenda ya kufunga fingerprints ama mashine ya alama za vidole kwenye vituo vikuu vya polisi wilaya za Tanzania Bara. Cha ajabu haikufanya kazi kwa ufanisi licha kutia kibindoni zaidi ya Tsh bilioni 100.

Pia kuna suala la mabilioni ya polisi yaliyotumika ktk manunuzi hewa ya Silaha, magari na sare.Hili aliwahi kutamka rais kwa mdomo wake mwenyewe bila kusahau yule mfanyabiashara aliyekuwa anaiba kwa kutumia EFD mashine mamilioni ya pesa kwa sekunde, yaani alipewa tenda na TRA kama wakala wa kukusanya mapato yeye akageuza mradi binafsi na kuwasilisha kidogo huku yeye akitukomba pakubwa!!!!!

Hili pia kaliibua Rais Magufuli. Sasa huu ukmya juu ya upotevu wote wa pesa za umma unatokana na nini?
 
Ukiona kimya ujue mfupa mgumu umemshinda...

Ukiacha Lugumi kuna wengi tu wamefanya ubadhilifu awamu zilizopita lakini hajawagusa.. Double Standard.

Hata hivi sasa sio kwamba watu hawapigi.. NO.

Watu wanapiga sana tu ila ni watu wake type ya mtoto kipenzi RC na mtoto wa Dada pale Hazina.

Mfano halisi hivi karibuni mtoto wa dada pale Hazina walikuwa wanalipana posho ya Tsh 400,000/ kwa kazi ambayo haina kichwa wala miguu.Wamelipana kwa mtu mmoja mpaka Tshs 18M mbona Mkuu yupo kimya tu??

So upigaji upo na utaendelea ila ni kwa watu wake tu.
 
Kuna mambo yanaumiza kichwa sana sana, ukianza kuyaainisha utachanganyikiwa kabisa. CCM walaaniwe kabisa, najua utaniuliza CCM wanaingiaje? Kwa mwenye akili atakua amenielewa.
 
Back
Top Bottom