Blue Bahari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,851
- 2,171
Uongo umechanganywa na ukweli.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani anaeleta mada kwamba rwanda anaingia DRC kwaajili ya kusaidia watutsi ni ujinga mtupu inamaana leo tanzania inavyowaondoa wamasai ngorongoro kenya inaweza kuingilia kwasababu na kenya kuna wamasai.Sorry Tanzania ikianza kuwafukuza wahaya w bukoba je Uganda itawatetea? Kisa kuna wahaya pia Uganda?
KAZI ni kipimo cha UTU
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAJE.Tuiombee nchi yetu amani, nchi ikianza hayo mambo ndio mwanzo wa anguko
Nchi inajengwa na watu wake ndani ya mipaka yake, wakifukuzwa wanakuwa wakimbizi hata kama kuna kabila lao nchi inayopakana.,
Nchi inabidi iweka tofauti za kikabila pembeni kudumisha utaifa wa watu wote ndani ta mipaka.
View attachment 3217063
Kabla ya kuilaumu Rwanda kuhusu suala la M23 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), nataka nikupatie historia fupi kuhusu kinachoendelea katika sehemu ya mashariki ya Congo. Hii ilianza vipi?
Unachosikia kila mara ni kwamba Rwanda inaunga mkono waasi wa M23, na serikali ya DRC inapambana na waasi wa M23 ili kukomboa sehemu ya mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hayo ndiyo unayosikia kwenye habari kila siku. Lakini nataka nikuambie kilicho nyuma ya pazia kinachoendelea huko.
Twende nyuma kwenye chanzo cha tatizo hili. Wakati wa Mkutano wa Berlin Confeence enzi za ukoloni, Wakoloni walikuwa wanaigawa Afrika miongoni mwao, Wabelgiji walichukua Congo, Wajerumani walichukua Rwanda, Wajerumani pia walichukua Tanzania, na Waingereza walichukua Uganda na Kenya. Waligawanya maeneo haya bila kujali mipaka ya makabila.
Makabila mengi barani Afrika yaligawanywa kwa mipaka ya nchi, utakuta kabila moja linapatikana pande zote mbili za mpaka. Hili ni jambo la kawaida sana Afrika kwa sababu Wakoloni hawakujali wanavyogawanya makabila haya, Wahaya unawakuta Uganda na Kagera, Wakurya unawakuta Kenya na Tanzania, Wamakonde unawakuta Tanzania na Msumbiji, Wanyakyusa unawakuta Tanzania na Malawi.
Katika mgawanyo huu, kabila la Watutsi liligawanywa kati ya nchi mbili: Rwanda na Zaire ya wakati huo ambayo sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Sasa, kwa nini waasi wa M23 wanapigana dhidi ya majeshi ya serikali ya DRC na Umoja wa Mataifa katika mashariki mwa Kongo? Na M23 ni akina nani?
Waasi wa M23 ni kundi la waasi lililoanzishwa na Watutsi wenyewe ili kulinda ardhi yao, ambayo ni sehemu ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Walijilinda dhidi ya nani? Dhidi ya serikali ya DRC ambayo imekuwa ikijaribu kuchukua ardhi yao kinyonyaji.
Labda unajiuliza, kwa nini kundi la watu linajaribu kujilinda dhidi ya serikali yao wenyewe? Ndiyo, hiyo ndiyo hali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hakuna utawala wa sheria. Kila mtu anajitafutia mwenyewe. Wanyonge hukosa ardhi na kusambaratishwa.
Mataifa Super power kama Marekani, China, na Urusi yameingia DRC na kuchagua maeneo wanayotaka kuchimba madini, Maeneo mengi yenye madini wenyeji huwa wanafukuzwa, kukiwa na upinzani wa wenyeji ndio unaweza kuyapa silaha makabila yanayoishi huko kupigana na makabila mengine yatayoleta upinzani, inapobidi jeshi hupelekwa ni mpaka serikali yenyewe inahusika.
Majeshi ya DRC mara nyingi hutumia mbinu za kuwahamisha watu wa maeneo fulani na kuruhusu makampuni ya Kimarekani, Kibelgiji, na Kifaransa kufanya uchimbaji wa madini katika maeneo hayo huku wakazi wa asili wa maeneo hayo wakisambaratishwa na kuwa wakimbizi, HICHO NDICHO WATUTSI WAMEKATAA !!
Hii ndiyo sababu Watutsi wa mashariki mwa Kongo walilazimika kujihami, kwanza kupitia Banyamulenge, na sasa kupitia M23. Katika DRC kabila lisilo na silaha ni kabila lililomalizika, hasa ikiwa linaishi kwenye ardhi yenye utajiri, Utafukuzwa ukileta kiburi unapigwa chuma.
Mashariki mwa Kongo ina utajiri wa madini kama uranium, lithiamu, na madini mengine yanayotumika kutengeneza simu, drones, na betri za magari ya umeme. Ndiyo maana mapigano yamejikita katika sehemu hiyo kwa sababu Super Powers wanataka kuchukua madini hayo lakini haijawa rahisi palewanapotaka kuwafukuza Watutsi wa eneo hilo kwa kutumia jeshi la Congo na vikosi vingine vinavyoaminishwa uongo kwamba maeneo hayo yametekwa na M23, lengo ni kuwatoa hao Watutsi wanaokataa kuhama.
Ndio maana watu wengi wamebaki midomo wazi kuona wakongo wa mahariki wakiserekea m23 walipoikamata Goma kwa muda, Ni wazi kwamba hata kushindwa kwa jeshi la Congo na vikosi vingine ni kwasababu ya kukosekana kwa ushirikiano na wananchi wa huko, wao wapo upande wa M23
View attachment 3216996
Rwanda inaingiaje kwenye hili? Watutsi wa mashariki mwa Kongo waliomba msaada kutoka Rwanda kwa sababu wanashirikiana lugha moja, tamaduni moja, na dini moja. Rwanda chini ya serikali ya Watutsi, haikuweza kuwapuuza.
Zaidi ya hayo, baada ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda, Wahutu waliokimbia walijikusanya mashariki mwa Kongo kujaribu kurudi na kuipindua serikali ya Rwanda kwa nguvu. Hivyo, usalama wa Rwanda unategemea kuwadhibiti Wahutu walioko DRC. Rwanda inatumia Watutsi wa mashariki mwa Kongo kuzuia tishio hilo.
Serikali ya DRC wanafanya kazi kwa maslahi ya mataifa mengine yenye hamu ya kuchukua madini ya mashariki mwa Kongo. Umoja wa Mataifa pia unatumika kama kifuniko kwa unyonyaji huo.
Kwa kumalizia, Watutsi wa mashariki mwa Kongo hawapaswi kufukuzwa kutoka kwenye ardhi yao. Serikali ya DRC inatumia propaganda dhidi ya Rwanda kwa maslahi ya kiuchumi na unyonyaji wa madini. Tunapaswa kuwa na mjadala wa wazi kuhusu ukweli huu.
View: https://x.com/Roel6825008/status/1883996837138555357?t=PS1N_WYp2FhC4v1gdIjlVw&s=19
Point nzito hii, ndicho ambacho hata Nyerere alikishauriDawa hapo, ni wakongo Watusi, wapewe ardhi Yao, wajitawale,
Au wwingize kwenye jeshi LA nchi,
Uwezi kuwafukuza Masai wa Arusha, waende Kenya, bila ardhi, kama uwataki, mega Arusha, iende Kenya na watu wake, sasa vuongozi wa Kinshasa, wao wanstaka wawafukuzewanyamurenge, Watusi wakongo, waende Rwanda, ila ardhi Yao, ibaki Congo! It's stupid! Ni sawa sawa, uwataki wahaya, unataka waende Uganda, ila kagera, ibaki TZ! Kama uwataki, wafukuze na ardhi Yao!
lSorry Tanzania ikianza kuwafukuza wahaya w bukoba je Uganda itawatetea? Kisa kuna wahaya pia Uganda?
KAZI ni kipimo cha UTU
💯%💐💐💐Dawa hapo, ni wakongo Watusi, wapewe ardhi Yao, wajitawale,
Au wwingize kwenye jeshi LA nchi,
Uwezi kuwafukuza Masai wa Arusha, waende Kenya, bila ardhi, kama uwataki, mega Arusha, iende Kenya na watu wake, sasa vuongozi wa Kinshasa, wao wanstaka wawafukuzewanyamurenge, Watusi wakongo, waende Rwanda, ila ardhi Yao, ibaki Congo! It's stupid! Ni sawa sawa, uwataki wahaya, unataka waende Uganda, ila kagera, ibaki TZ! Kama uwataki, wafukuze na ardhi Yao!
Kabla ya kuilaumu Rwanda kuhusu suala la M23 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), nataka nikupatie historia fupi kuhusu kinachoendelea katika sehemu ya mashariki ya Congo. Hii ilianza vipi?
Unachosikia kila mara ni kwamba Rwanda inaunga mkono waasi wa M23, na serikali ya DRC inapambana na waasi wa M23 ili kukomboa sehemu ya mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hayo ndiyo unayosikia kwenye habari kila siku. Lakini nataka nikuambie kilicho nyuma ya pazia kinachoendelea huko.
Twende nyuma kwenye chanzo cha tatizo hili. Wakati wa Mkutano wa Berlin Confeence enzi za ukoloni, Wakoloni walikuwa wanaigawa Afrika miongoni mwao, Wabelgiji walichukua Congo, Wajerumani walichukua Rwanda, Wajerumani pia walichukua Tanzania, na Waingereza walichukua Uganda na Kenya. Waligawanya maeneo haya bila kujali mipaka ya makabila.
Makabila mengi barani Afrika yaligawanywa kwa mipaka ya nchi, utakuta kabila moja linapatikana pande zote mbili za mpaka. Hili ni jambo la kawaida sana Afrika kwa sababu Wakoloni hawakujali wanavyogawanya makabila haya, Wahaya unawakuta Uganda na Kagera, Wakurya unawakuta Kenya na Tanzania, Wamakonde unawakuta Tanzania na Msumbiji, Wanyakyusa unawakuta Tanzania na Malawi.
Katika mgawanyo huu, kabila la Watutsi liligawanywa kati ya nchi mbili: Rwanda na Zaire ya wakati huo ambayo sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Sasa, kwa nini waasi wa M23 wanapigana dhidi ya majeshi ya serikali ya DRC na Umoja wa Mataifa katika mashariki mwa Kongo? Na M23 ni akina nani?
Waasi wa M23 ni kundi la waasi lililoanzishwa na Watutsi wenyewe ili kulinda ardhi yao, ambayo ni sehemu ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Walijilinda dhidi ya nani? Dhidi ya serikali ya DRC ambayo imekuwa ikijaribu kuchukua ardhi yao kinyonyaji.
Labda unajiuliza, kwa nini kundi la watu linajaribu kujilinda dhidi ya serikali yao wenyewe? Ndiyo, hiyo ndiyo hali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hakuna utawala wa sheria. Kila mtu anajitafutia mwenyewe. Wanyonge hukosa ardhi na kusambaratishwa.
Mataifa Super power kama Marekani, China, na Urusi yameingia DRC na kuchagua maeneo wanayotaka kuchimba madini, Maeneo mengi yenye madini wenyeji huwa wanafukuzwa, kukiwa na upinzani wa wenyeji ndio unaweza kuyapa silaha makabila yanayoishi huko kupigana na makabila mengine yatayoleta upinzani, inapobidi jeshi hupelekwa ni mpaka serikali yenyewe inahusika.
Majeshi ya DRC mara nyingi hutumia mbinu za kuwahamisha watu wa maeneo fulani na kuruhusu makampuni ya Kimarekani, Kibelgiji, na Kifaransa kufanya uchimbaji wa madini katika maeneo hayo huku wakazi wa asili wa maeneo hayo wakisambaratishwa na kuwa wakimbizi, HICHO NDICHO WATUTSI WAMEKATAA !!
Hii ndiyo sababu Watutsi wa mashariki mwa Kongo walilazimika kujihami, kwanza kupitia Banyamulenge, na sasa kupitia M23. Katika DRC kabila lisilo na silaha ni kabila lililomalizika, hasa ikiwa linaishi kwenye ardhi yenye utajiri, Utafukuzwa ukileta kiburi unapigwa chuma.
Mashariki mwa Kongo ina utajiri wa madini kama uranium, lithiamu, na madini mengine yanayotumika kutengeneza simu, drones, na betri za magari ya umeme. Ndiyo maana mapigano yamejikita katika sehemu hiyo kwa sababu Super Powers wanataka kuchukua madini hayo lakini haijawa rahisi palewanapotaka kuwafukuza Watutsi wa eneo hilo kwa kutumia jeshi la Congo na vikosi vingine vinavyoaminishwa uongo kwamba maeneo hayo yametekwa na M23, lengo ni kuwatoa hao Watutsi wanaokataa kuhama.
Ndio maana watu wengi wamebaki midomo wazi kuona wakongo wa mahariki wakiserekea m23 walipoikamata Goma kwa muda, Ni wazi kwamba hata kushindwa kwa jeshi la Congo na vikosi vingine ni kwasababu ya kukosekana kwa ushirikiano na wananchi wa huko, wao wapo upande wa M23
View attachment 3216996
Rwanda inaingiaje kwenye hili? Watutsi wa mashariki mwa Kongo waliomba msaada kutoka Rwanda kwa sababu wanashirikiana lugha moja, tamaduni moja, na dini moja. Rwanda chini ya serikali ya Watutsi, haikuweza kuwapuuza.
Zaidi ya hayo, baada ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda, Wahutu waliokimbia walijikusanya mashariki mwa Kongo kujaribu kurudi na kuipindua serikali ya Rwanda kwa nguvu. Hivyo, usalama wa Rwanda unategemea kuwadhibiti Wahutu walioko DRC. Rwanda inatumia Watutsi wa mashariki mwa Kongo kuzuia tishio hilo.
Serikali ya DRC wanafanya kazi kwa maslahi ya mataifa mengine yenye hamu ya kuchukua madini ya mashariki mwa Kongo. Umoja wa Mataifa pia unatumika kama kifuniko kwa unyonyaji huo.
SOLUTION
Huwezi kuwafukuza Wamakonde wa Mtwara waende Msumbiji bila ardhi, kama huwataki mega Mtwara ihamie Msumbiji na watu wake, it takes two to tangle ! sasa vuongozi wapo Kinshasa, wao wanataka wawafukuze watu huko Mahariki waende Rwanda, ila ardhi ibaki Congo! NI UONEZI !
- Ukiwafukuza wahaya wape ardhi yao waiunge Uganda au iwe nchi
- Ukiwafukuza Waha wape ardhi yao waiunge Burundi au iwe nchi
- Ukiwafukuza Wanyiha wape ardhi yao waiunge Zambia au iwe nchi
- Ukiwafukuza Wanyaki wape ardhi yao waiunge Malawi au iwe nchi
- Ukiwafukuza Wamakonde wape ardhi yao waiunge Msumbiji au iwe nchi
- Ukiwafukuza Wachaga wape ardhi yao waiunge Kenya au iwe nchi
- Ukiwafukuza Wamasai wape ardhi yao waiunge Kenya au iwe nchi
- Ukiwafukuza Wakurya wape ardhi yao waiunge Kenya au iwe nchi
View: https://x.com/Roel6825008/status/1883996837138555357?t=PS1N_WYp2FhC4v1gdIjlVw&s=19
Kama serikali inataka kuwanyanyasa na kutaka kuwaondoa kwenye ardhi yao wanaweza kujikusanya kupambana na serikali yao.ACHA UPUMBAVU.
KWAHIYO UNATAKA WAKURYA WA KENYA WAPAMBANE NA SERIKALI KULINDA ARDHI YAO?
HIVI HUU UPUMBAVU MNAANDIKA BAADA YA KULA NINI?
Tshesekedi ameamua kuwa mkabila kama waliomtangulia, hivi inawezekana vipi leo uwaambie Banyamurenge walioishi Congo kabla ya partition of Africa leo waondoke na kuwaita watusi wa Rwanda na kuanza kuwaua, imagine unawaambia wamasai au wakurya warudi Kenya na kuanza kuwaua, ni sawa na kina Kagame walipofukuzwa na kuwa wakimbizi kwa miaka 50 huku wakiambiwa hamuwezi kurudi nchi imejaa, ni very simple solution acha ukabila na wahakikishie usalama wao, hizo story za M23 wanataka kuigawa nchi ni upuuzi mtupu na kumbuka Banyamurenge walishafanyiwa genocide na Congolese army na vikundi vya wahutu waliokimbia Rwanda, mambo nani anafadhiri nobody cares na hayataleta amaniKuna kitu hakisemwi....
Ni nani wanazifadhili pande zote mbili za mapigano?
Yani hao M23 na Kagame wao VS DRC na wanajeshi wao...
Naombeni majibu.. maana hao ndo washenzi na tukiwajua ndo tumemjua mchawi. Which Western Countries is on either sides!?
Alafuuu...hao Mnaowaita Watusi wa Eastern Congo wanawajibika kwa Nchi gani!? Yani huduma za kijamii ie shule, maji , umeme, masoko(exchange) , banks, saragu ipi wanatumia... Au ni ka nchi kenyewe kasiye na Baba wala Mama...
Naomba majibu.