PDPC: Ukifika nyumba ya Kulala Wageni, marufuku kuandika unapotoka na unapokwenda

PDPC: Ukifika nyumba ya Kulala Wageni, marufuku kuandika unapotoka na unapokwenda

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
TUME ya Ulinzi wa Taarifa (PDPC), imesema kuwa unapokwenda nyumba ya kulala wageni hairuhusiwi kuandika ulikotoka na unakokwenda kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya taarifa binafsi.

Akiwasilisha mada ya zana ya taarifa binafsi, Mkurugenzi wa usajili na Uzingatiaji wa PDPC, Stephen Wangwe, amesema ni muhimu watu wakaijua sheria ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, na kwamba kwa kuandika mtu anatoka na kwenda wapi au kabila lake havihusiani na yeye kufikia kwenye nyumba aliyokwenda kulala.

“Unakwenda nyumba ya kulala wageni unaambiwa andika ulikotoka na unakokwenda, kabila lako lakini haya yote ni taarifa binafsi na wanavunja sheria. Au kipindi cha nyuma matokeo ya mitihani yalikuwa yanatangazwa kwa majina, inatakiwa kuweka namba ili kulinda taarifa za mtu,”amesema.

Amesema tangu kuwepo kwa sheria hiyo mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitafuatwa dhidi yake.

Chanzo: Nipashe
 
TUME ya Ulinzi wa Taarifa (PDPC), imesema kuwa unapokwenda nyumba ya kulala wageni hairuhusiwi kuandika ulikotoka na unakokwenda kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya taarifa binafsi.

Akiwasilisha mada ya zana ya taarifa binafsi, Mkurugenzi wa usajili na Uzingatiaji wa PDPC, Stephen Wangwe, amesema ni muhimu watu wakaijua sheria ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, na kwamba kwa kuandika mtu anatoka na kwenda wapi au kabila lake havihusiani na yeye kufikia kwenye nyumba aliyokwenda kulala.

“Unakwenda nyumba ya kulala wageni unaambiwa andika ulikotoka na unakokwenda, kabila lako lakini haya yote ni taarifa binafsi na wanavunja sheria. Au kipindi cha nyuma matokeo ya mitihani yalikuwa yanatangazwa kwa majina, inatakiwa kuweka namba ili kulinda taarifa za mtu,”amesema.

Amesema tangu kuwepo kwa sheria hiyo mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitafuatwa dhidi yake.

Chanzo: Nipashe
Sahihi kabisa.
 
Labda nyota tano mtu ndio ataandika majina yake halisi,lakini hizi mbute lodge hakuna anaeandika jina lake halisi
 
TUME ya Ulinzi wa Taarifa (PDPC), imesema kuwa unapokwenda nyumba ya kulala wageni hairuhusiwi kuandika ulikotoka na unakokwenda kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya taarifa binafsi.

Akiwasilisha mada ya zana ya taarifa binafsi, Mkurugenzi wa usajili na Uzingatiaji wa PDPC, Stephen Wangwe, amesema ni muhimu watu wakaijua sheria ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, na kwamba kwa kuandika mtu anatoka na kwenda wapi au kabila lake havihusiani na yeye kufikia kwenye nyumba aliyokwenda kulala.

“Unakwenda nyumba ya kulala wageni unaambiwa andika ulikotoka na unakokwenda, kabila lako lakini haya yote ni taarifa binafsi na wanavunja sheria. Au kipindi cha nyuma matokeo ya mitihani yalikuwa yanatangazwa kwa majina, inatakiwa kuweka namba ili kulinda taarifa za mtu,”amesema.

Amesema tangu kuwepo kwa sheria hiyo mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitafuatwa dhidi yake.

Chanzo: Nipashe

Ni jambo jema sana hili,
 
Kwani umekatazwa kudanganya ? Haya mambo mbona ni kama complication....

Huenda walioweka hivyo ni basi tu kama ikitokea tatizo umekufa au lolote waweze kusema mdau aliyetokea alipotoka na anakwenda anapokwenda amefia hapa n.k.; Au katika marketing research kufahamu wageni wao wengi ni wa wapi...; Sidhani kama wanakushikia bunduki hata ukidanganya mwanzo mwisho...
 
Wengi Huwa wanaandika uongo,ila kuna uzuri wake,ukikata moto!
Ukifia guest je taarifa zako watakwenda kupata kwa
Wangwe?

Polisi wa Tanzania bado wanafanya kazi zao kizamani Sana Kama vile bado wapo katika zama za mawe za kale, hakuna ukisasa katika Utendaji kazi zao.

Kwenye baadhi ya nchi zilizoendelea katika Sayansi na Teknolojia, sasa hivi Askari Polisi wanatumia Teknolojia za kisasa katika kuwatambua watu, hata wale waliofia mitaani au Gesti/Lodge na kwenye Hoteli ambako Utambulisho wao haujulikani.
Kwenye magari yao ya kufanya Doria huko mitaani, Askari Polisi wamekuwa wakibeba kwenye magari yao hayo Mashine na Mitambo ya Utambuzi wa Watu kwa kutumia Teknolojia ya Fingerprinting, Iris Scanner na Facial Recognition.

Wakiokota maiti ya Mtu ambaye hatambuliki kwa kukosa Kitambulisho chochote kile Cha kumtambua, Basi Polisi wanachofanya wanaiscan hiyo maiti kwenye hizi mashine pale pale kwenye eneo tukio (scene of crime) na kujua Utambulisho wake huyo mtu aliyekufa on the spot katika eneo la tukio.
 
Hili wanatafuta trend tu na watu wajue kuna kitu kama hiki. Kuandika taarifa sahihi kuna saidia mambo mengi.
1. Pale upatapo changamoto unaweza saidika.
2. Ukisahau au kupoteza kitu ndani ya nyumba ya wageni unatafutwa na kurudishiwa kitu chako.
3. Kuna mamlaka zinachukua too mbalimbali za kiserikali huko kwenye nyumba za kulala wageni usipoandika watajuaje mmelala ili wakusanye tozo.
4. Issue za kiusalama kama wafanyavyo polisi na uhamiaji usiku kukagua vyumba na kujua uhalali wa uwepo wako nchini.

Katika hili, napingana nao ila nyie wazinzi ndio mnafurahia.

Binafsi nikisafiri kikazi huwa naandika taatifa za kweli kwenye kitabu cha wageni na huwa nakidaigi ili nisaini kitabu.
 
Polisi wa Tanzania bado wanafanya kazi zao kizamani Sana Kama vile bado wapo katika zama za mawe za kale, hakuna ukisasa katika Utendaji kazi zao.

Kwenye baadhi ya nchi zilizoendelea katika Sayansi na Teknolojia, sasa hivi Askari Polisi wanatumia Teknolojia za kisasa katika kuwatambua watu, hata wale waliofia mitaani au Gesti/Lodge na kwenye Hoteli ambako Utambulisho wao haujulikani.
Kwenye magari yao ya kufanya Doria huko mitaani, Askari Polisi wamekuwa wakibeba kwenye magari yao hayo Mashine na Mitambo ya Utambuzi wa Watu kwa kutumia Teknolojia ya Fingerprinting, Iris Scanner na Facial Recognition.

Wakiokota maiti ya Mtu ambaye hatambuliki kwa kukosa Kitambulisho chochote kile Cha kumtambua, Basi Polisi wanachofanya wanaiscan hiyo maiti kwenye hizi mashine pale pale kwenye eneo tukio (scene of crime) na kujua Utambulisho wake huyo mtu aliyekufa on the spot katika eneo la tukio.
Hatujafika huko
 
TUME ya Ulinzi wa Taarifa (PDPC), imesema kuwa unapokwenda nyumba ya kulala wageni hairuhusiwi kuandika ulikotoka na unakokwenda kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya taarifa binafsi.

Akiwasilisha mada ya zana ya taarifa binafsi, Mkurugenzi wa usajili na Uzingatiaji wa PDPC, Stephen Wangwe, amesema ni muhimu watu wakaijua sheria ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, na kwamba kwa kuandika mtu anatoka na kwenda wapi au kabila lake havihusiani na yeye kufikia kwenye nyumba aliyokwenda kulala.

“Unakwenda nyumba ya kulala wageni unaambiwa andika ulikotoka na unakokwenda, kabila lako lakini haya yote ni taarifa binafsi na wanavunja sheria. Au kipindi cha nyuma matokeo ya mitihani yalikuwa yanatangazwa kwa majina, inatakiwa kuweka namba ili kulinda taarifa za mtu,”amesema.

Amesema tangu kuwepo kwa sheria hiyo mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitafuatwa dhidi yake.

Chanzo: Nipashe
Hii ni sawa kabisa
Nafikiri hawa jamaa wa "tuma kwa namba hii au mganga huyu sijui amenisaidia bila fedha ...."
 
Back
Top Bottom