JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
TUME ya Ulinzi wa Taarifa (PDPC), imesema kuwa unapokwenda nyumba ya kulala wageni hairuhusiwi kuandika ulikotoka na unakokwenda kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya taarifa binafsi.
Akiwasilisha mada ya zana ya taarifa binafsi, Mkurugenzi wa usajili na Uzingatiaji wa PDPC, Stephen Wangwe, amesema ni muhimu watu wakaijua sheria ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, na kwamba kwa kuandika mtu anatoka na kwenda wapi au kabila lake havihusiani na yeye kufikia kwenye nyumba aliyokwenda kulala.
“Unakwenda nyumba ya kulala wageni unaambiwa andika ulikotoka na unakokwenda, kabila lako lakini haya yote ni taarifa binafsi na wanavunja sheria. Au kipindi cha nyuma matokeo ya mitihani yalikuwa yanatangazwa kwa majina, inatakiwa kuweka namba ili kulinda taarifa za mtu,”amesema.
Amesema tangu kuwepo kwa sheria hiyo mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitafuatwa dhidi yake.
Chanzo: Nipashe
Akiwasilisha mada ya zana ya taarifa binafsi, Mkurugenzi wa usajili na Uzingatiaji wa PDPC, Stephen Wangwe, amesema ni muhimu watu wakaijua sheria ili kuepuka kuingia kwenye matatizo, na kwamba kwa kuandika mtu anatoka na kwenda wapi au kabila lake havihusiani na yeye kufikia kwenye nyumba aliyokwenda kulala.
“Unakwenda nyumba ya kulala wageni unaambiwa andika ulikotoka na unakokwenda, kabila lako lakini haya yote ni taarifa binafsi na wanavunja sheria. Au kipindi cha nyuma matokeo ya mitihani yalikuwa yanatangazwa kwa majina, inatakiwa kuweka namba ili kulinda taarifa za mtu,”amesema.
Amesema tangu kuwepo kwa sheria hiyo mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitafuatwa dhidi yake.
Chanzo: Nipashe