PDPC: Ukifika nyumba ya Kulala Wageni, marufuku kuandika unapotoka na unapokwenda

PDPC: Ukifika nyumba ya Kulala Wageni, marufuku kuandika unapotoka na unapokwenda

Hili wanatafuta trend tu na watu wajue kuna kitu kama hiki. Kuandika taarifa sahihi kuna saidia mambo mengi.
1. Pale upatapo changamoto unaweza saidika.
2. Ukisahau au kupoteza kitu ndani ya nyumba ya wageni unatafutwa na kurudishiwa kitu chako.
3. Kuna mamlaka zinachukua too mbalimbali za kiserikali huko kwenye nyumba za kulala wageni usipoandika watajuaje mmelala ili wakusanye tozo.
4. Issue za kiusalama kama wafanyavyo polisi na uhamiaji usiku kukagua vyumba na kujua uhalali wa uwepo wako nchini.

Katika hili, napingana nao ila nyie wazinzi ndio mnafurahia.

Binafsi nikisafiri kikazi huwa naandika taatifa za kweli kwenye kitabu cha wageni na huwa nakidaigi ili nisaini kitabu.

Zipo faida na hasara zake katika kufanya hivyo. Kwenye Nchi nyingi sana ambazo hakuna Demokrasia ya kutosha na Utawala wa Sheria kama hizi Nchi zetu za kiAfrika, jambo hili Lina hasara nyingi zaidi kuliko faida. Kama umeshawahi kufika na kulala Gesti, Lodge, au Hotelini katika nchi kama vile Zimbabwe, Rwanda, Urusi, na Nchi zingine zinazofanana na hizo, nafikiri utakuwa unanielewa vizuri Sana ninachomaanisha hapa.
Wale Watu ambao ni maarufu katika Jamii ndio wenye hatari kubwa zaidi kuhusiana na suala hili.
Nchini Rwanda kuna Watu wanaojulikana Sana na wenyeji wa huko wanaitwa kwa jina la "SEPO," na nchini Zimbabwe na pia nchini Urusi kuna Kitu kinaitwa "Operation Midnights."
So, take a great care to disclose your identity in those areas where you are there!
 
Kwanza kitabu cha wageni kilitakiwa kitumike mara moja tu kwa siku badala ya kitabu kimoja kutumika mwaka mzima.
 
Hatujafika huko

Tunaweza kabisa, kwa sababu NIDA tayari wameshachukua taarifa za Watu wengi Sana mpaka sasa hivi (Biometric Data). Hata Uhamiaji nao tayari wanayo Database kubwa sana ya taarifa za Watu.
Kikwazo kikubwa Sana ninachokiona Mimi ni kwamba katika Nchi zetu hizi za kiAfrika tuna bahati mbaya sana ya kuwa na Watawala wa nchi ambao hawana Maono yoyote yale, Watawala wapo wapo tu.

The problem of Africans is that those with ideas have no power, and those with power have no ideas!
 
Hivi Tanzania hakuna Sheria au utaratibu wa kuingia na ID .guest au lodge ?
 
Kwanza kitabu cha wageni kilitakiwa kitumike mara moja tu kwa siku badala ya kitabu kimoja kutumika mwaka mzima.
Sawa sawa, nchi km DRC , Burundi na Rwanda huwa vinakaguliwaga na Serikali
 
Hivi nimefika ugenini saa 12 asubuhi, nimepewa chumba lodge halafu inafika saa nne mnanigongea kusema muda wangu umeisha...kweli?!
Hiyo haikupaswa kuwa hivyo! Ungewapiga makofi! Na wewe ulikubalije wakutoze kwa siku ya Jana?
 
Amesahau Kuna wale jamaa wa doria huwa wanapita kukagua vitabu na majina yaendane na vitambulisho
 
Back
Top Bottom