Godblessme
Member
- Aug 5, 2014
- 22
- 3
Habari wapendwa. Nimeugua tumbo chini ya kitovu toka mwaka Jana august .kila nikienda hospitali naambiwa uti , nimepimwa magonjwa ya zinaa hayakuonekana, ukimwi hakuna, na kansa ya kizazi hakuna, ila baadae nilionekana na chronic cervicitis, nimetumia dawa Kali kama clavam, tazabactam sindano (sina hakika na herufi) muvera,dazolic na wala Sikupata nafuu. Nimefanya ultrasound tano hospitali tofauti mbili zilionesha vivimbe vidogo vya 2 cm kwenye ovary. Mwezi June mwaka huu nimefanya CT scan, nikaambiwa bulky uterus, left adnexa appears bulky, lesion on right adnexa and free fluid on pouch of Douglas. Docta haoni kama ni tatizo kubwa na wala hakunipa Dawa. Nikaenda muhimbili nikaambiwa nifanye Hsg. Nimeshafanya juzi il a sijarudi kwa dactari kwasababu ya weekend. Hsg inasema loculated spillage suggest pelvic fibrosis. Je haya magonjwa ndiyo chanzo cha ugumba ? Na je yanatibikaje? Nisaidieni Tafadhali natafuta mtoto na maumivu yaondoke. Very sorry for a long thread and thank you for your support, advice etc.