Pemba kunahitajika zaidi elimu ya uzazi wa mpango, Watoto wanateseka

Pemba kunahitajika zaidi elimu ya uzazi wa mpango, Watoto wanateseka

Thabit Madai

Member
Joined
Oct 8, 2024
Posts
54
Reaction score
140
IMG-20241009-WA0050.jpg



Naandika andiko hili fupi nikiwa Unguja - Zanzibar baada ya safari ya takribani Wiki Mbili nikiwa kisiwani Pemba.

Mimi ni Mwandishi wa habari na nimepata bahati ya kutembelea maeneo mengi Tanzania bara na Visiwani ila nilichokikuta Pemba bado kinanijastaajabisha hadi sasa naandika andiko hili.

Hivi unaweza kujiuliza kwa karne hii na uchumi tuliokuwa nao kuna Mwanamke anazaa watoto Wanne, Watano na hata Sita huku akiwa hajafika hata miaka 30.

Wacha nikusanue kidogo nilipokuwa Pemba nilitembea mitaani na nilichokigundua kuwa Wanawake wengi hawajui chochote kuhusu uzazi wa mpango, hawajui hata mensturation cycle inafanyaje kazimama mtu mzima hajui tarehe yake ya kuwa hedhini, hajui siku za hatari na salama ni zipi.


IMG-20241009-WA0051.jpg


Kwa wale wachache ambao wanauelewa kuhusu uzazi wa Mpango na faida zake anakumbana na mitazamo potofu ya watu wanaomzunguka kwamba hana uwelewa wa masuala ya Dini.

Nilipokuwa Pale Wawi ndio nilichoka zaidi nilikutana na Mama ana mimba, amembeba mtoto hajafika hata miaka 2 lakini mkononi anamtoto mwingine ambae kwa kukisia ana miaka Mitatu au Minne.

Nipomhadisia mwenyeji wangu aliniambia mbona ni jambo la kawaida tuu akanieleza kwamba huku unaweza kuona mama na binti yake wanakutana labor.


Anasema kuwa Mama ana mtoto wa miezi mitatu tayari ana mimba kabla hajakaa sawa bint yake ana mimba sasa hapo unakuta mama ananyonyesha na binti yake ananyonyesha.

Mjomba na Mpwa wake wanaumri sawa au Mpwa mkubwa kuliko Mjomba hata ile heshima tena inakuwa haipo tena.

Naiomba Serikali na hataa Mashirika binafsi kuongeza nguvu katika kutoa Elimu ya umuhimu wa Uzazi wa Mpango

Sheria itungwe juu ukomo wa kuzaa

Serikali iangalie kwa jicho la pekee kisiwa cha Pemba na kuongeza kasi ya kukifungua Kisiwa cha Pemba kiuchumi ili watu wawe na shughuli za kufanya na kuacha kuingia mdani mapema na kufyatua Watoto.

Picha kwa Hisani ya Mitandao ya Kijamii, BBC na ripoti juu ya Uzazi wa Mpango
IMG-20241009-WA0052.jpg
 
Wewe umetokea Ulaya au Tanzania? mbona hiyo ni hali kwotekwote Tanzania bara neenda Simiyu, Ukerewe Karagwe Tanga Geita Musoma nk child mothers ni wengi sana,

Mwanamke moja ana watoto 7, 8 mpaka 12, na hali yao ya uchumi mbaya hata kuliko ya wa pemba, usukumani kukuta mwanamke wa miaka 17 kua na watoto wawili na miba ni kawaida sanaa.
 
Baraka kutoka kwa Mungu:

Katika Zaburi 127:3, inasema, "Tazama, watoto ni urithi wa BWANA, na matunda ya tumbo ni thawabu." Hii inaonyesha kwamba watoto ni baraka kutoka kwa Mungu, na kuzaa watoto wengi ni ishara ya wema na neema ya Mungu.Kuimarisha familia: Kuwa na watoto wengi kunaweza kusaidia kuimarisha familia na kujenga uhusiano mzuri miongoni mwa wanachama wa familia.

Katika Mwanzo 1:28, Mungu aliwaambia wanadamu wazidishe na kujaza dunia, ambayo inaonyesha umuhimu wa uzazi katika kuimarisha jamii.
View attachment 3119663


Naandika andiko hili fupi nikiwa Unguja - Zanzibar baada ya safari ya takribani Wiki Mbili nikiwa kisiwani Pemba.

Mimi ni Mwandishi wa habari na nimepata bahati ya kutembelea maeneo mengi Tanzania bara na Visiwani ila nilichokikuta Pemba bado kinanijastaajabisha hadi sasa naandika andiko hili.

Hivi unaweza kujiuliza kwa karne hii na uchumi tuliokuwa nao kuna Mwanamke anazaa watoto Wanne, Watano na hata Sita huku akiwa hajafika hata miaka 30.

Wacha nikusanue kidogo nilipokuwa Pemba nilitembea mitaani na nilichokigundua kuwa Wanawake wengi hawajui chochote kuhusu uzazi wa mpango, hawajui hata mensturation cycle inafanyaje kazimama mtu mzima hajui tarehe yake ya kuwa hedhini, hajui siku za hatari na salama ni zipi.


View attachment 3119664

Kwa wale wachache ambao wanauelewa kuhusu uzazi wa Mpango na faida zake anakumbana na mitazamo potofu ya watu wanaomzunguka kwamba hana uwelewa wa masuala ya Dini.

Nilipokuwa Pale Wawi ndio nilichoka zaidi nilikutana na Mama ana mimba, amembeba mtoto hajafika hata miaka 2 lakini mkononi anamtoto mwingine ambae kwa kukisia ana miaka Mitatu au Minne.

Nipomhadisia mwenyeji wangu aliniambia mbona ni jambo la kawaida tuu akanieleza kwamba huku unaweza kuona mama na binti yake wanakutana labor.


Anasema kuwa Mama ana mtoto wa miezi mitatu tayari ana mimba kabla hajakaa sawa bint yake ana mimba sasa hapo unakuta mama ananyonyesha na binti yake ananyonyesha.

Mjomba na Mpwa wake wanaumri sawa au Mpwa mkubwa kuliko Mjomba hata ile heshima tena inakuwa haipo tena.

Naiomba Serikali na hataa Mashirika binafsi kuongeza nguvu katika kutoa Elimu ya umuhimu wa Uzazi wa Mpango

Sheria itungwe juu ukomo wa kuzaa

Serikali iangalie kwa jicho la pekee kisiwa cha Pemba na kuongeza kasi ya kukifungua Kisiwa cha Pemba kiuchumi ili watu wawe na shughuli za kufanya na kuacha kuingia mdani mapema na kufyatua Watoto.

Picha kwa Hisani ya Mitandao ya Kijamii, BBC na ripoti juu ya Uzazi wa Mpango
View attachment 3119666
 
Kwa kuongezea tu mie wa mjjjinnniii mjjiiniii na nna watano, na naona hawajatosha, lengo nlitamani nipate hata 10. Napenda wtt hatariii
 
Mkunaji mpemba akishavaa msuli wake na ndani akipulizwa na upepo wa bakhari akitoka akirudi imo, akienda markiti akirudi imo, akienda kuangalia mpira akirudi imooo, na vile wake zao hawaruhusiwi kutoka nyumbani kwenda popote sio gengeni wala markiti. Wanapewa amri ya kubaki nyumbani na kujiremba kujichora hina ili mume akirudi wampe wampe tena halafu wanaiomba tena kama kina Aucho🤣🤣🤣
 
Kwa kuongezea tu mie wa mjjjinnniii mjjiiniii na nna watano, na naona hawajatosha, lengo nlitamani nipate hata 10. Napenda wtt hatariii
Kikubwa uweze kuwahudimia, mambo ya kuleta viumbe kibao afu hata mavazi tu ni tatizo hiyo ndo noma..

Huko ughaibuni pia wapo wenye watoto kibao hata 30+ ila wenzetu wana namna nzuri ya kuzitunza familia za namna hiyo hadi kuandaa documentaries kuwahusu huku maokoto yakiingia kwa familia.
 
Kikubwa uweze kuwahudimia, mambo ya kuleta viumbe kibao afu hata mavazi tu ni tatizo hiyo ndo noma..

Huko ughaibuni pia wapo wenye watoto kibao hata 30+ ila wenzetu wana namna nzuri ya kuzitunza familia za namna hiyo hadi kuandaa documentaries kuwahusu huku maokoto yakiingia kwa familia.
Shida kuzalisha kizazi ambacho Duni sana Pemba licha ya kuwa na neema ya vyakula vya Asili lakini maisha yapo Duni hali ya kiuchumi ni ngumu sana
 
endeleeni kuzaa tupate waendesha bajaji na mabodaboda wengi nchini.

Tunahitaji wachimba mitaro, wajenzi, na mafundi mchundo. ZAENI KWELI KWELI.

Tunahitaji watumwa wengi katika taifa, wafanya kazi, na wanunuzi wa bidhaa.
 
Back
Top Bottom