Pemba: Polisi wachunguza vifo vya watu wawili waliofariki dunia wakipatiwa matibabu hospitali ya Ali Khamis Camp

Pemba: Polisi wachunguza vifo vya watu wawili waliofariki dunia wakipatiwa matibabu hospitali ya Ali Khamis Camp

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
photo_2024-12-26_14-38-01.jpg

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba linafanya uchunguzi wa vifo vya watu wawili ambao walifariki dunia wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali ya Ali Khamis Camp Vitongoji Chake Chake Pemba.

Watu hao ni:

  1. Othman Hamad Othman miaka 75 mshirazí na mkazi wa Kimango-Kiungoni Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.
  2. Amour Salim Khamis miaka 28 mshirazí na mkazi wa Kimango-Kiungoni Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Awali watu hao walikamatwa na maafisa wa mamlaka ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya Pemba wakiwa wanatuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya.

Uchunguzi huo unaendelea kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali pamoja na walioshuhudia ukamatwaji wa watu hao.
 
Back
Top Bottom