KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,187
- 17,167
Mkuu 'Joselela,' sasa naona tatizo lako lilipo. Hujui maana ya "vitu feki" ni nini.Feki hapana aisee niambie ni less-quality ambao huletwa kulingana na hali za kiuchumi za wananchi zilivyo.
'Definition' isiyochanganya mtu yeyote kuhusu hayo unayoyasema hapa ni rahisi.Mkuu nadhani hapa mnachanganya kidogo kwa kutumia neno 'fake'.. kimsingi hizi bidhaa nyingi zinazouzwa cheap sio fake.. ni bidhaa za grade iliyo chini ya ile grade ya juu.
Inapaswa serikali iweke clear guideline ili mnunuzi awe anajua wakati ananunua kama bidhaa ni highest quality, medium au low quality. Inataka tu usimamizi ili watu wapate huduma kulingana na level zao za kiuchumi.
Muhimu tu serikali iangalize yale maeneo sensitive sana wasiruhusu bidhaa ambazo ni medium au low quality.
Umachinga hauwezi kuisha maana hata dunia ya kwanza wametengewa maeneo yao. Dawa ni kutenga maeneo vijengwe vibanda designed kwa kuchukua nafasi ndogo halafu wapewe kwa bei rahisi hata kama watalipa elfu 30 kwa mwezi.Ukweli ni kwamba umachinga ni tatizo na unatakiwa kuisha kabisa. Watu wawe na maduka na walipe kodi badala ya huu utaratibu wa kuwa na vibanda nje ya maduka na hawalipi kodi. Huu sio utaratibu mzuri wa kutoa ajira na kiukweli wanao nufaika ni waingizaji wa vitu wasiolipa kodi sio hawa vijana. Viwanda, Uvuvi, ufugaji na Kilimo ndiyo suluhisho la vijana.
Vyuo vya veta vitumike kutoa elimu ya hivi vitu. Wamachinga wanachangia uchafuzi mkubwa wa mazingira, kuharibu mipangilio ya miji na kuongoza kwa kuuza vitu fake.
Jangwani ni sehemu yenye mafuriko na mikondo ya maji inatakiwa kutengenezwa kama sehemu ya kupumzika wamachinga wataishia kupafanya jalala pale na mvua ikija uchafu wote utaishia kwenye mkondo wa maji na mito.
Mwamposa atatangaza mfungo wa kupinga hiliHapana pale panajaa maji wawapeleke kawe Tanganyika Packers pana eneo kubwa la uwanja ni pazuri vipindi vyote watafanya kazi
Watu kama hawa Nyerere aliwapeleka Gezaulole wakalime.Wanabodi,
Ni dhahiri kwamba ipo changamoto kubwa sana ya wafanyabiashara hawa wadogo pale Kariakoo. Wamekuwa wengi mno na kusababisha adha kubwa sana kwa wenye maduka na wateja waendapo kupata huduma.
Ninapendekeza eneo lote la jangwani painuliwe, pajengwe vizuri na kuwekewa vibanda modern ambapo machinga wa pale kariakoo wapangishwe kwa malipo nafuu ili waweze kuendelea na kujikimu kimaisha.
Lile eneo ni zuri kwasababu lipo katikati ya mji, ni karibu na mahali watakapopata bidhaa (yaani maduka ya Kariakoo) na ni rahisi kwa wateja kuweza kuwafikia.
Ujenzi wa pale jangwani wala hauwezi kuwa complicated ikiwa ile mito mitatu itachimbwa na kujengewa vizuri ili ipitishe maji.
Muhimu tu ile mito ijengwe vizuri kwa plan ya kuwa njia ya usafirishaji kwa miaka ijayo. Ule mto unaweza kuchimbwa kutoka pale selander mpaka mbezi na kuvuta maji ya bahari ili kuwe na boti za abiria na utalii. Hii teknolojia ipo, nimeiona pale Dubai na Thailand.
Nawasilisha.
Mkuu kwa sasa mambo ya ujamaa kuwapeleka watu mashambani haifai tena. Hawa watu wana umuhimu wao katika mazingira tuliyonayo.Watu kama hawa Nyerere aliwapeleka Gezaulole wakalime.
Siyo kuwapa maeneo ya wazi ili wayachafue. Ni wengi na wataongezeka kila kukicha kila mji!
Yule aiyekuwa waziri wa elimu Mulugo amesema vijana milioni 1.8 wanamakiza shule za msingi next year. Unataka waje jangwani pia?
Tena hili siyo tatizo linaloweza kutatuliwa na team za ma RC na DC tunaoletewa. Wazecha- karata! ( Opportunists)
Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
Wapelekwe machinga complex kariakoo bei zishushweMkuu kwa sasa mambo ya ujamaa kuwapeleka watu mashambani haifai tena. Hawa watu wana umuhimu wao katika mazingira tuliyonayo.
Pia kwa sasa inatakiwa suluhisho kwa tatizo lililopo wakati inatafutwa solution ya muda mrefu.
Wajengewe vyoo kuingia sh 200, pia kuwe na mapipa ya uchafuHao sio wasitaarabu,huo mto utakuwa wakijani ndio utaziba kabisa
Pale kawe pia panaweza kutumika na panafikika kirahisi. Ninakuunga mkono ili hapo pia paboreshwe kwa kujengwa modern booths ili hawa ndugu zetu pia waendelee kujikimu kimaisha.Hapana pale panajaa maji wawapeleke kawe Tanganyika Packers pana eneo kubwa la uwanja ni pazuri vipindi vyote watafanya kazi
Pia pawepo na stand ya mabasiPale kawe pia panaweza kutumika na panafikika kirahisi. Ninakuunga mkono ili hapo pia paboreshwe kwa kujengwa modern booths ili hawa ndugu zetu pia waendelee kujikimu kimaisha.
Hayo maeneo mawili ya jangwani na tanganyika packers yanaweza kusaidia sana kupunguza wamachinga kwenye barabara.