Pendekezo: Kiswahili kitumike kama lugha ya kufundishia ngazi zote za elimu, ili tukomboke kifikra

Pendekezo: Kiswahili kitumike kama lugha ya kufundishia ngazi zote za elimu, ili tukomboke kifikra

Kidagaa kimemwozea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
3,680
Reaction score
6,554
Huu ndio wakati wa kuanza kutumia lugha ya Kiswahili kufundishia katika ngazi zote za elimu nchini

Pamoja na Kiswahili kupitishwa na Sera ya elimu mwaka 2014 bado hakijaanza kutumika kufundishia masomo katika elimu ya upili na elimu ya juu.

Sera ya Elimu ya mwaka 2014 inasema Kiswahili pamoja na kingereza zitakuwa ni lugha za kufundishia kuanzia elimu ya awali hadi elimu ya juu, lakini takribani miaka 6 imepita bila suala hilo kutekelezwa.

Tafiti nyingi zilizofanywa zilionesha kuwa lugha ambayo unaweza kuwapa maarifa na kuwafanya wanafunzi kuwa wavumbuzi ni kiswahili (rejea utafiti wa Mzee Makweta) licha ya tafiti kuonesha kuwa Kiswahili kilifaa kutumika kufundishia bado wadau wamekuwa wakilegalega kutoa maamuzi.

Mwaka 1991 ilikuwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuanza kufundishia masomo yote kwa Kiswahili lakini ilishindikana kutokana na ugumu wa kufanya maamuzi badala yake wakaishia kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya mawasiliano rasmi chuoni hapo.

Wapo baadhi ya watu pamoja na wataalam wengine wasio fuatilia mambo na kufanya uchunguzi wanaobeba madai yasiyokuwa ya kweli kuwa hakuna vitabu!

Mwaka 1972 vitabu vya Kemia na Baiolojia vya Lambert na Habort vilitafsiriwa na kuwa kwa Kiswahili kama mataifa mengine ya ulaya yalivyotafsiri vitabu hivi kuwa katika lugha zao.

Pamoja na hayo kwa sasa kuna vitabu vya Kiswahili vya sekondari vya Historia, Biolojia, kemia, fizikia, Geografia nk. Vilivyoandikwa kwa kiswahili.

Kiswahili kinavyoweza kutumika kufundishia masomo yote
Kiswahili kinaweza kuwa lugha ya kupitishia maarifa huku lugha ya Kingereza na lugha nyinginezo zifundishwe kama kozi ya lazima kuanzia awali hadi vyuo vikuu kuliko kingereza cha sasa kinachofundishwa kama somo na kutofuata kanuni zozote za ufundishaji lugha ya kigeni.

MKAZO
Hakuna nchi yeyote yenye maendeleo ya kweli kwa kutumika lugha ya watu wengine, kwasababu lugha ni uchumi Na ukitaka kukuza lugha yako lazima ukuze uchumi na hatimaye lugha hukuza uchumi.

Mkosi ulipoanzia, kama asemavyo profesa Mbaabu (2007), kuchapishwa kwa Kitabu cha African Education (1953) pamoja na mkutano wa elimu ya kiafrika 1953, mkutano ambao uliripoti kuwa kuchapishwa kwa African education ni hatua mkubwa katika mabadiliko ya sera ya uingereza kuhusu elimu ya Africa hasa afrika mashariki.

Kitabu hicho kilipendekeza kwamba, kusomeshwa kwa kiswahili kukomeshwe kwa sababu ndicho kizuizi kikubwa dhidi ya maendeleo ya kingereza. Serikali ya uingereza ilikuwa tayari kuanzisha mabadiliko yeyote ambayo yangesaidia kukabiliana na mwamko wa uzalendo wa Mwafrika ambao uliyatishia mamlaka ya kikoloni kwa kupigania uhuru.

Kuondolewa kwa kiswahili kungepunguza uwezekano wa mawasiliano kati ya makabila na kungesaisia kuua mwamko na mtazami wa kitaifa kati ya RAIA.

Jambo hilo lingehakikisha kwamba uingereza ingeendelea kuathiri nchi hizo hata baada ya uhuru ( Mbaabu I.(2007) Historia ya usanifishaji wa kiswahili)

Hitimisho
Ni wakati sasa wa kuahamisha maarifa yaliyomo katika lugha nyingine na kuyahamisha katika lugha ya Kiswahili na kisha kujifunza maarifa hayo kwa lugha yetu kama walivyofanya kisumeri kwenda kiakadi 2350kk, na Kigiriki kwenda Kiingereza- Kijerumani-Kfaransa nk.
 
Kiswahili kitumike KUFUNDISHIA NINI? Yani mnatakaje Mjifunze kiingereza kwa kutumia Kiswahili au mjifunze Kiswahili kwa Kiswahili?

Lugha hii haijajitosheleza, kuna misamiati mingi sana ya kitaaluma haina maneno mbadala ya Kiswahili au hayana Kiswahili chake. Hii ni taaluma zote, Mnaweza kusema fizikia, kemia, hata engineering au Medicine na famasia.

Tatizo lenu nini lakini, Mimi pia sikijui kiinglishi lakini naona kimesha dominate eneo hili la kufundishia, kwanini tusibaki tulivyo na badala yake mnataka tubadilishe?

Mtafaidika na nini kwa kutumia Kiswahili?

Maaana ninavyofahamu mimi kuna wananchi weengi pia wasiokifahamu Kiswahili kwa ufasaha, tutafika shule tena tutaanza kufundishana Kiswahili fasaha cha kujifunzia.

Iko siku atakuja kiongozi naye Kiswahili hakiwezi au hakimudu, atasema anapendekeza tutumie KIHA, KIKWAYA, KIJITA,KISUKUMA,AU KICHAGA kufundishia na wote mtafuata mkumbo.

Tutafute faida za kujifunzi kwa Kiswahili kwanza tuone kama zipo na ,kama zina mashiko.

Fanyeni hata Pilot study ya wanafunzi kumi kuanzia primary hadi chuo kikuu kisha muone mafanikio yao au majuto yao kwa kutumia lugha hiyo kuwafundisha.

Tusianze tu kama gwaride, mbele tembea bila sababu, au nyuma geuka bila sababu. Tuwe na sababu ya kufanya hivyo mnavyotaka.
 
Kama jamaa yenu hajui ung'eng'e mpelekeni kwa ras simba akapigwe twisheni.

This is not a national problem. Let him solve his shortcomings on his own. .

Shida yake ya kushindwa Kiingereza isilete laana kwa future ya watoto wetu. Tunawatakia mema watoto wetu!

Yeye kama anakipenda Kiswahili aajiri walimu wamfundishe hapo magogoni maana hata chenyewe kinamshinda pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MASSHELE,
Tatizo moja watu wengi hawajua hata ni kwanini Kiswahili
Hakitumiki ngoja nimkupe sababu ya ukweli hapa. Elimu ya juu inahitaji publication nyingi yaani vitabu vingi, maoni ya kimasomo n.k.

Hakuna publication za kutosha kwa kiswahili na wala hatuna utaratibu wa kutafsiri vitabu vya lugha nyingine kwa kiswahili. Sasa tujiulize kama hujui kiingeeza na hatufundishi wanafunzi wa PHD wataaoma vipi vitabu. PHD inahitaji mtu kusoma vitabu 90 sasa jiulize kama hujui kiingereza utasoma vipi.

Kuna nchi ambazo wana technologia za kufasiri au kama app za kutafsiri lakini vitu kama hivi inabidi viwekwe sawa kabla ya kubadilisha lugha yote. Vilevile tijue kiswahili cha mtaani sio sawa na cha darasani ukienda kuangalia watu waliochukua masoma A - level kiswahili ni kigumu kuliko hata kiingereza.
 
..tunatakiwa tuongeze nguvu ktk kufundisha Kiingereza.

..wahitimu wa Tz wanaonekana hawana weledi wanapokutana na wenzao toka nchi zinazotilia mkazo lugha ya Kiingereza.

..niliangalia mkutano wa nchi za SADC na maofisa toka waTz walikuwa wanatia huruma kutokana kutoimudu lugha ya Kiingereza.
 
MASSHELE,
Naunga mkono hoja ! Tatizo ni vijana wetu na huu utandawazi, hawakitaki kiswahili ! Wanataka kiendelee kuwa lugha ya pass time tuu na ya kuwasalimia wazee halafu ung'eng'e (wasio ujua fasaha) ndio utumike kwenye shule na vyuo na wanapokutana mitaani , disco na mitandaoni ! Kuna generational gap hapa na ni ngumu sana kuzibika tokana na utandawazi !
 
..tunatakiwa tuongeze nguvu ktk kufundisha Kiingereza.

..wahitimu wa Tz wanaonekana hawana weledi wanapokutana na wenzao toka nchi zinazotilia mkazo lugha ya Kiingereza.

..niliangalia mkutano wa nchi za SADC na maofisa toka waTz walikuwa wanatia huruma kutokana kutoimudu lugha ya Kiingereza.
Tunatakiwa tuongeze nguvu sana ya kuhimiza na kufundisha kiswahili fasaha sambamba na kiingereza! Huko mikutanoni tunatakiwa kuwa na wakalimani wa kutosha na mahiri sana ! Lugha ya kiswahili ni tamu sana ! Ninafurahishwa sana ninaposikiliza radio zetu hasa FM zilizo ajili vijana kabisa wenye kukitamalaki kiswahili sawia! Kwa kweli wanajitahidi sana kuongea kiswahili fasaha tofauti na kiswahili cha mtaani !

Mjerumani hazungumzi kiingereza mikutanoni japo anakijua vema ! Mchina, mjapani , mrusi, mswidi, mkorea, mfaransa, mwarabu..na mataifa mengi tuu mbona wanazungumza lugha zao mpaka UN ??

kwa sasa lugha ya kiswahili imeshakua sana na msamiati umeongezeka kukidhi haja ya ulinganifu na lugha nyingine, yawezekana bado kuna upungufu kiasi fulani lakini hii isiwe sababu ya kutokukitumia kimataifa.

Ikiwa sisi watanzania tuna buruza miguu katika matumizi ya lugha ya kiswahili ilhali duniani kote tunatambulika kama ndio taifa chimbuko la hii lugha vipi mataifa mengine hususan ya Afrika yakienzi ? Kasumba ya kikoloni ni mbaya sana ! Kuna hatari ya vizazi vijavyo vya watanzania kupoteza misamiati ya lugha hii adhimu ya kiswahili waje waanze kufundishwa na wanyarwanda na wakenya ambao kwa sasa wanatilia mkazo sana kujifunza lugha hii mpka kiwango cha chuo kikuu.

Tukumbuke enzi tunasoma riwaya dahali ya miaka iliyopita ! Vitabu vya waandishi nguli kama Shaaban Robert, Shafi Adam Shafi, Penina Mhando, (prof. Penina Mlama), William Semzaba na wengine wengi ! Nini kilikwenda mrama hadi leo hii watanzania wapoteza hamu ya lugha yao ? Tuna jambo la kufanya sisi kama watanzania kurudisha munkari na hamu ya lugha yetu.

Binafsi ningependelea kuona na kusikia runinga na radio zetu zinakua na vipindi maalum vya kufundisha, kuichambua ba kuhamasisha matumizi ya lugha fasaha ya kiswahili.

Wakatabahu, JMS
 
Unawafundishia kiswahili alafu baada hapo utawatumiaje wakati huna teknolojia

Sent using Jamii Forums mobile app
Exactly, na huo ni mtego wa viongozi wetu kwa sisi wa hali za kawaida, kama hili lingekuwa wazo zuri basi watunga sera wangeisha maliza na kulitekeleza siku nyingi, watunga sera wakati wanapeleka watoto wao ulaya ili kuwapa exposure za uko sisi tunakuja na wazo la oooh kiswahili ndiyo kiwe kila kitu.
Hacheni mawazo hayo.
 
Kwa Nini English medium ukiangalia matokeo somo la kiswahili wameongoza kitaifa kwa ufaulu kuliko shule za Swahili medium.Ushahidi Angalia matokeo ya shule za msingi ya miaka mitano 2014 Hadi 2019
 
Hata kiingereza kilipata upinzani kilipotaka kutumika kwenye sayansi,watu waliona bado hakijitoshelezi.
Sio kweli
Upinzani ulikuwa kwenye dini tu .Na ulitoka Roma ambao walitaka kusali kitumike kilatini tu dunia nzima sababu lugha zingine haxijitoshelezi kwa maneno ya kitheolojia.

Mfalme James wa uingereza akapinga .Akatafsiri Hadi Biblia kwa kiingereza na kuanza kusali kiingereza na kuachana na kilatini kwa nguvu

Ndio Hadi Leo tuna Biblia ya King James version

Wazee wengi Hata Tanzania walikuwa wakisali kwa kilatini .mapadre vijana nao wakagoma kusali kilatini kiswahili kikakubalika Kama lugha ya Sala katoliki pia
 
Wanangu siwezi wafundisha kiswahili Mimi sijaona faida take! Kalugha ka kuunga unga kako kwa ajili ya kujazana ubishi tu. Hivi taaluma za kuunda meli, ndege, udaktari nk utatumua kiswahili gani kuwaelewesha wanafunzi? Hebu tuache ujinga basi!
 
Back
Top Bottom